Monday, December 19, 2022

Dkt. Mpango kuzindua kongamano la Wahariri na wadau wa mazingira

 


Leo Disemba 19, 2022 Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akiwasili kwenye kongamano la wahariri na Wadau wa uhifadhi mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji Mkoani Iringa lilioandaliwa na Kituo cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na Taarifa (MECIRA)


 Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akisalimiana na HabibMchange Mwenyekiti wa Kituo cha Wanahabari Watetezi wa Raslimali na Taarifa (MECIRA) mara baada ya kuwasili kwenye kongamano la wahariri na Wadau wa uhifadhi mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji Mkoani Iringa

Makamu wa Rais Dk.Philip Mpango akikagua mabanda katika viwanja vya ukumbi wa Masiti mjini Iringa alipowasili kuhudhuria Kongamano la Wahariri na wadau wa uhifadhi wa Mazingira na Utunzaji Vyanzo Vya Maji lilioandaliwa na MECIRA.

Baadhi ya viongozi na wadau wa uhifadhi mazingira na utunzaji vyanzo vya maji wakifuatilia kwa makini kinachoendelea katika kongamano la wanahabari na wadau wa uhifadhi mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji linaoendelea katika ukumbi wa Masiti mjini Iringa

MAGAZETI YA LEO 19/12/2022

 

 











KINGOTANZANIA
0752881456

Sunday, December 18, 2022

Serikali yamega eneo la ranchi na kuwapa wananchi


Serikali imemega baadhi ya maeneo ya ranchi ya Kagoma yenye ukubwa wa hekta 50,690 na kuyarasimisha wananchi wa Kata ya Rutoro wilayani Muleba mkoani Kagera ili yatumike kwa ajili ya shughuli za makazi, kilimo na ufugaji..

Kauli hiyo imetolewa leo na Kamati ya Mawaziri wa Kisekta katika mkutano wa hadhara mazingira katika eneo la Shule ya Msingi Rutoro, Muleba .

Mkutano mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki, amesema hayo maeneo yatamegwa na kutoa wananchi kwa ushauri wa ushauri wa watalaam.

"Maeneo yatakayomegwa kwa ushauri wa kufanya maamuzi kuhusu biashara yatawekewa utaratibu wa kutuma na uongozi wa mkoa ukishirikiana na wilaya ili msigombanie kufanya jambo lolote katika maeneo hayo," Amesema Waziri Ndaki 

Katika hatua nyingine, amesema serikali imeridhia kukiacha Kitongoji cha Rwamisha B ambacho kiko wilaya ya Karagwe chenye kaya 480 ambacho awali kiliamuliwa kiondoke.

Sambamba na hilo Waziri Ndaki amewatoa hofu walioko katika ranchi ya Kagoma akiwaeleza kuwa wako salama na serikali imefanya mazungumzo na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ili uwekwe utaratibu mzuri ambao utawawezesha maeneo yatakayomegwa.

Naye, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ridhi Kikwete, amewataka wananchi kuheshimu sheria za ardhi hususani katika mpango wa maendeleo ya ardhi na kwamba kuna kazi ya kufanya katika ujenzi wa majengo ya majengo ya eneo la Rutoro yanakaa sawa.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja, amewataka wananchi wa Kata ya Rutoro kutumia ardhi waliyoyachiwa kwa maendeleo kwa miradi ya upandaji miti pamoja na ufugaji nyuki.

Ametoa wito kwa wananchi kutoyavamia maeneo yatakayoachwa kwa serikali kwa kuwa maeneo yanayotunzwa kwa faida ya kizazi cha leo na kinachokuja.

Kamati ya Mawaziri ya Kisekta imehitimisha ziara yake mkoani Kagera na itaendelea na zoezi hilo katika mkoa wa Ruvuma.

KINGOTANZANIA

0752 881456

Saturday, December 17, 2022

Punguzeni viboko na vitisho kwa wanafunzi - Dkt. Mtahabwa

Rai imetolewa kwa walimu wote wa shule za msingi na sekondari na vyuo nchini kupunguza matumizi ya viboko na vitisho kwa wanafunzi kama njia ya kufanya wafaulu katika masomo yao kwa kuwa huo si mtazamo sahihi.


Rai hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Elimu, Dkt. Lyabwene Mtahabwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili wa wadau wa Mradi wa Kuendeleza Elimu ya Ualimu (TESP) ambapo alimwakilisha Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Francis Michael 

Ameongeza kuwa walimu wanatakiwa wafahamu kuwa watoto wote hawana uwezo unaofanana hivyo wanatakiwa kuwachukulia watafute mbinu mbalimbali za kumsaidia kila mmoja.

"Maendeleo ya kweli katika nchi huletwa na elimu bora, elimu bora  huletwa na walimu bora na walimu bora sifa yao kuu ni upendo kwa wanafunzi na wadau wengine wa elimu. Mwalimu ni kioo cha jamii, amejaa hekima na busara na ni kimbilio la watu wote," amesema Dkt. Mtahabwa.

Amesema lengo la mkutano huo ni kutafakari namna ambavyo mradi umekuwa ukitekelezwa na kujadili jinsi ya kuimarisha na kuendeleza mambo yaliyotekelezwa kwa mafanikio baada ya mradi kuisha.

"Kwa hiyo siku hizi mbili tutaangalia nini kimefanyika kupitia Mradi huu wa TESP na kisha kuweka mikakati ya namna ya kuendeleza mradi huu," ameongeza Dkt. Lyabwene.

Mratibu wa Mradi wa TESP, Cosmas Mahenge amesema mradi huo unaofadhiliwa na Serikali ya Canada umejikita katika kuimarisha elimu ya ualimu, hasa katika ngazi ya Astashahada na Stashahada za Ualimu katika Vyuo vya Ualimu vya Serikali na kwamba una jumla ya zaidi ya Shilingi bilioni 90.

Ametaja kazi kubwa zilizofanywa na mradi huo kuwa ni kutoa mafunzo kwa Wakufunzi zaidi ya 1,300, kununua vifaa vya TEHAMA kwa vyuo vyote 35 vya umma na  kuviunganisha katika mkongo wa taifa wa mtandao.

Nyingine ni ujenzi wa Chuo cha mfano cha Ualimu Kabanga, ujenzi na ukarabati katika vyuo saba, kukarabati na kujenga maktaba za kisasa, maabara za Tehama na za sayansi, kuimarisha uongozi kwa kuwapa mafunzo ya uongozi kwa viongozi na maafisa Wizara ya Elimu Makao Makuu lengo likiwa kuimarisha mfumo wa kusimamia elimu ya ualimu.


Naye Mwenyekiti wa Wakuu wa vyuo vya Serikali, Tanzania Bara Agustine Sahili amesema wamenufaika na mradi huo kwa kupata mafunzo kwa wakufunzi wa vyuo vyote.

Ameongeza kuwa manufaa mengine waliyopata ni vyuo kujengewa na kukarabatiwa miundombinu ikiwemo maktaba mpya na maabara za Tehama na za sayansi.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Canada, Rasmatta Barry  ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa utekelezaji wa mradi huo ambao amesema umezingatia masuala ya mazingira na jinsia kwa kiasi kikubwa.

KINGOTANZANIA
0752881456

WHO yasema mabadiliko ya hali ya hewa yahusika na ongezeko la milipuko ya kipindupindu duniani mwaka 2022



Shirika la Afya Duniani linasema  mabadiliko ya hali ya hewa  yanahusika na ongezeko la idadi ya kesi za milipuko ya kipindupindu kote duniani  mwaka 2022.

Takriban nchi 30 zimeripoti milipuko ya ugonjwa huu unaoweza kusababisha vifo ambao umetokea mwaka huu, ambapo kuna ongezeko la juu zaidi kuliko ilivyo kawaida.

Phillippe Barboza ni kiongozi wa timu ya WHO kwa kipindupindu na magonjwa ya kuharisha. Anasema milipuko mikubwa sana ya kipindupindu imetokea sambamba na matukio mabaya ya hali ya hewa na yameonekana kuhusishwa moja kwa moja.

“Ukame mbaya sana kama vile, huko katika Pembe ya Afrika, huko Sahel lakini pia katika sehemu nyingine za dunia. Mafuriko makubwa, misimu ya mvua isiyo ya kawaida, vimbunga. Kwa hiyo, kwa mara nyingine tena, milipuko yote hii inaonekana kuchochewa na matokeo ya mabadiliko ya hali ya hewa,” anasema Barboza.

Hakuna ahueni ya haraka inayoonekana. Shirika la Hali ya Hewa Duniani linabashiri kuwa La Nina ambayo ni matokeo ya mabadiliko ya hali ya hewa itadumu hadi mwisho wa mwaka huu. Mwenendo, ambao ni kutoa ubaridi chini ya maji ya bahari, ulitarajiwa kuendelea mpaka mwaka 2023. Hiyo itapelekea vipindi virefu vya ukame na mafuriko na kuongezeka kwa vimbunga.

Hatimaye, maafisa wa afya wanaonya kuwa milipuko ya kipindupindu huenda ikaendelea na kusambaa kwenye maeneo makubwa katika kipindi cha miezi sita ijayo. Barboza anasema kuzuia milipuko ya magonjwa itakuwa ni changamoto.

Anasema uhaba wa chanjo ulimwenguni umeilazimisha WHO kusitisha kwa muda mkakati wake wa utoaji dozi mbili na kugeukia kwenye utoaji wa dozi moja. Hii itawaruhusu watu wengi zaidi kupatiwa chanjo dhidi ya kipindupindu. Hata hivyo, anasema inapunguza kipindi cha kinga ya mwili dhidi ya maambukizi.

Barboza anasema, “kwa hiyo hali itaendelea kuwepo kwa miezi kadhaa ijayo. Hakuna njia muafaka, hakuna suluhisho la ajabu na watengenezaji wanatengeneza idadi kubwa …kwa hiyo, hakuna matumaini kwamba hali itaboreka katika wiki au miezi ijayo.”

Barboza anasema ukosefu wa data unaifanya iwe vigumu kuangalia kwa usahihi idadi ya kesi za kipindupindu ulimwenguni pamoja na vifo. Hata hivyo, anaelezea habari kutoka walau nchi 14 ambazo zinaashiria kuwa kiwango cha wastani cha vifo ni juu ya asilimia moja. Ameongezea kuwa kiwango cha vifo vitokanavyo na kipindupindu ni vibaya huko Haiti ambayo ni kiasi cha asilimia mbili.

Kipindupindu ni ugonjwa mbaya wa kuharisha unaosababishwa na kula chakula kisicho salama au kunywa maji yasiyo masafi. Matibabu yake yanajumuisha kunywa maji mengi. Watu ambao ni wagonjwa sana wanahitaji kuwekea maji mwilini na kula dawa za antibiotiki. Kipindupindu kinaweza kuua ndani ya saa kadhaa kama hakikutibiwa.

KINGOTANZANIA

0752881456

Wadau 1,000 wakutana kujadili sekta ya habari nchini

 

Uploading: 450060 of 450060 bytes uploaded.



Wadau 1,000 wakutana kujadili sekta ya habari nchini
Kongamano la kwanza la sekta ya habari linafanyika leo Jumamosi Desemba 17, 2022 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam likihusisha waandishi wa habari, wahariri, wanafunzi wa vyuo vya uandishi wa habari, maofisa habari, wamiliki wa vyombo vya habari na vyama vinavyohusisha tasnia ya habari.


Dar es Salaam. Historia imeandikwa, hivi ndivyo inavyoweza kuelezwa baada ya kufanyika kongamano la la kwanza la maendeleo ya sekta ya habari lililoandaliwa na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.


Takribani washiriki 1,000 kutoka taasisi mbalimbali zinazohusisha sekta ya habari wamekutana pamoja kwa lengo la kujadili maendeleo ya sekta ya habari nchini.