Wednesday, September 4, 2013

YANGA WAWAPIGA MKWARA MZITO MBEYA CITY, MWAMBUSI AJIBU MAPIGO, ASISITIZA WAKO VITANI KUPAMBANA NA TIMU ZOTE, SEPTEMBA 14 SOKOINE “NGOMA INOGILE”

MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Klabu ya Yanga, wamewafagilia  wanandinga   wao  kwa kutekeleza majukumu yao na ndio maana wanafanya kazi kubwa kuhakikisha wanatetea taji lao walilotwaa msimu uliopita, huku wakimaliza ligi kuu kwa kuwateketeza watani wao wa jadi, Simba SC kwa mabao 2-0.

Afisa habari wa klabu hiyo Baraka Kizuguto amesema kuwa kwa sasa wanaendelea na mazoezi ya kujipanga kuelekea mchezo wa septemba 14 dhidi ya Mbeya City katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

“Yanga ndio mabingwa watetezi, washindi wa kikombe cha ngao ya jamii, mabingwa watarajiwa wa ligi kuu msimu huu, hivyo kazi ni moja tu, tunapambana na kujipanga kufanya vizuri zaidi, na kikubwa kinachotia moyo ni uwezo mkubwa wa kikosi na morali ya hali ya juu”. Alisema Kizuguto.
IMG_7295 
Mechi iliyopita, Yanga walikabwa na Wagosi wa Kaya na pichani juu, Ally Mustafa ‘ Batez’ golikipa wa Yanga akijaribu kumhadaa nahodha wa Coastal Union, Jerry Santo kabla hajapiga penati katika matokeo ya sare ya  1-1
Kizuguto ameongeza kuwa wanatambua Mbeya City imekuja kwa nguvu sana, lakini kwa Yanga bado sana na lazima cheche zao zitazimwa tu wakiwa nyumbani kwao.
Pia amewataka mashabiki wa Yanga,  nyanda za juu kusini kujitokeze kwa wingi kuwaona mabingwa  watetezi  kwani burudani kubwa itaonekana.

“Yanga ni timu ya wananchi, na kila inapocheza mashabiki wanajitokeza kwa wingi, hivyo tunaendelea kuwaomba wazidi kujipanga kuelekea kipute hicho”. Alijigamba Kizuguto.
DSC_0352 
Kikosi cha Mbeya City kilichotoka suluhu (0-0) na wakali wa Kagera Sugar kutoka Kaitaba katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania Bara, Agosti 24 Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya

.....................................................

TGNP WAJIPANGA KUMKOMBOA MWANAMKE WA PEMBEZONI KUSHIKA MADARAKA

Wanaharakati  wa  mtandao  wa kijinsia  Tanzania  (TGNP)  wakiwa katika maandamano  ya  miaka 11 ya  tamasha la TGNP nchini na maadhimisho ya miaka 20  ya harakati  za ukombozi wa mwanamke
\

WANAHARAKATI  wa mtandao   wa  jinsia  Tanzania (TGNP) wamefanya maandamano makubwa  ya kuazimisha  miaka 20 katika  kupinga  vitendo  vya ufisadi pamoja na ukandamizaji  wa  wanawake .
 
Huku mtandao  huo ukidai  kuwa  umejipanga  kuendeleza  mapambano  ili  kuwawezesha  wanawake  wa pembezoni  kuchukua  madaraka  ya  uongozi katika chaguzi  mbali mbali ili  kusaidia  kuwakomboa  wananchi  wa  pembezoni .
Mkurugenzi  mtendaji  wa  TGNP Usu  Mallya  alitoa kauli hiyo  leo   katika tamasha  la 11 la TGNP linaloendelea  katika viwanja  vya TGNP Mabibo  jijini Dar es Salaam.
 
 “Tunashuhudia  uporaji  wa  maliasili  zetu  yakiwemo  madini  katika maeneo  yetu
…sasa  tunataka  kuona Raslimali  za  Taifa  ziwanufaishe  wananchi   kwa kuzingatia   usawa  wa  kijinsia”
Alisema  lazima  wanawake  na jamii  nzima  kupambana  kuleta  mabadiliko ya  kweli ya  mwanamke na mwanaume  pamoja na  watoto huku  wakitazamwa  zaidi wale  waliopo pembezoni .
 
“….Uchambuzi  wetu  unaonyesha  kuwa  wanaozidi kubebeshwa  mizigo mikubwa zaidi ni wanawake  waliopo pembezoni ambao  TGNP  na  washirika  wengine  tumejipanga  kuendelea kuwapigania  ili nao  waweze  kufaidi matunda  ya  Taifa…
,hivyo  lengo  letu  kuwawezesha  wanawake  wa  pembezoni  kuchukua madaraka ili kuweza  kuwakomboa  wanawake  nchini “
 
Tumefanikiwa  topasa  sauti  kwa  kipindi  cha  miaka  20  sasa   katika  kupinga  vitendo  vya ufisadi pamoja na ukandamizaji  wa  wanawake .
Aidha alisema  kuwa harakati  ambazo TGNP na  washirika  wengine  wamekuwa  wakizifanya  ni zimelenga  kulikomboa  bara  la Afrika  ,kulikomboa  Taifa na  kukomboa  raslimali    za  taifa  zisiwanufaishe  watu  wachache .
Kwani  alisema  kuwa  TGNP wameanza  kupasa  sauti  katika  kuhakikisha  huduma  za  jamii  zinapatikana kwa  watu wote na  kuepuka  mfumo dume na kandamizi kwa  wanawake na  watoto toka  mtandao  huo  ulipoanzishwa  mwaka 1993.

 .....................................

ICC - Bunge la Kenya kujadili kujiondoa;

121202202625_sp_kenyatta_ruto_304x171_afp_nocredit_ca210.jpg
Bunge la Kenya limeitisha kikao cha dharura kujadili kujiondoa kwa nchi hiyo kama mwanachama wa Mahakama ya kimataifa ya Uhalifu ICC.
Naibu wa Rais wa Kenya William Ruto alikuwa amepangiwa kufika mbele ya mahakama hiyo ya ICC wiki ijayo kujibu mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu. Naye rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kufika mbele ya mahakama hiyo mwezi Novemba.(P.T)
Uamuzi huu umechukuliwa kutokana na shinikizo kutoka kwa wabunge na wanachama wa chama kinachotawala cha Jubilee kutaka kuondolewa mashtaka yanayowakabili viongozi Uhuru Kenyatta na William Ruto.
Naibu wa Spika Joyce Laboso amepanga kikao hicho kufanyika Siku ya Alhamisi. Hata hivyo hata ikiwa bunge hilo litapitisha hoja hiyo, kujiondoa kama mwanachama wa ICC, ni uamuzi ambao lazima ufikishwe kwa wananchi katika kura ya maoni.
Baada ya kupita hapo ndipo itawasilishwa kwa baraza la Usalama la Umoja wa mataifa kupata idhini na kueleza sababu kamili za kutaka kuchukua hatua hiyo, pamoja na kuwa wananchi wenyewe wameamua.
Hata hivyo kwa mujibu wa sheria za mahakama hiyo ya ICC, hata kama nchi itajiondoa kama mwanachama, kesi ambazo zilikuwa tayari zimeshawasilishwa katika mahakama hiyo kuwahusu raia wa nchi hiyo, lazima zitaendelea kusikizwa hadi mwisho na hukumu kutolewa.
Kwa hiyo hata ikiwa Kenya itajiondoa sasa, viongozi wao Uhuru Kenyatta na William Ruto bado wanayo mashtaka ya kujibu mbele ya mahakama ya ICC.

No comments: