Mwenyekiti wa (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli amewaonya wajumbe wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kuwa endapo watachagua viongozi kama waliokuwepo awali watambue watapata shida kwa miaka mingine mitano.
Magufuli amesema hayo leo Disemba 10, 2017 akiwa Makao Makuu ya nchi mjini Dodoma alipohudhuria Mkutano Mkuu wa tisa wa UVCCM Taifa ambapo amewataka vijana wa chama hicho wasiogope kufanya maamuzi yenye kuleta mabadiliko katika safu ya uongozi wa Umoja huo kwa kuwa viongozi waliokuwepo tayari wameonyesha kuwa na dosari na kuwakosesha nafasi vijana wengi kuweza kupewa nafasi katika serikali ya awamu ya tano.
"Mwenyekiti mtakaye mchagua, Makamu Mwenyekiti na uongozi wote wa vijana mtakaouchagua leo hao ndiyo watakuwa washauri wangu wakubwa ila mkichagua kama wale ambao hawakunishauri hata kwa kuniletea majina ya kuteua kwenye nafasi zenu, mkachagua tena katika mwaka huu mjue mna miaka mitano mingine ya kuumia" alisisitiza Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli aliwataka vijana hao kutowachagua viongozi wa UVCCM ambao wanatumia fedha kutaka kupata nafasi ndani ya umoja huo wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Magufuli amesema hayo leo Disemba 10, 2017 akiwa Makao Makuu ya nchi mjini Dodoma alipohudhuria Mkutano Mkuu wa tisa wa UVCCM Taifa ambapo amewataka vijana wa chama hicho wasiogope kufanya maamuzi yenye kuleta mabadiliko katika safu ya uongozi wa Umoja huo kwa kuwa viongozi waliokuwepo tayari wameonyesha kuwa na dosari na kuwakosesha nafasi vijana wengi kuweza kupewa nafasi katika serikali ya awamu ya tano.
"Mwenyekiti mtakaye mchagua, Makamu Mwenyekiti na uongozi wote wa vijana mtakaouchagua leo hao ndiyo watakuwa washauri wangu wakubwa ila mkichagua kama wale ambao hawakunishauri hata kwa kuniletea majina ya kuteua kwenye nafasi zenu, mkachagua tena katika mwaka huu mjue mna miaka mitano mingine ya kuumia" alisisitiza Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli aliwataka vijana hao kutowachagua viongozi wa UVCCM ambao wanatumia fedha kutaka kupata nafasi ndani ya umoja huo wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
No comments:
Post a Comment