Wednesday, January 21, 2015

STANDI YA DALADALA YA TUKUYU WILAYANI RUNGWE YASAHAULIKA KUKARABATIWA NA HALMASHAURI KUCHUKUA USHURU KILA SIKU KWA WATUMIAJI

USAFIRI KWA KWENDA USHIRIKA, KATUMBA, KIWIRA, MASOKO, MBAMBO, LUFILYO  NA LWANGWA HAPA NDIO STENDI KUBWA YA DALADALA ZINAPOANZIA KUELEKEA KUNAKOHUSIKA

MIUNDOMBINU MIBOVU YA STENDI YA TUKUYU MJINI HUKU HALMASHAURI IKIWA INACHUKUA USHURU KILA SIKU WA SOKO NA DALADALA TSH 500/= KWA MAGALI MADOGO NA MAGALI MAKUBWA NI SH 1000/=  KWA SIKU





BAADHI YA WAFANYAKAZI WA UJENZI WA BARABARA WAKIFURAHIA KAMERA YA KINGOTANZANIA





Wakati barabara za Tukuyu mjini  zikiendelea  kukarabatiwa kwa kiwango cha rami standi ya daladala ya magari yaendayo kiwira, ushirika, Katumba na Busokelo (karibu na ofisi ya CCM) zamani ulikuwa uwanja wa mpira wa miguu, imeonekana kusahaulika bila matengenezo yeyote na mamlaka husika wilaya ya Rungwe.

Standi hiyo imeonekana kuwa  na mashimo  yaliyojaa maji machafu na matope yanayosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika wilayani Rungwe na kusababisha kero kwa watumiaji  wa standi hiyo.

Ubovu  wa standi hiyo unatokana na Halmashauri ya wilaya ya Rungwe kubadilisha matumizi ya uwanja wa mpira wa miguu wa Tukuyu na kuwa soko la wamachinga na standi ya daladala bila maandalizi ya kuufanya uwe sehemu inayoweza kustahimili matumizi ya magari na wafanyabiashara.

Uwanja wa mpira uliogeuzwa kuwa standi na soko unapelekea madereva kupaki magari bila mpangilio na kufanya standi ionekane kuwa ni ndogo ukilinganisha na matumizi ya eneo hilo,pia kufanya abiria wapate shida katika standi hiyo hivyo huwalazim abiria kushuka  nje ya standi.

 Barabara zinazofanyiwa matengenezo ni zile  barabara zote  zinazotokea keepleft  na ile ya kutoka Makandana barabara kuu kwenda  hospital ya wilaya ya Rungwe ya Makandana kwa kiwango cha rami na zile zilizo nje ya Tukuyu mjini kama  barabara ya kutoka  Bagamoyo kwenda Katumba kipitia Lubiga na barabara ya Majengo au Bujinga kwa kiwango kisicho cha rami.

Baadhi ya barabara zimeanza kuharibika mara baada ya kumaliza kumwaga  mchanga na kushindilia na kufanya zirudi  katika muonekano wa mwanzo, na zingine kumeguka  kutokana na mvua  zinazoendelea kunyesha.

Wakizungumza na kingotanzania watumiaji wa stend ya Tukuyu kwa maana ya madereva na wamachinga wamesema kila siku halmashauri ya Rungwe inachukua ushuru  kwa kila mfanya biashara wa soko na kwa kila Gali linapotoka stendi hapo. Hivyo hadi sasa ubovu wa miundombinu ya stendi inatokana na watendaji wa halmashauri kutoichukulia maanani stendi kwa kuifanyia ukarabati zaidi ya kujipatia pesa bila ya kufanya ukarabati wa stendi ya daladala Tukuyu.

Katika kutaka kujua zaidi kuhusu muafaka wa standi hiyo na barabara zinazoendelea kujengwa  mhandisi wa wilaya alikataa kuongea na mwandishi wa Habari kwa madai  kuwa hana ruhusa ya kuzungumzia hayo na wala wao si wasemaji na kuelekeza kuwa mkurugenzi ndie mwenye uwezo wa kuzungumzia hayo na kutoa kibali cha wao kuzungumza, 

Kingotanzaniaikafika ofisi ya Mkurugenzi na  lakini ofisi ya mkurugenzi imesema kuwa kwa sasa muda wa kuongea nawe haupo (mda tuliofika ofisini kwakwe) hataweza kuzungumza wala kuonana na mtu kwani  anaenda kukagua miradi ya maendeleo vijijini.

TUMAIN OBEL
KINGOTANZANIA

No comments: