Friday, April 4, 2014

RIDHIWANI KIKWETE AELEZA HISTORIA YA MAISHA YAKE : "NILIINGIA CCM KABLA YA BABA YANGU JK"

Mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi Ndugu Ridhiwani Kikwete akiongea na waandhishi wa habari na kufafanua mambo mbalimbali katika Ikulu ya Msoga leo ikiwani muda wa lala salama za kampeni katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Jumapili Aprili 6 jimboni humo. IMG_6649 
Waandishi wa habari mbalimbali wakiwajibika katika mkutano huo IMG_6655 
…………………………………………………………………………………………………………….
Ridhiwani anasema ameingia CCM akiwa na umri wa miaka minne na wakati huo aliiingia kwasababu ya kupelekwa kucheza.

Anasema akiwa CCM na umri wake huo, alipata bahati ya kushiriki katika halaiki na alifanikiwa kucheza gwaride.
Wakati huo alikuwa na umri wa miaka mitano na wakati huo Rais Jakaya Kikwete alikuwa Monduli akitoa mafunzo ya Jeshi la Wananchi.

“Wakati nikiwa tayari nimeingia CCM kama Chipukizi , mzee wangu alikuwa hayupo CCM.Hivyo unaweza kuona namna ambavyo hali ilivyo.
Alifafanua kuwa mwaka 1984 alikuwa kiongozi wa gwaride Nachingewa lakini pia alifanikiwa kuwa kiongozi wa gwaride mwaka 1987.

“Rama Kisauti na Rajivu Fundikira, William Lukuvi nilikutana nao Dar es Saalam ambapo kwa wakati huo waliniambia wanataka kuanzisha gwaride Dar es Salaam.
“Nilikuwa mmoja wapo katika gwaride hilo, pamoja na wenzangu wengine akiwemo Tamila Makene.Pia nilikuwa kamanda wa gwaride.Wakati mzee wangu akiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini.
ENDELEA .........................................



“Wakati huo kulifanyika uchaguzi wa kumtafuta kiongozi kwa chipukizi wa CCM katika Wilaya ya Ilala.Niliombwa nigombee lakini nikataa,hivyo nikaombwa kufanya hivyo.Nikaletewa fomu,sikumbuki kama nilitia saini au kidole gumba,”anasema.
Historia yake katika CCM ni ndefu na nyenye kukumbuku nyingi za wapi alitoka na hadi alipofika sasa.

Anasema akiwa kidato cha kwanza akawa mwalimu wa kufundisha chipukizi na ilipofika mwaka 1998 akiwa kidato cha tano, anakumbuka Rais Benjamin Mkapa anakwenda Iringa , yeye alikuwa Shule ya Sekondari Mkwawa.

Alisema wakati akiwa katika shule hiyo, alifuatwa na viongozi watu wa CCM ambapo walimufuata Ridhiwani na kisha kumuomba atafute vijana wenzake ili kwenda kumpokea Rais.
Alisema ilipofika mwaka 2000, waliitwa tena kufanya kazi ya kuhamasisha vijana ili kusaidia chama katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huo.
“Kwa mara ya kwanza ndio ilikuwa naingia rasmi katika kufanya kampeni za uchaguzi mkuu ili kuhakikisha Mkapa anashinda tena urais.

“Mwaka 2001 akiwa chuoni ulitokea uchaguzi Wilaya ya Bagamoyo, nilifuatwa na Rehema Rashidi akitaka nigombee uenyekiti.Nilikataa.
“Hivyo akatafutwa Said Mtanda ili agombee nafasi hiyo lakini naye alikataa lakini baadaye akakubali na alishinda,”alisema.

Hata hivyo baada ya kushinda Mtanda aliamua kumchagua Ridhiwani kuwa Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM Wilaya ya Bagamoyo.
Alifafanua katika maisha yote hayo hajawahi kumshirikirisha mzazi wake(Rais Jakaya Kikwete).
Alisema anakumbuka akiwa katika nafasi hiyo ndipo alipoitwa na Rais Kikwete wakati huo akiwa mbunge wa Chalinze.
“Nakumbuka aliniambia wewe ndio Katibu wa Uhamasishaji Bagamoyo , ndipo aliponiomba nihamasishe vijana wenzangu kujenga shule ya sekondari Changalikwa.

“Wakati tunajenga shule, huku chuoni nako mambo yakawa yanakaribia kumalizika.Hata hivyo tukashauriana na wenzangu kuwa na ndipo tukagombea tena nafasi ya UVCCM Mkoa wa Pwani,”anasema Ridhiwani.

Anaongeza katika kipindi chote hicho hajawahi kushauriana jambo lolote kuhusu siasa na Rais Kikwete.
“Baada ya kupata nafasi hiyo katika Mkoa wa Pwani, wakati huo tayari bwana Kikwete amekuwa Rais.

“Akiwa Mwenyekiti wa CCM, Ridhiwani Kikwete alikwenda na wenzake kuzungumza na Rais na ndipo walipofanikiwa kusaidiwa vifaa mbalimbali vya UVCCM nchima nzima,”alisema.
Pamoja na yote hayo alisema katika siasa, hana kundi lolote yupo kwa ajili ya wote.
“Nafanya siasa ya kwangu mwenyewe sina siasa ya baba yangu.Nasaidiwa na marafiki zangu.Wananisaidia kwenye mambo mengi.

“Mzee wangu ni rafiki yangu mkubwa sana na ndio mwenye kumwambia kila kinachomhusu yeye hata kile ambacho hawezi kumwambia.
Hata hivyo, alisema kuwa mzee wake(Rais), anapenda wananchi wake na amekuwa akitamani kuona wanafanikiwa katika maisha yake.
“Mzee wangu kwa namna ambavyo namjua na yeye ndio mwenyekiti wa CCM, angeweza kukata jina lake.
“Anajua naweza ndio maana amekubali nigombee, asingekuwa tayari nikitie aibu chama changu wala kumtia aibu yeye,”alisema Ridhiwani , ndio mwenye nafasi ya kuamua
Hivyo mzee wake.
litokea nafasi ya kugombea 

SAA 4:30 , asubuhi ya Aprili 4 mwaka huu, Ridhiwani Kikwete anaamua kukutana na waandishi wa habari kwa lengo la kutoa tathimini ya kampeni za Chalinze.
Ridhiwani anapeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa jimbo la Chalinze ambao unafanyika kesho.

Akiwa amekaa katika kiti chake cha miguu minne,nyumbani kwake Msoga jana, Ridhiwani anatumia nafasi hiyo kuwakaribishwa waandishi wa habari.
Anaanza kwa kuaambia kuwa hapa ndipo nyumbani kwangu na wageni wangu wote huwa wanafikia hapa.

Baada ya kutoa ukaribisho huo,Ridhiwani anaanza kwa kuelezea mwenendo mzima wa kampeni tangu zilipoanza hadi kufikia jana.
Ridhiwani aanza kuwa kuwashukuru waandishi wa habari kwa kutenga muda wao na kubwa zaidi namna ambavyo wamefanya kazi kubwa ya kuuhabarisha umma kuhusu kampeni.
Anasema jamii imetambua mambo mengi ambayo yamezungumzwa kwenye kampeni na kwamba Chalinze ni jimbo kubwa kidogo.

Hata hivyo anasema kuwa jimbo la Chalinze yapo matatizo mbalimbali lakini yote yanaweza kupata ufumbuzi wake.
Anataja matatizo ya Chalinze ambako kwake yeye anaeleza kuwa maji ni tatizo kubwa.
Pili ajira kwa vijana wa Chalinze hawana ajira lakini tatizo la tatu ni afya ambayo bado inasuasua katika jimbo hilo.

Anasema kuwa bado kuna tatizo la zahanati na vituo vya afya lakini wakati huo huo kukiwa pia natatizo la uhaba wa dawa.
Ridhiwani anasema kuna tatizo la miundombinu ya barabara ambayo kwake yeye anaamini atashughulikia.

Wakati huo huo anasema anatambua tatizo la migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji.
Anafananua kuwa kuna tatizo la migogoro kati ya vijiji na vijiji lakini pia maeneo ya watu.Katika eneo hilo unakuta kuna migogoro ambayo inatokana na eneo la ardhi kuwa na mtu zaidi ya mmoja.

Kwa lugha nyingine ni kwamba migogoro ya ardhi imegawanyika katika upana wake.
Baada ya kutoa utangulizi huo wa matatizo ya jimbo hilo anatumia nafasi hiyo kuelezea tatizo moja baada ya jingine.
Maji 

Anasema hilo ni tatizo kubwa na juhudi za kuhakikisha maji yanapatikana yalianza muda mrefu.
Wanawake na vijana walikuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta maji.Tatizo la maji lilisababisha hata ndoa za watu kuvunjika.

Hata hivyo, juhudi za kutafuta suluhu ya adha ya maji, ndipo ukaja mradi wa maji Chalinze.Mradi huo ni mkubwa na unatakiwa kupita katika maeneo yote.
Anafafanua kuwa mradi huo wa Wami unatumia chanzo cha maji cha Mto wa Wami na kwamba, awamu ya kwanza ulianza kwa kupelekwa Chalinze na Mdaula na vijiji kadhaa ya maeneo hayo.

Mradi huo ni wa muda mrefu ambapo anafafanua anadhani ulianza mwaka 1978 na kwamba katika kufanikisha mradi huo unakwenda maeneo mengi zaidi yakiwemo ya Kata ya Msata, Kibindu na Miono.

Hata hivyo kuna baadhi ya maeneo ambayo mabomba ya mradi huo yamefika lakini kuna maeneo mengine bado.
Ridhiwani anasema awamu ya tatu ya mradi huo itafika maeneo mengi zaidi ili kuwawezesha wananchi kunufaika na mradi huo.

Pamoja na ufafanuzi huo kuna baadhi ya maeneo ambayo mradi huo haujakamilika kwasababu tu ya waliopewa kazi ya kusambaza mabomba wameshindwa kufanya kazi kiwango kinachotakiwa.

Anafafanua kuwa awamu ya tatu katika mradi huo ni kutoa maji kwenye vijiji na kisha kuvipeleka katika vitongoji.
Pamoja na hayo anasema changamoto kubwa, chanzo cha maji cha Wami kinakabiliwa na tope ambalo linasababisha tekeo kuingiza maji ndani ya mtando.

Anasema kuwa kutokana na matope hayo, mtambo huo ulishindwa kufanya kazi na watalaamu wakashauri kuwa mtambo uzimwe ili kusafisha mtambo huo.
“Mradi huu unasusua kwasababu tu kuna taka zimeingia lakini kazi inayoendelea ni kutafuta ufumbuzi wa moja kwa moja.

“Tutaangalia namga gani ya kufanya kama ni kutafuta dawa ya kusafishia maji au kuzungumza na wilaya jirani ili kutunza chanzo hicho,”anasema.
Ridhiwani anasema ,changamoto iliyopo sasa ni kuhakikisha marambo ya maji yanafufuliwa ili kupunguza tatizo la maji.

Anasema kuna baadhi ya marambo yamesahuulika lakini ni wakati muafaka sasa wa kuhakikisha yanafufuliwa.
Anatoa mfano wa Lulenge  na Matuli ambapo marambo hayo yalitengezwa kwa ajili ya binadamu lakini kilichotokea ng’ombe na binadamu wakawa wanachangia.
Hiyo ni changamoto kubwa lakini anatumia nafasi hiyo kutoa ufafanuzi kuwa umefika wakati pia wa kuchimba visima vya maji.

Anafafanua kuwa jimbo la Chalinze linavyanzo vingi vya maji ambavyo vikitumika vizuri wananchi watapata ufumbuzi.
“Nataka kuhakikisha tunatafuta ufumbuzi wa tatizo la maji kwa kusimamia mambo muhimu yakiwemo ya kuchimba visima, marambo na kutumia vyanzo vingine.
Ajira.

Ridhiwani anasema kuwa ajira ni tatizo kubwa katika jimbo hilo na changamoto kubwa watu wengi wamekosa elimu ya ujasiriamali.
Anasema kuwa kinachotakiwa ni wananchi kupata elimu ya ujasiriamali inayoweza kumsaidia mwananchi kutumia ardhi yake katika kupata maendeleo.
Katika eneo hilo anasema kuwa atasimamia vema matumizi ya trekta badala ya jembe la mkono ili kuongeza tija kwa wakulima.

Mwaka 1982 , akiwa mdogo anakumbuka matrekta ambavyo yalivyotumika kulima zaidi ya 1000 na kazi hiyo ilifanywa na mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo kwa wakati huo.
Anasema kuwa kauli mbiu yake kwa wakulima itakuwa ni kuhimiza kilimo cha kutumia trekta na kazi yake kama mbunge itakuwa ni kusimamia.

“Kupeleka trekta kwa kila kijiji ni jambo ambalo linawezekana na nitasimamia.Matrekta yanatoka wapi, mnajua, Suma JKT wanatoa mikopo ya matrekta lakini pia nchi mbalimbali nazo zinatoa mikopo,”anasema.

Anafafanua anataka kuona njaa inaondoka Chalinze kwa kutumia mpango wa matrekta na kwamba akipata ushirikiano mzuri wa viongozi wengine baada ya miaka miwili Chalinze inaweza kutoa chakula kwa ajili ya mikoa yote.

Hivyo anapozungumzia ajira , anazungumza namna ya kijana kuondokana na ajira tegemezi na badala yake asimame kwa miguu yake.
Anatoa mfano wa eneo la Bwilingu na Pera ambako kuna vijana wengi hawana ajira.
Anasema vijana wengi wa eneo hilo kazi yao kubwa ni kuuza bidhaa ndogondogo kwa abiria wanaosafiri kwenye mabasi yanayopita eneo hilo.

Anasema lazima atafute eneo ambalo vijana hao watafanya kazi zao na katika kuwahakikishia kupata sehemu ya kufanya biashara ni kujengwa kwa kituo cha mabasi Chalinze.
Anasema kutakapokuwa na kituo cha mabasi, vijana watakuwa na uhakika wa kufanya biashara zao tofauti na sasa ambako wanafanya katika mazingira magumu.
“Vijana wanapoteza maisha pale Chalinze ambako kwa mwaka jana zaidi ya vijana 70 wamepoteza maisha kutokana na kukanyagwa na magari katika eneo hilo wakati wanafanya biashara zao,”anasema.

Ridhiwani anasema kupitia kilimo anataka vijana wapate ajira.Kazi kubwa itakuwa kuwezesha vijana kupata mitaji ambayo wataitumia kulima kilimo cha mazao mbalimbali.
Pia anataka awe mbunge ambaye atatengeneza mazingira mazuri ya vijana wa bodaboda kumiliki pikipiki.
Ridhiwani, anasema kuwa anataka Chalinze iwe na viwaanda ambavyo vitasaidia kutoa ajira kwa vijana wa Chalinze.
Afya.
Akizungumzia suala la afya anasema kuwa kwa kutumia Serikali ya Serilali, atahakikisha zahanati zinajengwa katika vijiji ili kupunguza umbali kutoka eneo moja kwenda jingine.
Anasema kuwa kuna baadhi ya vitongoji vipo mbali na makao makuu ya vijiji hali inayofanywa wananchi kutumia muda mwingi kutafuta huduma za afya.
Anafafanua kuwa kazi iliyopo mbele yake ni kuhakikisha zahanati zinajengwa lakini pia madaktari wanakuwepo ili kurahisisha upatikanaji wa ajira.

Anafafanua zaidi kuwa , mbali ya zahanati kuboreshwa anataka kuwepo na mfumo ambao utawezesha kuwa na madaktari ambao watakuwa wakienda kwenye vitongoji kwa ajili ya kutoa huduma za afya.
“Lazima tutengeneza mpango wa kupeleka madaktari kwa ajili ya kutoa huduma za afya.Kuiga jambo nzuri si dhambi na hili nitalisimamia vema.
Katika eneo hilo la afya anasema changamoto kubwa ni kuzidiwa kwa vituo vya afya kutokana na idadi kubwa ya wanaokwenda kupata matibabu.
Anasema kuwa Chalinze ndio imekuwa kimbilio la wananchi wa jimbo hilo na hata wale ambao wanapata ajali za magari.

“Chalinze imezidiwa maana sasa imekuwa kama Hospitali ya Rufaa, idadi ya watu kubwa kuliko uwezo wake.Hii nichangamoto kubwa .
“Nataka tuone ndani ya jimbo la chalinze tunatanua huduma za afya katika jimbo la Chalinze.Lazima tujenge zahanati kubwa lakini moja ya malengo  yangu ni kuhakikisha inajengwa hospitali kubwa,”anasema.

Pia anasema katika eneo hilo la afya kuna tatizo la upungufu wa madaktari na katika baadhi ya zahanati hakuna madaktari.
“Unakwenda katika zahanati unakuta daktari hayupo, ukiuliza amekwenda wapi unaambiwa amekwenda kuchaji simu.Kinachoonekana kauli ya kwamba kazi hiyo ni wito inaanza kupotea,”anasema.

Hata hivyo, anasema kuwa kazi iliyopo mbele yake ni kuangalia namna amayo itawezesha madaktari kukaa katika zahanati.
Anasema kwake yeye anataka kushirikiana na vijiji kuangalia namna ya kutekeleza ilani ya CCM ambayo inazungumzia ujenzi wa nyumba za madaktari.
Kuhusu afya ya akina mama, anasema , anataka kuwepo na mpango ambao utawawezesha wajawazito kujifungua katika mazingira salama.

Anasema anataka kusimamia ili kutoka Chalinze iliko na kwamba anataka aone mama baada ya kujifungua yeye na mtoto wake wanakuwa na uhakika wa kuwa salama.
“Si mara moja, mara mbili akina mama wanafiriki kwasababu ya kujifungua.Changomoto zipo nyingi ikiwemo ya umbali mrefu lakini nina uhusiano mzuri na wadau katika eneo hilo.
“Nia yangu ya dhati ni kuona napambana ili kuhakikisha tunamaliza matatizo yaliyopo katika eneo hilo, lazima mama na mtoto wawe salama na hili litafanikiwa kuwa kutengeneza mazingira mazuri ya mjazito kujifungua salama,”anasema Ridhiwani.
Elimu
Ridhiwani anasema kuwa katika eneo hilo kunachangamoto kubwa.
Anasema kuna maeneo ambapo wanafunzi wamefanya vizuri lakini wamekosa mahali pakwenda.
Anasema hawezi kuahidi kusomesha vijana wake lakini anataka kutengeneza mfumo ambao utawawezesha wanafunzi kusoma.

Anasema kupitia fedha za mfuko wa jimbo anataka kuona anasomesha vijana kati ya 50 hadi 100 kila mwaka ili wasome na hatimaye kulifanya jimbo la Chalinze kuwa na wasomi wengi.
Anasema anatambua changamoto katika sekta ya elimu.Zipo baadhi ya shule ndani ya Chalinze mazingira yake si rafiki.

Anatoa mfano kuwa kuna shule ambayo mazingira yake ni magumu kwa mwanafunzi na hata mwalimu lakini imekuwa kifanya vizuri kwa kipindi cha miaka mitatu.
“Moja ya vitu ambavyo nimepanga kuvifanya ni kujenga shule hii yote.Hii ni dhamira yangu na itakuwa mfano mzuri kwangu mimi wa kuilezea shule hiyo.

Hata hivyo anasema, changamoto nyingine katika sekta ya elimu ni walimu ambapo hawatoshi.
Hivyo atahakikisha anafanikisha upatikanaji wa walimu wa kutosha lakikubwa zaidi ni kuboresha mazingira yao.

“Nataka nishirikiane na madiwani wenzangu ili kuhakikisha walimu wanakaa katika maeneo shule.
“Katika eneo la kitaaluma bado tupo chini , lakini natambua baadhi ya shule zetu za sekondari ikiwemo ya Shule ya Sekondari Chalinze, Lugoba, Miono na  Mbwe zinafanya vizuri sana.
Barabara

Katika eneo hilo, Ridhiwani anasema kuwa hiyo ni changamoto kubwa kwani barabara nyingi hazipitiki.
Sera ya CCM inaweka wazi namna ambavyo inahitaji vitongoji kuunganishwa na vijiji vyao ili wananchi waweze kufika kwa urahisi.
“Kuna baadhi ya barabara hazipiti na ushahidi upo, kuna baadhi ya maeneo tulikwama kwa saa sita.Hata hivyo nieleza tu kwamba waliopita wamefanya kazi kubwa na jukumu lililobaki ni sisi kuendelea kuziboresha.

Hata hivyo barabara hizo zimegawanyika maeneo mawili.Zipo barabara ambazo zipo chini ya Tanrods ambazo hizo kazi yake itakuwa ni kuisimamia Serikali kujenga barabara hizo.
Anatoa mfano barabara ya kutoa Muavi kwenda Mkenge hadi Magulumatali ambapo hizo nazo zipo chini ya Tanrod.Hivyo kwa kushirikiana na viongozi wa halmashauri atasimamia ili zijengwa.

Hata hivyo anasema mpango wake wa kwanza , ni kufanikisha barabara hizo ziweze kupita na baadhi ya barabara zinahitaji madaraja madogo.
“Barabara ambazo zipo ndani ya halmashauri  hizi tutazisimamia kwa nguvu zaidi.Tunataka barabara hizi zipitike wakati wote.
“Pamoja na juhudi hizo ni wakati muafaka sasa wa kuhakikisha barabara zinatunzwa vizuri na hilo ni jambo la msingi.
Ardhi

Anaweka wazi kuwa Chalinze kuna jamii mbili ambayo ni wakulima na wafugaji.
Anasema katika kila kijiji na kila kata ambayo amepita amekutana na tatizo la migogoro ya ardhi.

Anasema kuwa imefika mahali ambapo baadhi ya maeneo ambapo hawataki kabisa wamasai na wanasema hadharani.

“Kuna maugomvi mengi ambayo yametokea, watu wamechomwa visu, mashamba yameharibiwa lakini pia kuna ng’ombe zimekufa kwasababu baadhi ya wakulima wameamua kuweka sumu kwenye mashamba yao.Ndipo ambapo hali imefikia hapo,”anasema.
Anafafanua kuwa tatizo la yote hayo , ni kwamba hakuna mpango bora wa matuzi ya ardhi.Katika eneo hilo viongozi wameshindwa kufanya kazi ya kutosha ya kuhakikisha makundi hayo yanazingatia matumizi ya ardhi.

“Jimbo la Chalinze asilimia 35 ya viongozi wa vijiji, wameondolewa na sababu yake ni moja tu wanafanya mambo ambayo hayaridhishi wananchi,”anasema.
Anaweka wazi, katika migogoro kati ya wakulima na wafugaji, kuna baadhi ya watu wamekuwa viburi.Baadhi ya maeneo mtu anaambiwa asiingize ng’ombe kwenye shamba, bado wanaingizwa.

“Hiyo ni changamoto ambayo naiona.Suluhu kubwa ya hili ni kupata mpango bora wa matumizi ya ardhi ili tuondokane na migogoro ya ardhi.
Pia changamoto nyingine katika eneo hilo la ardhi ni migogoro ya mipaka kati ya kijiji na kijiji ambapo hiyo imesababisha wananchi kutoelewana.

“Kuna matatizo lukuki ya mipaka, imefika mahali watu hawaongei .Kuna tatizo la mpaka kati ya Msolwa na Msata, kuna tatizo la mpaka kati ya kambi ya Jeshi na Kijiji cha Pongwe Sungura na vijiji vingine vingi tu,”anasema.

Anasema atakachofanya ni kukutana na viongozi wa vijiji vyote hivyo ili kuzungumzia mipaka hiyo na ikiwezekana kurudi kwenye mipaka ya asili badala ya ile mipaka iliyowekwa mwaka 2008 kwa baadhi ya maeneo ya jimbo hilo.
“Pale ambapo kutakuwa ulazima basi kinachotakiwa ni wananchi kulipwa fidia.kwa kutumia taaluma yangu nataka nishirikiane na wenzangu kumasimamia haya.
Chalinze ipangwe

Pamoja na yote hayo,Ridhiwani anasema umefika wakati kwa Chalinze kukaa katika mpangilio tofauti na sasa.
Pia anasema kuwa , umefika wakati kwa Chalinze kuwa kituo cha biashara na katika hilo anaona haja ya uwekezaji mkubwa kufanyika.

Anafafanua kuwa Chalinze ikiwa na mpango mzuri, itapunguza hata msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam, maana Chalinze ikiwa imejipanga vizuri hakutakuwa sababu ya mtu wa mkoani kufuata bidhaa Dar es Salaam wakati vitapatikana katika eneo hilo.
Umoja na mshikamano

Ridhiwani anasema kuwa, umoja na mshikamano ni jambo muhimu katika maisha yake.
Pia anasema sera ya CCM inazungumzia umoja na mshikamano na kwamba ndani ya jimbo la Chalinze kumeanza kuibuka tabia ya watu kutoangaliana vizuri.
Anasema katika jimbo hilo kumeibuka ukabila,kumeibuka tabia ya kuona hawa wazawa na wengine wakuja.

Anasema katika maisha yake, amekuwa akishuhudia namna ambavyo wananchi wa Chalinze wakiishi kama ndugu na hakukua na ubaguzi.
“Kazi yangu mimi nataka kuona mshikamano unaendelea, nataka niwe na timu ya wazee wa jimbo la Chalinze.

“Nitakusanya wazee wote ambao wanatoka katika kabila zote na makundi yote ya jimbo hili.Naanza kuona mpasuko wa mshikamano wetu
“Watu wamepasuka , imefika mahali watu wanakataana hadharani.Jambo hili kwangu sitaki kuona linaendelea Chalinze,”anasema.
Anasema nia yake ni kuona umoja na mshikamano unaendelea Chalinze.
Anataka kuona watu wanaishi bila kubaguana , na siasa za Chalinze isiwe sababu ya kutofautiana.

“Sina ugomvi na wanasiasa , na hata kampeni za Chalinze haziwezi kuwa sababu ya kulumbana .Nikiwa mbunge nataka nilete vyama vyote vya Chalinze ili tushirikiane kuleta maendeleo.

“Nipo tayari kwa matokeo ya aina yoyote , kubwa nataka tushirikiane kuleta maendeleo yetu.Maslahi yangu ni Chalinze na hao wagombea vyama vingine vya siasa nao wanataka kuijenga Chalinze yetu,”anasema.
Michezo

MOJA ya mambo ambayo mgombea ubunge wa CCM,Chalinze Ridhiwani Kikwete ni kuinua michezo katika jimbo hilo.
Akizungumza katika mikutano yake mbalimbali ya kuomba kura kwa wananchi wa jimbo hilo,Ridhiwani anaonesha dhamira njema na kuhakikisha michezo inapewa kipaumbele.
Katika kuhakikisha anafanikiwa katika eneo la michezo anasema atatumia wadau mbalimbali ili kuwezesha vijana kushiriki kwenye michezo.

Akizungumzia zaidi kuhusu michezo Ridhiwani anasema CCM imekuwa na sera ya kuhamasisha michezo kupitia viongozi mbalimbali.
Anasema anataka kurudisha kombe la mbunge ili kuwawezesha wananchi kupata fursa ya kushiriki kwenyw michezo.

Anasema jimbo la Chalinze kulikuwa na timu ya Ibo na Nyundo na kwamba anataka kuona timu hizo zinarudi.
Anafafanua inawezekana isiwe kwa majina yale yale ya zamani lakini ni vema timu hizo zikarudi katika jimbo la Chalinze.

Anasema kuwa anafahamu kuwa na kuna mashindano kwenye kata mbalimbali za Chalinze na kwa kutumia madiwani hao atakuwa akianzisha ligi ya mbunge.
Anasema anataka kuona timu ambazo zinakuwa na ushindani kwa kila kata.Wanapofika kwenye ligi ya kombe la mbunge ushindani unakuwepo.
Ridhiwani anasema malengo yake ni kuona kuna vipaji vipya katika soka ambavyo vinatoka Chalinze.

Hata hivyo anasema changamoto iliyopo hakuna uwanja wa uhakika katika jimbo la Chalinze hivyo kazi atakayokuwa nayo ni kusimamia ujenzi wa uwanja.
Anasema kuna kiwanja cha Mwenge ambacho atahakikisha kinajengwa hata kama kitaanza kuwa na uwezo wa kuingiza watu 500 na baadae wakaongezwa.
Katika eneo hilo la michezo anasema, kuwa anataka kuona wanawake nao wanashiriki kwenye michezo.

Hata hivyo, anasema kwa kutumia shule zilizopo katika jimbo hilo kutasaidia vijana kupata nafasi ya kuonesha vipaji vyao kuanzia ngazi ya chini.
“Chalinze tunazo shule za kutosha ambazo hizi tukizitumia vizuri tutakuwa na timu zenye ushindani katika soka na aina nyingine ya michezo.

“Tunataka Chalinze iwe yenye kusika kwa michezo na hata pale ambapo timu kubwa za Simba na Yanga ziweze kuchukua vijana wetu kwenye timu zao,”anasema Ridhiwani.
Anafafanua hakuna jambo nzuri kama kuona kijana anasifa kwenye michezo lakini unapouliza anatoka wapi iwe ni Chalinze.

Kwenye mikutano ya kampeni, Ridhiwani hakusita kuelewa wananchi anavyotaka kusimamia michezo na amekuwa akitaka vijana kutambua kuwa katika eneo hilo atasimamia makini.
Umoja na mshikamano

Ridhiwani anasema kuwa, umoja na mshikamano ni jambo muhimu katika maisha yake.
Pia anasema sera ya CCM inazungumzia umoja na mshikamano na kwamba ndani ya jimbo la Chalinze kumeanza kuibuka tabia ya watu kutoangaliana vizuri.
Anasema katika jimbo hilo kumeibuka ukabila,kumeibuka tabia ya kuona hawa wazawa na wengine wakuja.

Anasema katika maisha yake, amekuwa akishuhudia namna ambavyo wananchi wa Chalinze wakiishi kama ndugu na hakukua na ubaguzi.
“Kazi yangu mimi nataka kuona mshikamano unaendelea, nataka niwe na timu ya wazee wa jimbo la Chalinze.

“Nitakusanya wazee wote ambao wanatoka katika kabila zote na makundi yote ya jimbo hili.Naanza kuona mpasuko wa mshikamano wetu
“Watu wamepasuka , imefika mahali watu wanakataana hadharani.Jambo hili kwangu sitaki kuona linaendelea Chalinze,”anasema.

Anasema nia yake ni kuona umoja na mshikamano unaendelea Chalinze.
Anataka kuona watu wanaishi bila kubaguana , na siasa za Chalinze isiwe sababu ya kutofautiana.

“Sina ugomvi na wanasiasa , na hata kampeni za Chalinze haziwezi kuwa sababu ya kulumbana .Nikiwa mbunge nataka nilete vyama vyote vya Chalinze ili tushirikiane kuleta maendeleo.

“Nipo tayari kwa matokeo ya aina yoyote , kubwa nataka tushirikiane kuleta maendeleo yetu.Maslahi yangu ni Chalinze na hao wagombea vyama vingine vya siasa nao wanataka kuijenga Chalinze yetu,”anasema.

KINGOTANZANIA

No comments: