Monday, December 30, 2013

FILIKUNJOMBE: RAIS WETU KIKWETE AMEMALIZA MGOGORO WA MPAKA ZIWA NYASA KATI YA MALAWI NA TANZANIA

Wananchi  wa Manda  wakiendelea na shughuli zao katika ziwa Nyasa
Mkazi  wa Manda  akichota maji  ziwa Nyasa


Mwalimu Dominic Haule  akiuliza bei ya  samaki kwa mvuvi  wa ziwa nyasa eneo la Manda ambapo samaki huyo alikuwa akiuzwa Tsh 5000

Wananchi  wakiongelea  katika  ziwa Nyasa  eneo la Manda
Mkazi  wa Manda  akifua ngua kando ya ziwa Nyasa  eneo la Manda
  
Samaki  waliovuliwa  ziwa  nyasa 
Mbunge  wa jimbo la  Ludewa  Deo Filikunjombe  wa tatu  kulia akiwa na mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Solomon Madaha wa tatu  kulia ,mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ludewa Bw Kolimba na  viongozi  wengine  wakitembelea ziwa  nyasa
Mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjome wa  pili kushoto akimwonyesha mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha  kushoto nchi  ya Malawi  inavyoonekana  ukiwa eneo la Manda mwambao  mwa ziwa Nyasa  baada ya  kutembelea  eneo hilo kuhamasisha  wananchi  kuendelea na shughuli zao na kuondoa hofu ya kutokea  vita ya mpaka kati ya nchi ya Malawi na  Tanzania
Na  Francis Godwi
 
MBUNGE wa  jimbo la Ludewa  mkoani Njombe Deo Filikunjombe amepongeza  jitihada kubwa  zilizofanywa na serikali ya  chama  cha  mapinduzi (CCM) chini ya Rais Dr Jakaya  Kikwete katika  kumaliza mgogoro  wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi na  kuwataka  wananchi   wanaoishi mwambao wa ziwa Nyasa  kuendelea na shughuli zao  bila hofu  yoyote.
 
Filikunjombe  alisema  kuwa serikali ya Rais  Kikwete ni  serikali  sikivu na  ndio  sababu  ya  kulishughulikia suala  hilo la mgogoro  wa mpaka kwa  wakati zaidi bila kutokea machafuko ya aina  yoyote .
 
Akizungumza kwa nyakati  tofauti na  wananchi wa kata ya Ilela na Manda wakati  wa ziara  yake ya  kusherekea pamoja na wapiga kura  wake  sikukuu ya Krismas na Mwaka  mpya juzi ,Filikunjombe  alisema  kuwa awali  baada ya  kuwepo kwa  taarifa ya Rais  wa Malawi Joyce Banda  kudai ziwa Nyasa  lote ni mali ya nchi yake  ya Malawi wananchi  wa Tanzania  wanaoishi jirani na ziwa  hilo  upande wa Tanzania  walianza kuigiwa a  hofu  kubwa .
 
Mbali ya kuingiwa na  hofu  hiyo ya kiusalama  ila  bado  walikuwa wakifanya shughuli  zao kwa hofu  kubwa na baadhi  yao kushindwa  kuwajibika  vema katika  shughuli za kimaendeleo kwa kuhofu vita kutokea .
 
Hata  hivyo  alisema  kutokana na  serikali  ya  CCM kuwa  sikivu  zaidi baada ya kubaini  suala   hilo mara  moja jitihada za  kulifanyia kazi hilo  bila kumwaga  damu  ilianza kufanyika na  kuwa  kwa  sasa Rais Kikwete amemaliza mgogoro  huo na hakuna tatizo  tena.
 
” Ninawahakikishia  wananchi  wangu  wa Manda na Ilela  pamoja na kata  nyingine  zote kama Makonde, Lifuma na  zote ambazo zipo jirani na ziwa Nyasa na  wanategemea  maisha  yao kwa kuvua  samaki na dagaa katika  ziwa  hilo ….kuendelea na shughuli  zao  bila hofu  yoyote” alisema  mbunge Filikunjombe  huku akishangiliwa na  wananchi  hao
 
Alisema  kuwa  Rais  Kikwete  amekuwa akijituma  sana katika  kuwatumikia  watanzania ila  wapo  baadhi ya   watendaji  wa serikali ambao  ni mzigo  katika  serikali yake na  wamekuwa  wakishindwa  kuwatumikia wananchi vema.
 
Filikunjombe  alisema yeye kama mbunge  na mwakilishi wa wananchi wa jimbo la Ludewa kamwe hatakubali  kuona  wananchi  wake  wanakosa  huduma za msingi kama  ilani ya CCM inavyosema kutokana na baadhi ya  viongozi  kushindwa  kutimiza majukumu  yao vema.
 
Alisema  kuwa  kwa kutumia fursa    za ziwa Nyasa  wananchi  wa maeneo ya mwambao mwa  ziwa hilo  wanaweza  kujikwamua kiuchumi kwa  kupatiwa  vitendea kazi vya kisasa kwa ajili ya uvuvi  badala ya  kuendelea  kuifanya kazi  hiyo kwa kutumia  vitendea kazi duni na kufanya  uvuvi  wao  kutokuwa na tija ya kimaendeleo.
 
Akizungumza kwa niaba ya wananchi  wenzake John Haule  alisema  kuwa  awali  walikuwa na  hofu kubwa ya  kuendelea  kufanya  shughuli za maendeleo  kutokana na hofu ya kutokea vita  ya mpaka kati ya Malawi na Tanzania na kuwa  hata  wakati  mwingine   wakiona ndege zikipita angani   walikuwa  wakiogopa kuwa  yawezekana ni ndege za  vita kutoka Malawi na  zinataka  kuwaangamiza.
 
“Tunakupongeza kwanza  wewe mwenyewe  mbunge wetu Deo Filikunjombe kwa  kutuwakilisha  vema kwa Rais Kikwete na  bungeni  pia tunataka  kuwaeleza viongozi wa CCM sisi wana Ludewa  tumechoka  kuendelea kuwa na mbunge wa  kipindi  kimoja kimoja    sisi kwa  sasa hatuhitaji mbunge mwingine zaidi yako  na kama watafanya wao  watakavyo tupo tayari  kuhama na  wewe papote”
 
Kwa  upande  wake  mkuu  wa  wilaya ya  Ludewa Juma Madaha  mbali ya kuungana na mbunge Filikunjombe  kuwahakikishia usalama  wananchi hao bado  alisema  kuwa  ni  vema  wananchi hao kutumia  mvua  zilizopo kwa  kulima mazao yanayohimili ukame kama mihogo ambayo  imekuwa ikistawi zaidi katika maeneo hayo .
 
Kwani alisema  kuwa wataalam wa  hari ya  hewa  wanadai kuwa hali  ya mvua kwa mwaka  huu  si nzuri  sana pia   upo uwezekano  wa mwakani Taifa  kutokuwa na neema  kutokana na wataalam  hao   katika uzoefu  wao  kuonyesha  miaka  yote  inayo malizika na namba 4  kuwa na tatizo la neema.

No comments: