Friday, December 12, 2014

Tanzania yasaini mkataba wa Sh. bilioni 15.5 kutoka benki ya ADB kuboresha kituo cha utafiti MUHAS.

unnamed
Katibu Mkuu Wizara ya fedha Bw. Servacius Likwalile (kushoto) akikisaini Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) kwa ajili ya kuboresha kituo cha utafiti wa magonjwa ya moyo kinachosimamiwa na Chuo Kuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Muwakilishi wa Benki ya ADB nchini Tonia Kandiero akisaini mkataba huo kwa niaba ya Rais wa benki hiyo Dkt. Donald Kaberuka.
unnamed1
Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donan Mmbando (kushoto) akitoa neno la shukurani baada ya kusainiwa  Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) kwa ajili ya kuboresha kituo cha utafiti wa magonjwa ya moyo kinachosimamiwa na Chuo Kuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) leo jijini Dar es salaam. Wa kwanza kulia ni Muwakilishi wa Benki ya ADB nchini Tonia Kandiero na katikati ni Katibu Mkuu Wizara ya fedha Bw. Servacius Likwalile.
………………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
Serikali ya Tanzania imetiliana saini mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 9.4 ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 15.5 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) kwa ajili ya kuboresha kituo cha utafiti wa magonjwa ya moyo kinachosimamiwa na Chuo Kuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).
Mkataba huo wa makubaliano umesainiwa leo jijini Dara es salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Muwakilishi wa Benki ya ADB nchini Tonia Kandiero kwa niaba ya Rais wa benki hiyo Dkt. Donald Kaberuka.
Dkt. Likwelile alisema kuwa kituo hicho kitasaidia kupunguza tatizo la wataalam wa afya nchini na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na hivyo kupunguza idadi kubwa ya  wagonjwa wanaotibiwa nje ya nchi.
Kwa upande wake Muwakilishi wa Benki ya ADB nchini Tonia Kandiero ameipongeza Tanzania kuwa nchi ya kwanza kusaini mkataba huo kati ya nchi nne za jumuiya ya EAC zinazokusudiwa kujenga kituo kama hicho.
Bi Tonia alisema kuwa benki ya ADB imejiwekea lengo kuboresha rasilimali watu katika fani ya afya ambapo mradi wa ujenzi wa kituo kinachojengwa MUHAS upo katika mkakati wa benki hiyo ambao uulianza 2011 hadi 2015, mpango mkakati wa benki wa 2013 hadi 2017 na mfumo mpya wa elimu katka nchi za Afrika.
Mfumo huo unalenga kutatua tatizo la utaalaam katika soko la ajira kwa kupitia vituo bora vya kanda vya afya ili kuendana na dira ya maendeleo ya Taifa na mkakati wa kupunguza umasikini ifikapo mwaka 2025.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donan Mbando ameushukuru uongozi wa benki ya ADB kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania na kuahidi fedha hizo zitatumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa.
Hadi kukamilika kwa kituo hicho cha afya kinachojengwa katika chuo cha MUHAS kitagharimiwa na benki ya ADB kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.

No comments: