Wednesday, February 6, 2013

MASAA SITA ABIRIA WATUMIAO STANDI KUU YA TUKUYU WILAYANI RUNGWE WAPATA SHIDA BAADA YA MGOGORO WA MADELEVA WA MABASI YANAYOFANYA SAFARI YA KYELA, TUKUYU MBEYA WAIBUKA TENA KUGOMA NA KUSABABISHA KELO NA USUMBUFU MKUBWA


HAPA WAPIGA DEBE NA MADELEVA WA MABASI WAKIENDELEA NA MGOMO WA KUSAFIRISHA ABIRIA KWENDA TUKUYU MBEYA NA KYELA

HAPA NI SAA TANO ASUBUHI  KATIKA MJI WA TUKUYU NA HAKUNA USAFIRI KWA KWENDA KYELA WALA MBEYA


SASA KWAKUWA VIONGOZI WAMECHELEWA KATIKA KIKAO WALICHOKAA NA VIONGOZI WA MABASI NA KAMATI YA ULINZI NA UASALAMA YA WILAYA SASA VIJANA WAKAENDA KUCHUKUA XSO ILI KUKATA MITI NA KUWEKA BARABARANI ILI KUZUIA MAGARI YEYOTE KUTOPITA BARABARANI HAPO

GALI YA SERIKALI YA PILI KUTOKA KULIA NAYO IKAJIKUTA INAINGIA KATIKA MGOGORO WA KUZUIWA KUFANYA SHUGHURI ZAKE KWA KUWA LEO NI SIKU YA SHERIA NCHINI NA HII GALI NI YA MAHAKAMA YA WILAYA YA RUNGWE HIVYO KUJIKUTA WANASHINDWA KUFANYA SHUGHURI ZAO

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA RUNGWE MALA IKAWASIRI KATIKA UWANJA WA MPIRA TUKUYU ILI KUONGEA NA WAHUSIKA WA MGOMO HUO. ISHU HAPA NANI AMFUATE MWENZAKE WALIO JUKWAANI AU WAGOMAJI WALIOKO STANDI NA BARABARANI?
BUSALA ZIKAFANYIKA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA MADELEVA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA KUWAFUATA WAHUSIKA WA MGOMO NA KUWATULIZA KWAKUWA MAKERERE YALITAWALA KWA KILA MTU KUJIFANYA MUONGEAJI WAKASAHAU KUWA WANA VIONGOZI WAO WALIOWATUMA KUONGEA NA UONGOZI WA WILAYA ILI KUPATA MUAFAKA WA MADAI YAO. 1.

KATI YA MADAI YA WAGOMAJI NI KWANINI HALMASHAURI YA RUNGWE WAKAMATE GALI YA GOD IS WILING STAND NA IKIWA INAFANYA SERVICE NA KUILIPISHA FAIN LAKI MBILI NA ALOBAINI NA TANO  KWA  SABABU YA KUCHAFUA MAZINGIRA? BAADA YA KUWEPO SINTOFAHAM KWA SIKU TATU NDIPO MADELEVA WAKAAMUA KUGOMA KULIPA USHURU STANDI HAPO NA KUDAI KUONEWA KWA KUTOZWA KIWANGO KIKUBWA CHA PESA BILA YA UFAFANUZI, KITENDO KILICHOIBUA MALALAMIKO MENGINE MAWILI KUTOKUWEPO KWA HUDUMA YA CHOO KWA MASAA 24, NA SEHEMU YA KUPUMZIKA WASAFIRI KUVUJA MAJI KIPINDI HIKI CHA MVUA. MADAI HAYO BAADA YA KUPELEKWA KATIKA KAMATI YA USALAMA YA WILAYA MAAMUZI YALIYOAFIKIWA NI KURUDISHWA KWA PESA ZA NYONGEZA KWA MAANA YA USUMBUFU NA ULINZI WA GALI LILIPOKAMATWA TSH 145,000/=  NA HAO PICHANI DT WA HALMASHAURI YA RUNGWE MR SHIRIMA AMEKABIDHI PESA HIZO KWA MWENYEKITI WA MADELEVA MKOA WA MBEYA NA MADAI MENGINE KUSHUGHURIKIWA KWA WAKATI HUKU CHOO KIKITAKIWA KUFANYA KAZI MASAA 24 BADALA YA UTALATIBU WA AWALI KUFUNGA IFIKAPO JIONI


MWENYEKITI WA MADELEVA  MR MWANDUMBYA AKIONGEA MAAMUZI WALIO KUBARIANA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA RUNGWE


SASA MAADA IMEKOLEA NA USIKIVU UMEONGEZEKA

MMOJA WA MADELEVA AKIONGEA KELO YA KUFUNGWA KWA CHOO WAKATI WA USIKU

DIWANI WA KATA YA BAGAMOYO MR MADODI AKIONGEA NA MADELEVA NA KUWASIHI KUANZA KUFANYA KAZI NA KUWAASA KUWA NA UTARATIBU WA KUKAA MEZANI KUONGEA NA VIONGOZI WAO PINDI WANANCHI WANAPOKUWA NA KELO KULIKO KUJICHUKULIA MAAMUZI AMBAYO YANAPELEKEA WASAFIRI WENGINE KUSUMBUKA

KAIMU MKURUGENZI WA WILAYA YA RUNGWE MR MWANSASU AKIONGEA NA MADELEVA HAO KUTII SHERIA BILA SHURUTI KWA KUJIWEKEA UTARATIBU WA MATUMIZI MAZURI YA STANDI KULIKO KUFANYA STANDI YA MABASI KUWA SEHEMU YA  MATENGENEZO YA MAGALI

MGOGORO UKAISHA NA KAZI ZIKAANZA. HUU MGOGORO UNAOPELEKEA KUFUNGWA KWA BARABARA UMEKUWA WA NNE TANGU MWAKA JANA KWA WANANCHI KUWA NA SABABU ZAO AMBAZO HAZIHUSIANI NA BARABARA KUU ILA WAO HUKIMBILIA KUFUNGA BARABARA KWA KUWEKA VIZUIZI NA KUCHOMA MATAILI ILI KUSHINIKIZA UONGOZI UWASIKIRIZE KWA HARAKA. KWA MFANO MGOGORO WA KIWILA MWANKENJA KUMWONDOA MADARAKANI MWENYEKITI WA KUJIJI VIJANA WALIJIKUSANYA NA KUCHOMA MATAILI NA KUCHOMA MOTO ZAHANATI YA KIJIJI ILI TU KUMWONDOA MWENYEKITI WAO JE ZAHANATI NI YA NANI NA KWA NINI UCHOME NA KUVUNA PAMOJA NA KUIBA VITU?



VIONGOZI WA MABASI WAKAWA NA KIKAO CHAO CHA KUHITIMISHA MGOGORO HUO


MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA AWAONGOZA WAKAZI WA RUNGWE KATIKA  SIKU YA SHERIA NCHINI

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE AKITETA JAMBO NA DAS MOSES MWIDETE KATIKA SHEREHE HIYO

SHEREHE ILIANZA KWA BURUDANI ILIYO JAA MAUDHUI YA KUPINGA RUSHWA NA UWAJIBIKAJI KATIKA KAZI HASA SECTA YA MAHAKAMA

KWAYA YA SEKONDARI YA BULYAGA

HAKIMU MKAZI WA WILAYA YA RUNGWE MHE, O.H. KINGWELE

MR LEBI  G. MWAKATOBE

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE ALIYE MBELE NA NYUMA MWENYE KOTI JEUSI NI MHE, MWAKIPUNGA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA BUSOKELO

SHEREHE ILIANZA KWA DUA NA MAOMBEZI

BAADHI YA WWAFANYAKAZI WA MAHAKAMA YA WILAYA YA RUNGWE

WADAU WA RUNGWE NA MWENYE SHATI JEUPE NI DIWANI WA KATA YA BULYAGA MR MWALUSAMBA

WADAU

MWENYE TAI NI MWENYEKITI WA CCM WILAYA YA RUNGWE NA MWENYE SHATI JEKUNDU NI MR JEREMIA MENEJA WA PRIDE WILAYA YA RUNGWE

KATI YA VITU VILIVYO CHEKESHA WATU NA KUHUZUNISHA NI MATUMIZI MABAYA YA PESA YA SERIKALI NI PALE MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA ALIPOKUWA AKIONGEA NA WANANCHI KUHUSU ADHABU MBADALA KULIKO KUWALUNDIKA WATU HATA WENYE MAKOSA MADOGO GEREZANI NA MKUU WA GEREZA AKADAKIA NA KUSEMA KUWA "MKUU PALE KWANGU KUNA MTU AMEFUNGWA KWA WIZI WA KUKU KWA MIEZI SITA HADI MWAKA NA UKIANGALIA GHARAMA YA KUKU NA CHAKULA ANACHOKULA KWA SIKU NI GHARAMA SANA MAANA KWA SIKU MFUNGWA MMOJA ANATUMIA TSH 8000/= JE KWA MIEZI SITA AU MWA HUO ATAKAYO KUWA HAPO KWANGU ATATUMIA SHILINGI NGAPI?"

HIZI NI TABASAM ZA NJE YA MAHAKAMA NGOJA WAWE KAZINI UWAONE WANAVYO KUUWA

KATIKATI YA SHEREHE UMEME UKALETA HITILAFU LAKINI MAFUNDI WA TANESCO WALISHUGHURIKIA NA MAMBO YALIENDELEA KAMA KAWAIDA

KIJANA AKILAP KWA HISIA KALI MAUDHUI YAKE NI KUPINGA RUSHWA MAENEO YA KAZI MAANA WANYONGE WANAONEWA NA WENYE PESA

HAKIMU  MKAZI MFAWIDHI WA WILAYA YA RUNGWE AKIONGEA NA WANANCHI NA WADAU NA VIONGOZI KUWASHUKURU KWA KUFIKA KWAO KUJUA NINI MAHAKAM INAFANYA NA KUTAMBUA CHANGAMOTO ZAKE

PICHA YA PAMOJA

PICHA YA PAMOJA YA WAFANYAKAZI WA MAHAKAMA WILAYANI RUNGWE

MUNGU IBARIKI TANZANIA
AKIONGEA NA WANANCHI NA WATENDAJI WA MAHAKAMA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AMEWATAKA WATENDAJI WA MAHAKAMA KUTOFANYA KAZI KWA MAZOEA NA AMEWATAKA WANASHERIA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU KWAKUWA CHANGAMOTO ZINAZOJITOKEZA NCHINI ZA MIKATABA MINGI KUWA NA KASOLO NI KUTOKANA NA WANASHERIA KUTOKUWA WAADILIFU NA UZALENDO WA NCHI YAO

PIA AMELITAKA JESHI LA POLISI KUFANYA KAZI KWA KUFUATA UTARATIBU WA SHERIA KULIKO KUWABAMBIKIZA WATU KESI ILI TU KUWAKOMOA AU KUJIPATIA KIPATO KISICHO HARALI KWAO

ZAIDI MEELA AMESEMA WANANCHI WAKIKATAA KUTOA RUSHWA BASI HAKUNA HAKIMU ATAKAYE MFUATA MTU KUOMBA RUSHWA HIVYO AMEKEMEA RUSHWA KUWA NI ADUI WA MAENDELEO KATIKA KILA NYANJA NA KUWATAKA KILA MTU KUWAJIBIKA KATIKA NAFASI YAKE NA KUFUATA  UTARATIBU WA SHERIA BILA SHURUTI

MKOANI MBEYA

SIKU YA SHERIA NCHINI YAFANA MBEYA

JAJI MFAWIDHI NOEL PETER CHOCHA AKIJIANDAA KUKAGUWA GWARIDE LILILOANDALIWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA NCHINI
JAJI MFAWIDHI NOEL CHOCHA AKIKAGUA GWARIDE LA KIKOSI CHA FFU MBEYA
KAIMU KAMANDA WA POLISI NA MKUU WA MKOA MBEYA PAMOJA NA WATUMISHI WA MAHAKAMA KUU WAKIWA WANAANGALIA GWALIDE LA KIKOSI CHA FFU MBEYA




  KITAIFA

RAIS KIKWETE ASHIRIKI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA NCHINI

S14 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia  leo Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini 
(PICHA NA IKULU)
s1 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Jaji Mkuu Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Kiongozi  Mhe Fakihi Jundu, Jaji January Msofe, Spika Anne Makinda, Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Mathias Chikawe na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Saidi Mecky Sadik leo Februari 6, 2013 baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini
s2 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mchungaji Christopher Mtikila leo Februari 6, 2013 baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini. Kushoto ni Jaji Mkuu Mhe Mohamed Chande Othman
s3 
Viongozi wa dini ya Kihindu wakielekea kwenye kipaza sauti ili kuomba dua leo Februari 6, 2013 wakati wa  maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini. Viongozi wa dini za Kiislamu na Kiktristo pia walishiriki kwenye maadhimisho hayo.
s5 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na majaji wa Mahakama ya Rufaa leo Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini
s6 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania leo Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini
s7 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na majaji wakuu wastaafu na viongozi wengine leo Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini
s8 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa dini pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu  Rais wa Mawakili leo Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini
s9 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wanasheria  leo  Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini
s10 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu leo Februari 6, 2013  katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania jijini

 

WILAYA YA CHUNYA – ASKARI POLISI MMOJA AUAWA KATIKA MAPAMBANO YA KURUSHIANA RISASI NA MAJAMBAZI


 MNAMO TAREHE 06.02.2013 MAJIRA SAA 00:30HRS HUKO  KATIKA HOSPITALI YA MWAMBANI – MKWAJUNI WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA . ASKARI POLISI G.68 PC JAFARI KARUME MOHAMED MIAKA 30,MUHA WA KITUO CHA POLISI MKWAJUNI   ALIFARIKI DUNIA WAKATI AKIENDELEA KUPATIWA MATIBABU HOSPITALINI HAPO . CHANZO CHA TUKIO NI MAJAMBAZI  WANNE WAKIWA NA SILAHA  IDHANIWAYO KUWA AINA YA SMG WALIVAMIA KITUO CHA MAFUTA KILICHOPO KIJIJI CHA MATUNDASI MALI YA SAMORA S/O MUYOMBE NA KUPORA PESA TSHS 2,200,000/=  WAKITUMIA GARI T.227 BST AINA YA TOYOTA COROLA ILIYOKUWA IKIENDESHWA NA SHABAN S/O MSULE,MIAKA 33,MBENA MKAZI WA MAKAMBAKO .MAREHEMU AKIWA DORIA NA ASKARI WENZAKE WALIFUATILIA TUKIO HILO NA KATIKA MAPAMBANO YA KURUSHIANA RISASI ASKARI HUYO ALIJERUHIWA KWA KUPIGWA RISASI UBAVU WA KULIA NA KUKIMBIZWA HOSPITALINI KWA MATIBABU ZAIDI . KATIKA TUKIO HILO JAMBAZI SHABAN S/O MSULE ALIUAWA KWA KUPIGWA RISASI .GARI  LILILOTUMIKA KATIKA TUKIO HILO LIMEKAMATWA NA MAGANDA 9 YA RISASI AINA YA SMG/SAR NA RISASI 6 ZIMEOKOTWA ENEO LA TUKIO. MWILI WA MAREHEMU ASKARI G.68 PC JAFARI KARUME MOHAMED UMEHIFADHIWA HOSPITALINI HAPO .MSAKO MKALI UNAENDELEA CHINI YA UONGOZI WA RCO MBEYA ROBERT MAYALA – SSP,   ASKARI  POLISI NA WANANCHI ILI KUWABAINI NA KUWAKAMATA WATUHUMIWA WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI .KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA MRAKIBU MWANDAMIZI WA POLISI BARAKAEL MASAKI  ANATOA WITO KWA MTU/WATU WENYE TAARIFA JUU YA MAHALI WALIPO WATU WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE , VINGINEVYO WAJISALIMISHE MARA MOJA.       


                                                       [  BARAKAEL MASAKI – SSP ]
                                  KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
 
 
MICHEZO

Stars yaichapa Cameroon 1-0

mbwanasamata 6e65d
HA HA HA HA WATANZANIA
Smile


No comments: