Monday, January 26, 2015

WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA YAJIZATITI KULINDA MAZINGIRA KWA KUGAWA MITI MBALIMBALI BILA MALIPO KWA WANANCHI WAKE

HALMASHAULI YA RUNGWE YAOTESHA MICHE YA MITI MBALIMBALI NA KUIGAWA KWA WANANCHI NA TAASISI ZA SERIKALI NA BINAFSI.
AFISA MISITU WILAYA YA RUNGWE CSTOLY MAKEULA  MWENYE DAFTALI AKIWA ANAGAWA MITI KWA WANANCHI MBALIMBALI  WALIOJITOKZA KUPATA MITI BULE  NA KUIPANDA KATIKA MANEO YAO
AFISA MISITU WA WILAYA YA RUNGWE CASTORY MAKEULA AKIONGOZA WANANCHI WA WILAYA YA RUNGWE KUWAGAWIA MITI BILA MALIPO ILI KUPANDA KATIKA MAENEO YAO MBALIMBALI . BWANA CASTORY AMEWATAKA WANANCHI KUWA WAAMINIFU KUIPANDA VIZURI MITI NA KUITUNZA VIZURI



WANAFUNZI MBALIMBALI WAKIONGOZWA NA SCAUT WAKIWA MAKINI KUPATA MICHE YA MITI KWENDA KUPANDA MASHULEN KWAO

WANANCHI MBALIMBALI WAKIONGOZANA NA WAHESHIMIWA MADIWANI WAKIWA WANAANGALIA UGAWAJI WA MITI UKIENDELEA MWENYE TRACK YA KIJANA NI MHE DAUD THOMAS KASIGILA AKIWA MAKINI KUANGALIA MGAO WAKE WA  MITI ATAKAYO KABIDHIWA NA KUIPANDA KATIKA MAENEO YAKE YA KATA

Tafiti zinaonyesha kuwa takribani Hekta milioni 44 za misitu hupotea kila mwaka nchini, ambayo ni hasara inayotokana na uharibifu wa ardhi, hasara hii kubwa kwa Taifa hususan kwa mkulima aliyeko kijijini inahitaji matumizi endelevu ya ardhi yatakayosaidia kupambana na kuenea kwa hali ya jangwa na ukame na kuongoa ardhi iliyoharibika.



WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA YAJIZATITI KULINDA MAZINGIRA KWA KUGAWA MITI MBALIMBALI BILA MALIPO KWA WANANCHI WAKE

Wilaya ya Rungwe kupitia ofisi ya mali asili  imeotesha miche ya miti mbalimbali na  kuigawa bila malipo yeyote miche laki moja na thelathini kwa wakazi wa wiraya ya Rungwe kwa kujumuisha taasisi zote za kiserikali na taasisi binafsi pamoja na wananchi wa kawaida ambao ni wakazi wa wiraya ya Rungwe.

Taasisi zilizohusika ni pamoja na mahakama,shule za msingi na sekondari vyuo,vivijiji, kata, makanisa, magereza na  takukuru. Na idadi ya wananchi walio husika katika kugawiwa miti ni wananchi  mia mbili kumi na nane. Na aina ya miche iliyotolewa ni misindano ambayo ndio mingi zaidi, mipodo na miti ya matunda mbalimbali.

Idadi ya miche iliyogawiwa mwaka huu imeongezeka ukilinganisha na mwaka jana kwani miche ya mwaka jana 2014 ilikuwa miche laki moja na ishirini na mwaka huu ni miche laki moja na therathini, hii inatokana na wananchi kutambua na kupata uelewa wa kupanda miti.

Afisa misitu wilaya ya Rungwe Bwana Castory Makeula amesema kwamba  mwaka  fedha wa 2014 na 2015 wameweza kufufua mashamba ya halmashauri yalioko simike yenye ukubwa wa hekta kumi kutokana na bajeti waliyokuwa wamepewa na kupanda miche elfu nane ya miti.

Bwana Castory ameomba Serikali kupitia Halmashauri ya wilaya Rungwe kuongeza bajeti  katika mwaka wa fedha wa 2015 na 2016 ili kuweza kufufua mashamba mengine ya Halmashauri ili waweze kupanda miti mingi zaidi kwani mahitaji ya wananchi kupanda kiti wilayani Rungwe ni makubwa ukilinganisha na miche ya miti mbalimbali inayozaliswa kwa sasa.


TUMAIN OBEL

KINGOTANZANIA

No comments: