Wednesday, August 20, 2014

MWINYI,SERIKALI HAIKUFUTA AZIMIO LA ARUSHA

4488510_orig
Na Joseph Ishengoma

Rais wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi amesema serikali haijawahi kufuta Azimio la Arusha kama inavyodaiwa na baadhi ya wananchi, bali ilizimua azimio hilo kuwapatia viongozi wa kati uwezo wa kumudu makali ya maisha.
“Serikali haikufuta Azimio la Arusha. Ililizimua azimio hilo kuwapatia viongozi wa kati kumudu makali ya maisha, lakini baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia vibaya nafasi hiyo kuvunja sheria ya maadili ya viongozi,” amesema.
Alhaji Mwinyi ameeleza hayo leo jijini Dar es Salaam katika semina ya siku moja ya maandalizi ya sheria ya kudhibiti mgongano wa maslai miongoni mwa viongozi na watumishi wa umma iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Maadili ya viongozi.
“Baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya nafasi hiyo kuvunja maadili ya viongozi wa umma kwa kutumia raslimali za umma kujinufaisha. Tabia hii imewafanya wananchi kutokuwa na imani na viongozi wao,” amesema.
Kwa mujibu wa Alhaji Mwinyi, mgongano wa maslai ini tatizo kubwa nchini linalotakiwa kuangaliwa kwa umakini vinginevyo baadhi ya viongozi wataendelea kujinufaisha kwa kutumia nafasi zao kazini.
Kwa upande wake Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya viongozi Jaji Salome Kaganda amesema lengo na makusudi ya mapendekezo ya sheria hii ni kuleta amani na utulivu wan chi.
Jaji Kaganda amesema, “mapendekezo ya sheria hii hayalengi kuwafanya viongozi kuwa maskini, bali kasi yao ya ukwasi iendane na halii halisi ya kipato chao.”
“Sheria hii itakapopitishwa na ngazi husika, itapunguza ubinafsi wa viongozi walioko madarakani kujipendelea wenyewe na maeneo wanayotoka,” amesema na kuongeza kuwa, “Lazima kuwepo na hatua uya serikali kurejesha maadili ya maadili. Kama itazingatiwa na kuheshuimiwa, taifa litafikia maendeleoo ya haraka yaliyokusudiwa.”

No comments: