Mbrazil
Marcio Maximo hakuwa na mahusiano mazuri na Juma Kaseja mwaka 2007
alipokuwa anaifundisha Taifa Stars, lakini sasa amesema kazi inatakiwa
kundelea Yanga kama kawaida na kusahau yaliyopita.
KOCHA
Mbrazil, Marcio Maximo na msaidizi wake Leonadro Neiva wanatarajia
kuanza kazi rasmi jumatatu baada ya kumwanga wino kuitumika Yanga sc
kwa mkataba wa miaka miwili.
Jana
Maximo na mwenzake Neiva walikuwa na mkutano na waandishi wa habari
makao makuu ya Yanga, makutano ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, jijini
Dar es salaam ambapo walieleza malengo yao na kujibu maswali ya
wanahabari.
Ulikuwa
mkutano mzuri na muhimu kwa wanamichezo, kwasababu walikuwa na kiu ya
kujua nini Maximo ataongea kwa mara ya kwanza baada ya kurudi nchini,
safari hii ikiwa ni Yanga na sio majukumu ya kitaifa.
Moja ya
mambo aliyosema Maximo ni kufurahia kurudi Tanzania, iliwasifu
watanzania kwa kuwa wakarimu, wapenda mpira na akaahidi kufanya kazi kwa
ueledi mkubwa.
Pili
Maximo hakusita kutoa shukurani zake kwa viongozi wa Yanga kwasababu
wamemuamini na kumpa nafasi hiyo muhimu. Alikiri kufuatwa kwa awamu tatu
mfufulizo, lakini safari hii akaona bora akubali.
Kitu
ambacho wengi walisubiri kusikia kutoka kwa Mbrazil huyu mwenye heshima
kubwa nchini, nikiwemo mimi, ni mipango yake ya kuifanya Yanga kuwa
bora.
Maximo
alipata fursa ya kueleza mipango yake ambapo alisema anatarajia kuanza
kazi moja kwa moja siku ya jumatatu pamoja na msaidizi wake Neiva kwa
kushirikiana na kocha wa kikosi cha U-20.
Alisema ataanza na wachezaji waliopo na wachezaji wa kikosi cha U20 ambapo watakua wakifanya mazoezi pamoja.
“Natambua
tuna wachezaji wengi katika timu za Taifa mbalimbali ikiwemo ya
Tanzania (Taifa Stars), Uganda (The Cranes) na Rwanda (Amavubi) ambao
wapo wanayatumikia mataifa yao, na punde watakapomaliza majukumu hayo
wataungana nasi kwa maandalizi”
No comments:
Post a Comment