Saturday, July 27, 2013

Mishahara mipya serikalini 2013

 

Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimuudumia mgonjwa hospitalini hapo. Wafanyakazi wa sekta ya afya ni miongoni wa walio ongezewa mishahara na serikari katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14. Picha na Maktaba  

Dar. Serikali imetangaza mishahara mipya kwa watumishi wa umma itakayoanza kutumika mwezi huu, huku kima cha chini kikiongezwa kwa asilimia 41.18 kutoka Sh 170,000 hadi Sh240,000.
Vilevile, mishahara ya watumishi wengine wa umma imeongezwa kwa wastani wa asilimia 8.41. Waraka namba moja kwa watumishi wa umma uliotolewa na Katibu Mkuu, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi Julai 2 mwaka huu, unaeleza kuwa marekebisho hayo ya mishahara yatahusu watumishi wa serikali kuu na watumishi wa serikali za mitaa.
Wengine watakaonufaika na marekebisho hayo ni watumishi walioshikizwa kwenye taasisi za umma na watumishi ambao watakuwa kwenye likizo inayoambatana na kuacha kazi, kustaafu kazi au kumaliza mikataba baada ya Julai mosi mwaka huu.
Waraka huo umeonyesha kuwa watumishi wa serikali ambao wanapata mishahara binafsi isiyo ndani ya viwango vya mishahara ya serikali hawatahusika na marekebisho hayo.
Mei 29 mwaka huu, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, aliliambia Bunge, kwamba Serikali imekamilisha majadiliano ya kuongeza kima cha chini cha mshahara katika sekta 12 binafsi, kitakachoanza kutumika rasmi Julai mosi.
Waziri Kabaka alitaja sekta hizo kuwa ni ya Ujenzi, Shule Binafsi, Nishati, Viwanda na Biashara, Hoteli na Huduma za Majumbani, Ulinzi Binafsi, Madini, Afya, Uvuvi na Huduma za Majini, Usafirishaji, Mawasiliano na Kilimo. Kwa mujibu wa Kabaka, mishahara imepanda kwa kiwango cha asilimia kati ya 21 na 65 huku Afya ikiongoza kwa kuongezwa ikifuatiwa na sekta ya hoteli na huduma za nyumbani yenye asilimia 55.
Mei mosi mwaka huu akiwa mkoani Mbeya, Rais Jakaya Kikwete, aliahidi unafuu wa maisha kwa wafanyakazi kwa kuangalia uwezekano pia wa kupunguza kodi kwenye mishahara, Lipa Kadiri Unavyopata (PAYE).
Kuhusu kuongeza mishahara, Rais Kikwete aliahidi wafanyakazi wote kwamba Serikali itaendelea kuiongeza kulingana na hali ya uchumi wa nchi. Waraka huo unaonyesha kuwa mishahara mipya kwa watumishi wa serikali kada ya masharti (operational service), ngazi ya mshahara na mshahara mpya kwenye mabano ni;
TGOS A
TGOS A 1. (Sh240,000), TGOS A 2. (Sh245,600), TGOS A 3. (Sh251,200), TGOS A 4. (Sh256,800), TGOS A 5. (Sh262,400), TGOS A 6. (Sh268,000), TGOS A 7.(Sh272,000), TGOS A 8(Sh279,000), TGOS A 9.(Sh284,800), TGOS A 10(Sh290,400), TGOS A 11(Sh296,000), TGOS A 12(Sh301,600), TGOS A 13(Sh 307,200), TGOS A 14(Sh312,800), TGOS A 15(Sh 318,400), TGOS A 16(Sh324,000), TGOS A 17(Sh329,600) na TGOS A 18(Sh335,200).
TGOS B
TGOS B 1. (Sh347,000), TGOS B 2. (Sh356,500) TGOS B 3 . (Sh366,000), TGOS B 4 . (Sh375,500), TGOS B 5. (Sh385,000), TGOS B 6. (Sh394,500), TGOS B 7. (Sh404,000), TGOS B 8. (Sh413,500), TGOS B 9. (Sh423,000), TGOS B 10. (Sh432,500), TGOS B 11 . (Sh442,000) na TGOS B 12. (Sh451,500).
1 | 2 | 3 | 4 | 5 | 6 | 7 | 8 | 9 | 10 | 11 | 12 | 13 Next Page»
..........................................................................................................................
 

TANZANIA TUMETOLEWA MICHUANO YA CHAN

images d6db8
Tanzania (Taifa Stars) imeshindwa kufuzu Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) kwa mara ya pili mfululizo baada ya leo (Julai 27 mwaka huu) kufungwa mabao 3-1 na Uganda Cranes, hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 4-1.
hdg

Stars ambayo ilicheza fainali za kwanza zilizofanyika Ivory Coast mwaka 2009 ilimaliza kipindi cha kwanza katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Kampala ikiwa sare ya bao 1-1.
Wenyeji ndiyo walioanza kufunga bao dakika ya saba katika mechi hiyo iliyochezeshwa na Kanoso Abdoul Ohabee kutoka Madagascar. Frank Kalanda alifunga bao hilo akimalizia mpira uliopigwa ndani ya eneo la hatari la Tanzania.
Bao hilo halikuonekana kuichangaza Taifa Stars, kwani ilitulia na kufanikiwa kusawazisha dakika ya 18 mfungaji akiwa Amri Kiemba kutokana na pasi nzuri ya Mrisho Ngasa kwenye kona ya eneo la mita 18.
Dakika ya 32 nusura Taifa Stars ipate bao, lakini mkwaju maridadi wa Mrisho Ngasa ambao tayari ulikuwa umempira kipa HAmza Muwonge uligonga mwamba kabla ya kuokolewa na mabeki wa Uganda Cranes.
Mabao mengine ya Uganda Cranes yalifungwa dakika ya 48 kupitia kwa Brian Majwega na lingine dakika ya 63 mfungaji akiwa tenda Kalanda kutokana na makosa ya Salum Abubakar kupokonywa mpira wakati akiwa katika nafasi nzuri ya kutoa pasi kwa mwenzake.
Kocha Kim Poulsen alifanya mabadiliko dakika ya 43 kwa kumuingiza Simon Msuva badala ya Frank Domayo aliyeumia, na dakika ya 78 akawaingiza kwa mpigo Haruni Chanongo na Vincent Barnabas badala ya David Luhende na John Bocco. Hata hivyo mabadiliko hayo hayakubadili matokeo ya mchezo.
Kikosi cha Stars kilipangwa hivi; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, David Luhende/Vincent Barnabas, Aggrey Morris, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Frank Domayo/Simon Msuva, Salum Abubakar, John Bocco/Haruni Chanongo, Amri Kiemba na Mrisho Ngasa.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itarejea nyumbani kesho (Julai 28 mwaka huu) saa 4 usiku kwa ndege ya PrecisionAir.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
................................................................................................

UFUNGAji MAFUNZO YA AWALI YA POLISI NA UHAMIAJI katika picha


A 2935f
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI MH, Dr. EMMANUEL NCHIMBI AKIKAGUA GWARIDE LA WAHITIMU WA MAFUNZO YA AWALI YA ASKARI POLISI WAKATI WA SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO HAYO JANA KATIKA CHUO CHA POLISI MOSHI (CCP). TAKRIBANI ASKARI POLISI ELFU TATU NA TISINI NA MBILI WALIHITIMU MAFUNZO, WAKIWEMO ASKARI WA UHAMIAJI HAMSINI NA MOJA

B 6d323
ASKARI POLISI WALIOHITIMU MAFUNZO, WAKIONYESHA PIKIPIKI INAVYOWEZA KUSAIDIA KATIKA KUKABILIANA NA WAHALIFU KWA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI MH, Dr. EMMANUEL NCHIMBI ALIYEKUA MGENI RASMI KATIKA SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI KWA ASKARI POLISI NA UHAMIAJI JANA MJINI MOSHI. TAKRIBANI ASKARI POLISI ELFU TATU NA TISINI NA MBILI WALIHITIMU MAFUNZO, WAKIWEMO ASKARI WA UHAMIAJI HAMSINI NA MOJA
C 3822c
WASANII WA KIKUNDI CHA NGOMA CHA CHUO CHA POLISI MOSHI WAKITOA BURUDANI JANA MJINI MOSHI WAKATI WA SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI KWA ASKARI POLISI NA UHAMIAJI. TAKRIBANI ASKARI POLISI ELFU TATU NA TISINI NA MBILI WALIHITIMU MAFUNZO, WAKIWEMO ASKARI WA UHAMIAJI HAMSINI NA MOJA. PICHA NA HASSAN MNDEME-JESHI LA POLISI.

No comments: