Wednesday, January 21, 2015

SHULE KUMI NA NNE ZA SEKONDARI ZA WILAYANI RUNGWE ZIMEFUNGIWA MATOKEO YA KIDATO CHA PILI

MWL LUSEKELO MKUMBWA AFISA ELIMU VIFAA NA TAKWIMU SEKONDARI WILAYA YA RUNGWE AKIONGEA NA KINGOTANZANI KUHUSU SAKATA NA SHULE KUMI NA NNE KUFUNGIWA MATOKEO YA KIDATO CHA PILI MWAKA 2014 - 2015.




Shule kumi na nne za wilayani Rungwe mkoani Mbeya  zimefungiwa  matokeo ya kidato cha pili kutokana na kucheleweshwa kwa ada ya mtihani kutoka kanda kwenda  wizarani.

Akizungumzia sakata hilo Afisa Elimu vifaa na takwimu  wa wiraya ya Rungwe Mwl. Lusekelo Mkumbwa  amesema kwamba tatizo limetokea  kwa wakaguzi wa kanda  kwa kuchelewesha  taarifa ya malipo ya ada za mitihani kwenda wizarani, na kudai kuwa waalimu wakuu wa shule hizo ndio wanaotakiwa kuwasiliana na kanda  moja kwa moja kwa ajili ya kuhakiki malipo ya ada hizo na si kufika ofisini kwake.

Afisa elimu  amezitaja baadhi ya shule zilizopatwa na  mkasa  huo na zilizoweza kufika ofisini kwake kuwa ni shule ya Lubala, Tukuyu, Masukulu, 
Bujinga,Mwaji,Mpuguso na Lufingo ambapo  shule zilizofungiwa matokeo  zimethibitisha kulipa ada ya mitihani hiyo ya kidato cha pili mwaka 2014. 

Kutokana na tatizo hili la baadhi ya shule kufungiwa matokeo  Mwl. Mkumbwa amedai kuwa  wemeshindwa kupata takwimu sahihi ya  ufaulu wa wanafunzi hao kwa mwaka 2014 na2015 kwani ni shule chache zimepata matokeo ya kidato cha pili ya mwaka 2014 na 2015.

Afisa elimu sekondari wilayani Rungwe mwl.  Mkumbwa ameitaka wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi  kuweka utaratibu maalumu na wa kueleweka wa kushughulikia masuala ya mitihani na sio kuchanganya kanda na wizara kama walivyo fanya mwaka huu kwani kanda imeshughulikia malipo na wizara  kushughulikia mitihani na matokeo ya mitihani , hivyo kusababisha makosa  kama  ya kufungiwa matokeo kwa baadhi ya shule.

Mpaka sasa wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha pili mwaka 2014 hawajaripoti shule bado wakisubili matokeo ya uhakika kama wataweza kuendelea na kidato cha tatu.
TUMAIN OBEL
KINGOTANZANIA

No comments: