Saturday, September 22, 2018

Waliofariki Dunia Wafika 209 ajali ya MV Nyerere


Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi mchana Septemba 20, 2018 imefikia 209

Hayo yamebainisha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe  leo jioni Jumamosi Septemba 22, 2018, alipozungumza na waandishi wa habari katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe, Kamwelwe amesema watu waliopatikana wakiwa hai ni 41, baada ya mmoja kuongezeka leo ambaye ni mhandisi wa kivuko hicho, Alphonce Charahani.

Waziri Isack Kamwelwe amesema miili iliyotambuliwa ni 172, kati ya hiyo 112  tayari imeshachukuliwa na ndugu kwa ajili ya maziko.

“Miili 37 bado haijatambuliwa, nieleze tu kuwa ndugu wanaochukua miili kwa ajili ya maziko wanapatiwa ubani wa Sh500,000 kama ambavyo Serikali imeahidi,” amesema Kamwelwe.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  John Mongella amesema meli ya MV Nyehunge kutoka Mwanza inaelekea kisiwa cha Ukara ikiwa na vifaa maalum vitakavyotumika kukinyanyua kivuko hicho ili kurahisisha uokoaji na taratibu nyingine.

Maandalizi ya mazishi ya waliofariki ajali MV Nyerere yaanza


Maandalizi ya maziko ya waathiriwa wa mkasa wa MV Nyerere hapo kesho yameanza karibu na eneo ambalo kivuko hicho kilizama.

Tayari jeshi la akiba nchini limeanza kuchimba makaburi ya pamoja ambapo waliofariki watazikwa siku ya Jumapili.


No comments: