Tuesday, January 16, 2018

Daktari wa White House asema afya ya akili ya Trump ni nzuri

Donald Trump shakes hands with Dr Ronny Jackson after his annual physical exam at Walter Reed National Military Medical Center in Bethesda, Maryland, 12 January 2018Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionBw Trump akimsalimia Dkt Jackson bbada ya uchunguzi Ijumaa
Rais Trump hajaonyesha dalili zozote za matatizo ya kiakili kufuatia uchunguzi wa kiafya na yuko la afya nzuri, daktari wa White House amesema.
"Sina wasi wasi wowote kuhusu afya ya akili ya Trump," Ronny Jackson alisema Jumanne.
Wiki iliyopita Trump alifanyiwa uchunguzi wa afya wa saa tatu, ambao ni wake wa kwanza tangu awe rais wa Marekani.
Hii ni baada ya kutolewa kitabu chenye utata kulichoeneza uvumi kuhusu afya ya kiakili ya Rais Trump.
Akiongea na waandishi wa habari wakati wa mkutano huko White House, Dkt Jackson alisema kuwa kwa jumla afya ya rais ni nzuiri.
"Anaendelea kufurahia moyo wenye afya na afya yote kwa jumla kutokana na kutovuta sigara na kutokunywa pombe," aliongzea.
White House physician Ronny Jackson answers question about US President Donald Trump's health after the president's annual physical at the White House in Washington, 16 January 2018Haki miliki ya pich
Image captionDr Jackson alisema hana wasi wasi na afya ya kiakili ya Trump
Hata hivyo Dkt Jakcson alisema kuwa Bw Trump, 71, atanufaika kwa kupunguza vyakula vyenye mafuta na mazoezi zaidi.
Siku ya Ijumaa rais alichunguzwa na madaktari wa kijeshi katika kituoa cha afya cha Walter Reed huko Bethesda, Maryland katika uchunguzi uliotajwa kuwa uliofanikiwa.
Kulingana na Michael Wolf ambaye ni mwandishi wa kitabu cha Fire and Fury: Inside the Trump White House, ni kuwa wafanyakazi wote wa White House walimuona Trump kama mtoto.
Trump alijibu kwa kusema kwa kitabu hicho kimejaa uongo huku naye waziri wa mashauri ya nchi za kigeni akikana madai kuwa afya ya rais ilikuwa inafeli.

No comments: