Sunday, May 25, 2014

MBEYA CITY FC WAICHACHABANGA ACADEMIE 3-2, MWAMBUSI AWASIFU WANANDINGA WAKE: CECAFA NILE BASIN CUP


IMG_7961 IMG_8009 IMG_8039 IMG_8061
WAGONGA Nyundo wa jijini Mbeya,  Mbeya City fc jana walitoka nyuma na kushinda mabao 3-2 dhidi ya Academie Tchite ya Burundi katika mchezo wa kundi B wa michuano ya CECAFA Nile Basin Cup inayoendelea mjini Khartoum nchini Sudan.
 
Mbeya City fc waliofika Khartoum siku moja kabla ya mechi walianza kufungwa bao katika dakika ya 10 baada ya Rashid kumtungua kipa wao, lakini walirudi mchezoni baada ya Paul Nonga kusawazisha bao hilo dakika 5 baadaye. 
 
Dakika ya 27, nahodha wa Mbeya City fc, Mwegane Yeya kama ilivyo kawaida yake alifunga bao la pili kwa njia ya kichwa. Them Felix `Mnyama` alihitimisha karamu ya mabao dakika ya 37 baada ya kufunga bao safi na kuwapeleka Mbeya City mapumziko wakiwa na furaha.

No comments: