Wednesday, June 25, 2014

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YAANZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KWA MFUMO MPYA WA BVR

??????????????????????????????? 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi hapa nchini Jaji Mstaafu Damian Lubuva (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jana, kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Liana Hassan na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Joseph Mchina.
Na Hillary Shoo, SINGIDA. 
TUME ya Taifa ya Uchaguzi imeanza mchakato wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura,kwa kuwashirikisha kwa karibu waandishi wa habari hapa nchini. 
Lengo la kuwashirikisha waandishi wa habari ni kutokana na uwezo na hekima katika kupeleka taarifa na kuhamasisha jamii na wananchi kwa ujumla kupitia vyombo vya habari.
 
Hayo yamebainisha jana mjini hapa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubuva wakati  akifungua mkutano na waandishi wa habari wa Mkoa wa Singida.
 
Jaji Lubuva alisema lengo ni kuhakikisha kuwa wale wote wenye sifa za kuwa wapiga kura wanajitokeza kwa wingi katika vituo vya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. 
Aidha alisema kuwa Tume inatarajia kufanaya uboreshaji wa Daftari la Kudumu wa Wapiga kura kwa awamu ya kwanza hivi karibuni kwa kutumia Teknolojia mpya ya Biometric Vote Regstration ( BVR). 
Alisema mfumo huo mpya ni wa kuchukua au kupima taarifa za mtu za kibaiolojia au tabia ya mwanadamu na kuhifadhi katika kanzi data kwa ajili ya utambuzi. 
“Mfumo huu hutumika katika kumtambua mtu na kumtofautisha na mwingine, ingawa tabia hizo za binadamu ziko nyingi, lakini kwa ajili ya kuandikisha wapiga kura alama za vidole kumi vya mikono, picha na saini ndizo zitachukuliwa na kuhifadhiwa kwenye Kanzi Data (Database) ya wapiga kura.” Alisisitiza Jaji Lubuva.  
Hata hivyo alisema kwa kutumia mfumo huu wa (BVR), wananchi wote wenye sifa za kuwa wapiga kura na wale walio na kadi za mpiga kura watatakiwa kuandikishwa upya.
 
Jaji Lubuva alisema mafunzo kwa Watendaji yanatarajiwa kufanyika muda kuanzia Mwezi Julai mwaka hauu kabla ya zoezi la uboreshaji wa Daftari kufanyiaka.
 
Mwenyekiti huyo alibainisha kwamba uhakiki wa vituo vya kuandikisha wapiga kura umeshafanyika na kwa sasa uandikishaji utafanyika katika vituo vilivyo katika ngazi ya vitongoji, Vijiji na Mitaa. 
“ Kutokana na utaratibu huu wa sasa vituo vya kujiandikisha vimeongezeka kutoka 24,919 hadi kufikia vituo 40,015 ambavyo vimewekwa katika ngazi za Vitongoji, Vijiji na Mitaa’. Alisema na kuongeza 
 “Ili kuwezesha kuwa karibu zaidi na wanancahi na hivyo kupunguza malalamiko ya auambali wa vituo vya kujiandikisha na kuaongeza mwamko wa kujiandikishwa na kupiga kura.” Alifafanua Jaji Lubuva. 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Joseph Mchina, alisema maandalizi yote muhimu kwa ajili ya zoezi hilo katika Manispaa yake yamekamilika na hivyo kuwa na vituo 154 badala ya 84 vya awali.

No comments: