Monday, April 28, 2014

Unyonyaji kwa mkulima; Licha ya Serikali kupiga marufuku uuzwaji wa mazao ya wakulima bila kutumia vipimo sahihi bado tatizo hilo limeendelea kuota mizizi katika maeneo mbalimbali Mkoani Mbeya huku mkulima akiendelea kuumia na kuishi kwa umaskini zaidi.

Baadhi ya wakulima wa viazi wakiwa wamejaza LUMBESA zao hakika mkulima anaibiwa anajiona je wahusika wa vipimo mpo?

Usipojaza LUMBESA sinunui kwako hapo sasa mweee mkulima apeleke kilio chake wapi? wahusika mpo tu maofisini 

Wakulima wasijue la kufanya wakiuza kwa lazima zao la viazi kwa vipimo visivyo halari kwa kumnufaisha mnunuzi

Hii ndiyo hali halisi ya LUMBESA , viazi vyote juu ya gunia ndio lumbesa ambapo mkulima kashaibiwa hapo


Soko la Tandale Tukuyu zao la Maparachichi nako hivyo hivyo bila LUMBESA hujauza



Mkulima anasubiri kuuza ndizi zake wa walanguzi





Licha ya Serikali kupiga marufuku uuzwaji wa mazao ya wakulima bila kutumia vipimo sahihi bado tatizo hilo limeendelea kuota mizizi katika maeneo mbalimbali Mkoani Mbeya.

Baadhi ya wakulima wanaoathiriwa na hali hiyo ni pamoja na wakulima wa viazi,ndizi,mahindi,ufuta,mpunga,karanga,karoti na nyanya mazao ambayo hupimwa kwa kutumia bakuli(ndonya) au debe na mara nyingine kujazwa katika magunia(LUMBESA).

Hali imekuwa na mbaya kwa wakulima hao kutokana na kutokuwa na Asasi ya kuwatetea na wafanya biashara na wachuuzi kutumia fursa hiyo kuwafuata mashambani na kuwalipa ujira mdogo na wengine kuwadhulumu wakidai watawalipa pindi mazao yatakapofika Sokoni.

Baadhi ya Wafanya biashara kutoka Mikoa mbalimbali wameanza kuingia Mkoani Mbeya na kuwarubuni wakulima kwa kununua mazao yao mashambani mwao na wao kupata faida mara tatu kwa kisingizio cha ukosefu wa usafiri.

Wakulima wa viazi wa Kata ya Itewe ni miongoni mwa wakulima waliokumbwa na dhahama hii ambapo kina mama ndiyo wamekuwa wahanga wakubwa kutokana na ukosefu wa pembejeo wamejikuta wamegeuka watumwa kwa kulipwa shilingi elfu mbili tu kwa kuvuna gunia moja la viazi.

Wameomba Benki mbalimbali nchini kuwakopesha wanawake pembejeo za kilimo kwani wao ndio wafanyaji kazi wakubwa shambani na wao ndiyo hutunza familia na wanao uwezo wa kurudisha mikopo hiyo kwa wakati.

Ombi limetolewa na wakulima hao ambao hawakupenda kutajwa majina yao kwa mamlaka za vipimo waache kukaa ofisini bali waende mashambani ambako wakilima ndiko hupata athari kubwa za kiuchumi.

Hivi karibuni Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro alipiga marufuku vipimo vya Debe na kuanza kutumia mizani hali iliyowafanya wakulima wa zao la ufuta kunufaika zaidi licha ya kauli hizi kujirudia kila mala na kukosa usimamizi madhubuti ambapo mkulima hudhurumiwa mazao yake kwa vipimo vya kiunyonyaji .

Juhudi hizo pia zimekuwa zikipiganiwa na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe kwa zao la ndizi na kahawa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Michael Kadege akipiga marufuku uuzwaji wa kahawa mbichi.

No comments: