Tuesday, September 9, 2014

KIJANA GABRIEL MWASYEBULE AUAWA AKITUHUMIWA NA WANANCHI KWA TUHUMA ZA IMANI YA KISHIRIKINA BUSOKELO‏ WILAYANI RUNGWE

MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE ENZI ZA UHAI WAKE
WANANCHI WA LWANGWA NA VITONGOJI YAKE WAKIWA WAMEMPIGA MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE HADI KUUA NA KUMCHOMA MOTO

KAMERA YA KINGOTANZANIA ILIFANIKIWA KUFIKA KWENYE TUKIA MUDA WA SAA NANE BILA YA KUSHUHUDIA MTU YEYOTE WOTE WAKIWA WAMEJIFICHA KWA KUOGOPA KUKAMATWA NA VYOMBO VYA DORA. HAPO NI MHE DIWANI ALIPOKUWA ANASHUHUDIA MAUAJI YALIVYOFANYIKA

SAA KUMI NA MBILI ASKALI POLISI WALIFIKA ENEO LA TUKIO NA KUUONDOA MWILI WA MAREHEMU ENEO LA UKIO NA KWENDA NAO TUKUYU KWA AJILI YA KUFANYA UCHUNGUZI KABLA YA KUKABIDHIWA NDUGU



KULIA NI MWENYEKITI WA KIJIJI CHA IKAMA MBANDE GWAKISA MWANDEMELE AKIWA NA MHE DIWANI AKIELEZA TUKIO LA MAUAJI LILIVYOTOKEA. GWAKISA AMESEMA KUWA TANGU ASUBUHI WATU WENGI WA KILA PANDE WALIKUSANYIKA KATIKA UWANJA WA MBADE NA KUSUBIRI VIONGOZI KWAMAANA YA CHUFU ANDINDI MWAKALOBO KWENYE MKUTANO WA HADHARA  AJE ATOE MAELEKEZO KUHUSIANA NA TUKIO LA UCHAWI LINALOENDELEA. TOFAUTI NA MATARAJIO YA WENGI NI PALE CHIFU ANDINDI MWAKALOBO ALIPOHAIRISHA MKUTANO NA KUWATANGAZIA WANANCHI WAKE KUWA KIKAO HAKIPO HUKU  WANANCHI WAKITEGEMEO KUMUONA MCHAWI WAO NA VITU VYAKE VYA KICHAWI, MAKUTANO MKUBWA UKAMZOMEA NA KUMSONGA CHIFU KUWA KALA RUSHWA KUTOKA KWA MHUSIKA,  NDIPO VIJANA NA WENGINE WAKAAMUA KWENDA KIJIJI CHA NDEMBO AMBAKO NDIKO ALIPOKUWA  GABRIEL NA KUAMUA KUMLETA MKUTANONI LAKINI WALIPOFIKA NYUMBANI PAMOJA NA KUMKOSA WALIAMUA KUVUNJA MILANGO WAKIDHANI AMEJIFICHA LAKINI MWISHO WA SIKU WALIKIFANIKIWA KUMKUTA POLINI AKIWA AMEJIFICHA NA KUMKAMATA NA KABLA YA KUMFIKISHA UWANJANI WALIAMUA KUMPIGA HADI KIFO NA KUMCHOMA MOTO.

MAREHEMU AKIPAKIWA KWENYE GALI TAYARI KUMPEREKA CHUMBA CHA KUHIFADHIA MAITI TUKUYU UKISUBIRIWA UCHUNGUZI

NYUMBA YA MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE ANAYOTUHUMIWA KUIJENGA KWA UCHAWI

MOJA YA SHAMBA LA VIAZI VINAVYO SUBIRIWA KUVUNWA MWEZI HUU,  SHAMBA LA  MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE, MASHAMBA AMABAYO PIA NI MOJA YA SABABU AMBAZO WANANCHI WA LWANGWA WANAMTUHUMU MAREHEMU KUWA ALIKUWA ANAWALIMISHA WATU KIUCHAWI NA KUIBA MAZAO YA MASHAMBA MENGINE KIUCHAWI ILI SHAMBA LAKE LIWE  NA MAZAO MENGI NA MAZURI

HII NDIO STOO YA KUWEKEA MAZAO MBALIMBALI AMBAYO MAREHEMU ALIKUWA ANATUMIA KUTUNZIA MAZAO YAKE KATIKA MISIMU MBALIMBALI KAMA MAHINDI , NYANYA NA VIAZI.

BAADA YA MAUAJI KUFANYIKA KAMERA YA KINGOTANZANIA IMESHUHUDIA VIJANA WENGI WA LWANGWA NA VIJIJI VYAKE KUTOLOKEA KUSIKO JULIKANA WAKIHOFIA KUKAMATWA NA POLISI

BAADA YA KUUSILIRI MWILI WA MAREHEMU KWENYE JENEZA HAPA NDUGU WAKITOKA NA NA JENEZA LA MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE KATIKA CHUMBA CHA KUHIFADHIA MAITI  KATIKA HOSPITAL YA WILAYA TUKUYU NA KUELEKEA SEHEMU YA MAZIKO KIJIJINI KWAO NDEMBO LWANGWA

NDUGU NA JAMAA WAKISHIRIKI MAZIKO YA GABRIEL MWASYEBULE KIJIJINI KWAO NDEMBO LWANGWA

JENEZA LA MWILI WA MAREHEMU LIKIINGIZWA KABURINI

BAADHI YA WANAKIJIJI NA NDUGU WAKISHIRIKI MAZIKO YA MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE

BABA MDOGO WA MAREHEMU AKIONGEA BAADA YA MAZIKO , AKIWASHUKURU WANANCHI WALIOFIKA KUHUDHULIA MAZIKO YA MWANAE ALIYEUWAWA NA WATU KWA TUHUMA ZA KUWA MCHAWI. HUKU AKIWAPA TAARIFA ZA KIKAO CHA FAMILIA KILICHOKAA SIKU MOJA KABLA YA TUKIO LA MAUAJI AMBAPO FAMILIA YOTE ILIKAA NA MKUSIKA KUULIZWA KAMA ANAHUSIKA NA TUHUMA ZA UCHAWI ZINAZOONGELEWA NA WATU AMA HAUSIKI LAKINI BAADA YA MAULIZANO YA MUDA MLEFU SANA MAREHEMU GABRIEL MWASYEBULE ALIKATAA KUWA HANA UCHAWI WOWOTE ULE ILA NI MAMBO AMBAYO YANATENGENEZWA ILI ACHAFUKE ASIFIKIE MAFANIKIO YAKE YA MAISHA. NDIO YALIKUWA MANENO YA FAMILIA YA MWASYEBULE KATIKA MAZIKO NA KUWATAKA FAMILIA KUWA WATULIVU KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU SANA
MATUKIO ya kujichukulia sheria mikononi bado yanazidi kuyakumba baadhi ya maeneo mkoani Mbeya ambapo katika tukio hili  kijana Gabriel Mwasyebule miaka 39 ameuawa na wananchi wenye hasira kali wakimtuhumu kwa imani za kishirikina.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kumtaja marehemu liyetambulika kwa jina la Gabriel Mwandemwa (Mwasyebule) mkazi wa kijiji cha Ikamambande (Lwangwa) Wilaya ya Rungwe aliuawa na watu wasiofahamika kwa kukatwa na vitu vyenye ncha kali sehemu za kichwani na kifuani.
 
Alisema tukio hilo lilitokea siku ya jumapili majira ya saa tano asubuhi huko katika Kijiji cha Ikamambande, kata ya Lwangwa, Tarafa ya Busokelo, Wilaya ya Rungwe, mkoaniMbeya
 
Alisema taarifa za awali zinadaiwa kuwa, uongozi wa kimila kijijini hapo  uliitisha kikao cha dharura ukihusisha viongozi wa vitongoji na vijiji jirani na ndipo waliamua kumtafuta na kumlazimisha marehemu kuhudhuria katika kikao hicho na kisha kuanza kumpiga na kupelekea kifo chake.
 
Alisema marehemu alikuwa akituhumiwa kuwa ni mshirikina kijijini hapo kwa kuwa anawaroga watoto na kuwa anajipatia mazao mengi ya mavuno ya viazi na kujipatia pesa zilizowezesha ujenzi wa nyumba yake aliyoweka malumalu na Gipsam pia kumiriki pikipiki moja huku akitarajia baada ya mavuno mazuri ya mwaka huu kununua gali la kutembelea.


KINGOTANZANIA - 0752881456

No comments: