WAGONGA Nyundo wa jijini
Mbeya, Mbeya City fc jana walitoka nyuma na kushinda mabao 3-2 dhidi ya
Academie Tchite ya Burundi katika mchezo wa kundi B wa michuano ya
CECAFA Nile Basin Cup inayoendelea mjini Khartoum nchini Sudan.
Mbeya City fc waliofika
Khartoum siku moja kabla ya mechi walianza kufungwa bao katika dakika ya
10 baada ya Rashid kumtungua kipa wao, lakini walirudi mchezoni baada
ya Paul Nonga kusawazisha bao hilo dakika 5 baadaye.
Dakika ya 27, nahodha wa
Mbeya City fc, Mwegane Yeya kama ilivyo kawaida yake alifunga bao la
pili kwa njia ya kichwa. Them Felix `Mnyama` alihitimisha karamu ya
mabao dakika ya 37 baada ya kufunga bao safi na kuwapeleka Mbeya City
mapumziko wakiwa na furaha.
No comments:
Post a Comment