Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba
NA ELIYA MBONEA, ARUSHA
ALIYEWAHI
kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa
Arusha, Samson Mwigamba, amesema hakuwa kichaa wala punguani wakati
alipopeleka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa malalamiko ya kuvunja Katiba
ya chama hicho kwa kubadili kipengele cha Katiba kilichoondoa ukomo wa
uongozi.(Martha Magessa)
Mwigamba, ambaye kwa sasa ni Kaimu Katibu
Mkuu wa Chama cha ACT- Tanzania, alimshukuru Mungu kwa Ofisi ya Msajili
kusimamia na kuwaeleza ukweli wanachama wa Chadema juu ya
alichokiwasilisha.
"Unajua
wakati napiga kelele ndani ya chama baadhi ya viongozi na wanachama wa
Chadema waliniona mimi kama kichaa na punguani. Wakaamua kunivua uongozi
na uanachama.
"Ni
wakati muafaka sasa kwa wanachama wao kutambua kuwa nilikuwa napigania
mambo ninayoyajua, sikuwa kichaa kama walivyodhani na kuamua kunitukana
na kunidharau," alisema Mwigamba.
Mwigamba
alikwenda mbali na kufananisha kombora alilowapiga Chadema kuwa ni sawa
na la kivita ambalo hurushwa na kuishambulia ndege kila inakoelekea na
hatimaye kuidondosha.
Alisema
katika mazingira ya kutokuelewa, Chadema walimfukuza uanachama wakiamini
kwamba hoja ya kuvunja katiba ya chama aliyokuwa ameiwasilisha kwa
ofisi hiyo ya msajili ingetupwa.
"Baada ya
wao kunifukuza uanachama kwa kweli sikufuatilia tena hoja niliyokuwa
nimeipeleka Ofisi ya Msajili kwa sababu nilijua sipo huko na tayari
nilikuwa naendelea na mambo yangu mengine.
"Lakini
cha ajabu kumbe msajili aliona hoja niliyoipeleka ilikuwa na mashiko na
ndiyo maana aliendelea kuifanyia kazi na hatimaye amejiridhisha kuwa
Chadema walikuwa wamevunja katiba ya chama chao," alisema.
CHANZA:MTANZANIA
No comments:
Post a Comment