Korea Kusini imependekeza kufanyika mazungumzo ya kijeshi na Korea Kaskazini, baada ya majuma kadhaa ya msukosuko, kufuatia hatua ya Korea Kaskazini ya kufanya majaribio ya makombora.
Ikiwa mazungumzo hayo yatafanyika, yatakuwa ndiyo ya kwanza ya juu tangu mwaka 2015.
Maafisa wa vyeo vya juu walisema kuwa mazungumzo hayo yatalenga kisitisha vitendo vyote vyote ambavyo huchangia kuwepo misikusuko ya kijeshi katika eneo lenye ulinzi mkali kati ya Kusini Kaskazini.
Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in tangu mwanzo alikuwa ameashiria kuchukua hatua ya kuleta ushirikiano wa karibu na Korea Kaskazini.
No comments:
Post a Comment