Waziri wa
Nchi (OR) ikulu na utawala bora Dr. Mwinyihaji Makame Mwadini Zanzibar
akisalimiana na katibu Mtendaji wa SADC Dkt.Stergomena Tax wakati
wakisubiri Rais Jakaya Mrisho Kikwete ahutubie na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa
Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mamia
ya wanahabari wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika
uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa
Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho kikwete akipanda jukwaani tayari kuhutubia na kuaga rasmi wakati
wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili
June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini
Johannesburg, Afrika Kusini.
Shehemu ya wajumbe wa Mkutano wa
25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano
wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Brigedia Jenerali Sara Thomas Rwambali, Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Afrika katika Sudan ya Kusini akiwa kwenye kwenye Mkutano
wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14,
2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini
Johannesburg, Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa
Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Rais wa Visiwa vya Comoro baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Mama Salma Kikwete akimpongeza mumewe Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akiongea na Mwenyekiti wa AU Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na rais
Yoweri Museveni wa Uganda baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wajumbe mbalimbali baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais wa Somalia Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu wa Misri Mhe Ibrahim Mahlab baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mjumbe maalumu wa Marekani katika Maziwa Makuu baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mfalme Mswati wa Swaziland baada ya kuhutubia na kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg,
Afrika Kusini.
……………………………………………………………………………
Rais Kikwete: Sera ya Nje itabakia ile ile
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa siasa ya nchi za
nje na misingi mikuu ya kuongoza mahusiano ya Tanzania na nchi za
kigeni hayatabadilika hata baada ya yeye kuondoka madarakani mwanzoni
mwa Novemba, mwaka huu, 2015.
Aidha, Rais Kikwete
amewahakikishia viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kuwa
yeye anaondoka madarakani lakini Tanzania waliyoizoea na kuijua itabakia
pale pale na kuwaomba viongozi hao kumpa ushirikiano mkubwa mrithi wake
kama walimpa yeye.
Rais Kikwete ametoa uhakikisho
huo mara mbili leo, Jumapili, Juni 14, 2015, wakati alipohutubia kuwaaga
wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa
Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa leo kwenye
Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika
Kusini. Wakati wa mkutano ujao wa kawaida wa AU mjini Addis Ababa,
Ethiopia, Januari, mwakani, Tanzania itakuwa na Rais mpya, Rais wa Tano.
Aidha, Rais Kikwete amerudia
kauli na msimamo huo wa Tanzania wakati alipokutana na kufanya
mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Somalia, Mheshimiwa Hassan Sheikh
Mahmoud ambako kiongozi huyo wa Somalia amemjulisha Rais Kikwete kuwa
angependa kutembelea Tanzania baadaye mwaka huu.
Alisema Rais Kikwete kuwa
misingi ya siasa za nchi za nje za Tanzania na misingi mikuu ya kuongoza
mahusiano yake na nchi za nje yaliwekwa tokea Uhuru na hasa tangu
kutungwa wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania mwaka 1972 na tokea wakati
huo hajapata kubadilika kama kama wamebadilika viongozi mara nne sasa.
“Hatujapata kubadilisha misingi
hiyo inayoelekeza kuwa mahusiano yatajengwa kuanzia nchi za jirani,
zikifuatiwa na nchi za Afrika, nchi marafiki duniani na nchi
nyinginezo.”
“Sina shaka kabisa kuwa misingi
ya siasa za nje na misingi mikuu ya uongozi wan chi yetu itabakia ile
ile isipokuwa kama Rais ajaye atatoka chama kingine. Kitakachobadilika
ni staili ya uongozi tu lakini misingi ya uongozi itabadilia pale pale
kwa sababu ni misingi mizuri, ni misingi ya busara ambayo imeongoza nchi
yetu vizuri kwa miaka mingi.”
Ameongeza Rais Kikwete: “Ni
matumaini yangu kuwa Watanzania tutachagua kiongozi mzuri atakayeendela
kutoa kipaumbele cha juu kwa masuala ya Afrika pamoja na uanachama na
ushiriki wetu katika Umoja wa Afrika. Haya ni miongoni mwa misingi mikuu
ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania tangu uhuru mpaka sasa. Nawaomba
mumpe ushirikiano mkubwa kama mliopnipatia mimi na hata kuzidi.”
by SOLO Mazalla
No comments:
Post a Comment