Monday, May 22, 2017

IJUE RUNGWE NA MLIMA WA TATU KWA UREFU TANZANIA (MLIMA RUNGWE)

 mlima Rungwe kwa mbali uonekanavyo.

mlima unavyoonekana ukiwa katika mji wa Tukuyu.

ukiwa vijiji jirani karibu na mlima.

Muonekano wa mlima rungwe ambao kwa urefu ni watatu Tanzania ukianza na mlima kilmanjaro  wenye  mita 5,895 ukifuata mlima meru 4,566 na unafuata mlima rungwe  2,960 ambao una, mabwawa yasiyopungua maji wala kuongezeka,  maporomoko ya maji, wanyama mbalimbali wakiwepo na vyula wanaopatikana rungwe tu na nyani aina ya kipunji anayepatikana katika mlima rungwe tu duniani kote. 

Mlima Rungwe ni volkeno iliyozimika ya Tanzania kusini magharibi ikikadiliwa ya kwamba mlipuko wake wa mwisho ulitokea mnamo miaka 2,000 hadi 5,000 iliyopita. mlima huu una kimo cha mita 2,960 ni mlima mkubwa mkoani mbeya. 

Mlima unasimama juu ya ncha kaskazini ya ziwa nyasa, upande wa kusini mashariki wa mlioma hupokea usimbishaji wa milimita 3,000 kwa mwaka ambao ni juu kabisa katika Tanzania.

Mazingira ya mlima ni nchi yenye rutuba na kilimo, pia Rungwe ni eneo la wanyakyusa jina la mlima limekuwa pia jina la Wilaya ya Rungwe 

Endelea kufuatana na KINGOTANZANIA Kujua fulsa zaidi zinazopatikana katika mlima Rungwe 

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya, Karibu Rungwe, Karibu Busokelo 

Karibuni sana KINGITANZANIA

No comments: