Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia
wananchi wa mjini Singida wakati alipowahutubia katika mkutano wa
hadhara uliofanyika kwenye uwanja vya Peoples mjini humo ambapo mawaziri
mbalimbali wamehudhuria na kuwaelezea wananchi mpiango ya serikali
katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 katika mipango
ya maendeleo, Mkutano huu ulikuwa ni wa mwisho kabla ya kumalizia ziara
yake katika mkoa wa Singida hapo kesho kabla ya kuendelea na ziara hiyo
katika mkoa wa Manyara keshokutwa , Ambapo katika ziara hiyo Kinana
anaongozana na Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye,
Mawaziri waliohudhuria katika mkutano huo mkubwa ambao umerushwa moja
kwa moja na kituo cha televisheni cha Star Tv ni Dr. Charles Tizeba
naibu waziri wa uchukuzi, Amos makala Naibu Waziri wa Maji, Mwigulu
Nchemba naibu waziri wa Fedha na Uchumi na, Mbunge wa jimbo la Iramba
Mashariki na Naibu Katibu Mkuu wa CCM,Stephen Wasira Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) na Adam Malima Naibu
waziri wa Fedha na Uchumi na viongozi mbalimbali wa kitaifa na mkoa wa
Singida.
Mwigulu
Nchemba naibu waziri wa Fedha na Uchumi na, Mbunge wa jimbo la Iramba
Mashariki na Naibu Katibu Mkuu wa CCM akiwahutubia wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini Singida
leo.
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Singida
Aliyekuwa
mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Singida Mashariki Bw. Andrew Andalu
akipongezwa na Mh. Stephen Wasira mara baada ya alipotangaza kukihama
chama cha CHADEMA na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara mjini
Singida, kutoka kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mgana
Msindai, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana, Mwenyekiti wa CCM
Wilaya ya Singida mjini Khamis Nguli na Mwigulu Nchemba Naibu Katibu
Mkuu wa CCM.
Aliyekuwa
mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Singida Mashariki Bw. Andrew Andalu
akitoa ushuhuda uliomfanya aachane na CHADEMA na kujiunga na CCM.
Naibu
Waziri wa Maji Mh. Amos Makala akiwahutubia wananchi wakati akiwaelezea
kuhusu mipango ya serikali kuhusu maji katika mkutano wa hadhara mjini
Singida. Naibu Waziri wa Uchukuizi Mh. Charles Tizeba akiwaelezea wananchi mipango ya serikali katika suala la ukarabati wa reli ya kati.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa meza kuu na viongozi mbalimbali katika mkiutano huo.
Mkuu
wa mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone akiwaelezea wananchi mafanikio
yaliyopatikana katika mkoa huo chini ya ilani ya uchaguzi ya CCM.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Singida Mgana Msindai katikati na Nape Nnauye wakifurahia jambo katika
mkutano huo.
Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohamed Dewji akizungumza na wananchi wa jimbo lake f
Mwigulu
Nchemba Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Mbunge wa jimbo la Singida mjini
Mh. Mohamed Dewji wakiwa wamepanda bodaboda wakielekea kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini Singida.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulhman Kinana akishiriki kazi ya useremala wakati
alipotembelea mradi wa kikundi cha vijana seremala kinachoitwa Aikande
Workshop mjini Singida.
Mitambo
mipya ya maji katika mradi wa maji iliyofungwa katika kiiji cha Ng’aida
manispaa ya Singida katika kupunguza tatizo la maji kwenye manispaa
hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulhman Kinana akimsikiliza mhandisi wa maji wa SUWASA Mhandisi Isaack Nyakonji wakati alipotembelea na kukagua mradi huo.
Mh. Mohammed Dewaji akishiriki katika kupiga ripu kwenye shule ya sekondari ya Mughanga mjini Singida
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulhman Kinana akiondoka mara baada ya kukagua
hospitali ya rufaa ya mkoa wa Singida, kulia ni Mbunge wa jimbo la
Iramba Mashariki Mh. Mwigulu Nchemba na kutoka kushoto ni Katibu Tawala
wa mkoa wa Singida Bw. Liana Hassan na anayefuata ni mbunge wa jimbo la
Singida mjini Mh. Mohammed Dewji.
Pendael
Masai Afisa Muuguzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Singida akitoa
maelezo kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati
alipotembelea hospitali hiyo kulia ni Mwigulu Nchemba Mbunge wa jimbo la
Iramba Magharibi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua hospitali hiyo
kutoka kulia ni Pendaeli Masai Afisa Mhuuguzi wa hospitali hiyo,
Mwigulu Nchemba Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi na kutoka kushoto ni
Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Bw. Liana Hassan na mkuuu wa mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozwa na Pendaeli
Masai Afisa Mhuuguzi wa hospitali hiyo kulia nia Daktari Bingwa wa Afya
ya Mama na mtoto katika hospitali hiyo Dr. Suleiman Mutani kushoto.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Dr. Doroth Gwajima mganga mkuu wa mkoa wakati alipowasili katika hospitali hiyo.
No comments:
Post a Comment