Dk Sengondo Mvungi.PICHA|MAKTABA
Hospitali ya Millpark ya 
Johannesburg, Afrika Kusini, imesema madaktari waliokuwa wakimtibu 
aliyekuwa Kamishna wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi 
walibaini kuharibika kwa ubongo wake kutokana na kumwagika kwa maji 
yanayoutunza ambayo kitaalamu yanaitwa ‘cerebrospinal fluids’ au CCF.
Msemaji wa Hospitali hiyo, 
Tebogo Nyembezi alisema Dk Mvungi alicheleweshewa tiba baada ya kupata 
tatizo la maji hayo yanayotunza ubongo kumwagika mara baada ya 
kujeruhiwa.
Dk Mvungi (61), alipata majeraha
 makubwa baada ya kujeruhiwa na watu waliovamia nyumbani kwake Kibamba, 
Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, Novemba 3 mwaka huu. Alifariki dunia
 jana mchana.
SOMA ZAIDI.....
 
SOMA ZAIDI.....
“Maji hayo ambayo ni miligramu 
50 tu katika ubongo wa mwanadamu ambayo huufanya ubongo uelee 
yakimwagika nusu tu, basi mgonjwa yupo hatarini, lakini akiwahishwa na 
kupata tiba sahihi anaweza kupona,” alisema Nyembezi.
Alisema iwapo mgonjwa atapewa 
tiba sahihi ndani ya saa 48, ubongo wake unaweza kurudi katika hali ya 
kawaida, lakini saa hizo zikizidi hawezi kupona kabisa kwa sababu maji 
hayo yanapomwagika ubongo hujigonga kwenye mifupa ya sakafu yake na 
kuharibika kabisa.
Mtaalamu wa mishipa na neva za 
fahamu (neurosurgeon) katika Hospitali ya Regency, Dar es Salaam, Dk 
Hariff Najin alisema kazi kubwa ya maji hayo ni kuulinda ubongo pindi 
inapotokea ajali ili usidhurike lakini endapo maji hayo yatamwagika nao 
huharibika.
“Haya maji yanaufanya ubongo 
uelee na usielemee kichwa. Hivyo inapotokea maji haya yakaisha au 
kupungua, ubongo hujigonga na kukosa ukinzani na kuharibika,” alisema.
Alisema maji hayo ambayo hufika 
hadi kwenye uti wa mgongo yakikosekana katika ubongo, husababisha damu 
isitembee kwenye eneo hilo jambo ambalo pia linaweza kusababisha mishipa
 katika sehemu ya nyuma ya ubongo kuharibiwa.
Akizungumzia suala hilo, 
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya 
Fahamu Muhimbili (Moi), Profesa Lawrence Museru alisema anachofahamu ni 
kuwa Dk Mvungi alipelekwa Afrika Kusini kwa kuwa alipata madhara makubwa
 kwenye ubongo na wala si kwa sababu ya kumwagika kwa maji kama 
ilivyoelezwa Afrika Kusini.
“Majeraha hayo yalisababisha 
damu kuvilia katika ubongo na kusababisha uvimbe ambao kwa kitaalamu 
unaitwa ‘traumatic brain injury’ na sisi tulithibitisha vipimo hivyo vya
 awali na kumsindikiza mpaka huko,” alisema Profesa Maseru.
Profesa Museru alisema Dk Mvungi
 alipata majeraha makubwa kichwani na sehemu nyingine mwilini ambayo 
yanaonekana yalisababishwa na kupigwa kwa vitu vyenye ncha kali au 
magongo na hivyo kuleta madhara katika ubongo.
Alisema
 hawezi kuthibitisha chanzo hasa cha kifo hicho kwani kinaweza kuwa ni 
kuharibika kwa ubongo au sababu nyingine zilizotokana na tatizo hilo 
(secondary causes).
Naye Dk Mugisha Clement ambaye 
alimuhudumia Dk Mvungi alipofikishwa Moi na baadaye kumsindikiza hadi 
Afrika Kusini, alisema kitaalamu kumwagika kwa maji yanayolinda ubongo 
hakuwezi kuleta madhara kama aliyoyapata mwanasheria huyo, bali tatizo 
lilikuwa ni kuvimba na kuvilia damu katika ubongo.
“Maji ya CSF hayakuwa sababu ya 
kifo cha Dk Mvungi, sisi tulitambua tatizo la awali kuwa majeraha 
yalisababisha kuvimba na kuvilia damu. Kitaalamu haiwezekani maji hayo 
yakasababisha madhara makubwa,” alisema.
Kucheleweshwa kwa matibabu
Kuhusu kutokuwapo kwa opereta wa
 mashine ya CT Scan inayotumika kupima ubongo siku ambayo Dk Mvungi 
alipelekwa Moi, Profesa Museru alisema hatua za kinidhamu zitachukuliwa.
Hata hivyo, alisema kukosekana kwake hakukusababisha au kuchochea madhara kwa Dk Mvungi.
“Ni kweli kutokuwapo kwa opereta
 ni kosa lakini halikuwa na madhara kwa Dk Mvungi kwa sababu hakuwa 
akihitaji upasuaji wa haraka. Lakini ni kosa limefanyika,” alisema 
Profesa Maseru.
Alisema
 matumizi ya CT Scan ni ya muhimu lakini, hata kipindi cha nyuma ambacho
 wagonjwa walipata matatizo katika ubongo bado walitibiwa bila ya kuwapo
 ulazima wa kupata huduma ya mashine hiyo.
CHANZO: MWANANCHI
KINGOTANZANIA 
No comments:
Post a Comment