Thursday, February 5, 2015

UJENZI WA MAABARA WAFIKIA ASILIMIA 95 WILAYANI RUNGWE


AKITOA TAARIFA YA SERIKALI KWENYE BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA RUNGWE MKUU WA WILAYA YA RUNGWE AMESEMA KUWA WILAYA YA RUNGWE IMEFIKIA ASILIMIA 95% YA UTEKELEZAJI WA UJENZI WA MAABARA


MOJA YA MAABARA ZILIZOJENGWA KATIKA SHULE YA SEKONDARI TUKUYU


PAMOJA NA UJENZI ULIPOFIKIA KWA 95% NI ASILIMIA TANO TU ZIMEBAKI  KUKAMIRISHA UTENGENEZAJI WA SAMANI NA KUPATIKANA KWA VIFAA VYA MAABARA

KIWANGO CHA UFAURU KWA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA RUNGWE IMEFIKIA 73%  KITAIFA




Agizo la Mheshimiwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr Jakaya Mrisho Kikwete la kujenga maabara tatu kwa kila shule ya sekondari umekamilika kwa kiwango cha asilimia 95 mpaka sasa katika harmashauri ya wilaya ya Rungwe na shule ambazo bado wapo katika hatua za mwisho za ujenzi wa maabara.

Na kuweka azimo kwamba ifikapo tarehe ishirini na nane ya mwezi huu wanne shule zote za halmashauri ya wilaya ya Rungwe ziwe zimekamilisha ujenzi huo kabla ya kufikia agizo la Mhe. Rais la mwezi  wa sita ili kujipanga na ujenzi wa maktaba kwa kila shule.kwani serikali imetoa vitabu ishirini na tano  elfu vya sayansi katika shule za Halmashauri ya wilaya ya Rungwe.

 Akiongea na madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe katika baaraza la madiwani mkuu wa wilaya Mhe.Chrispin Meela amesema kuwa Ujenzi wa maktaba ni lazima ufanyike ili usaidie kuondokana na kutunza vitabu kwenye ofisi ya mkuu wa shule kwani kunapelekea wanafunzi kutopenda kusoma kama itakavokuwa vikiwekwa maktaba wanafunzi watakuwa huru kujisomea muda wowote pamoja na siku za wikiendi.

Mhe.Meela ameongeza kuwa matokeo ya darasa la nne kwa mtihani ulofanyika mwaka jana Halmashauri ya wilaya ya Rungwe imeshika nafasi ya kwanza katika Halmashauri kumi na kwa darasa la saba Halmashauri imeshika nafasi ya pili kimkoa na kiwango cha ufauru kimeongezeka na kufikia 51.2%.hivyo amewataka walimu wa shule za msingi kuongeza juhudi katika ufundishaji ili kuongeza kiwango cha ufauru na kufakia kiwango kama cha shule za sekondari zenye kiwango cha ufauru wa 73%.

Mkuu wa wilaya amewagiza madiwani na waratibu kata wa elimu kusimamia na kufuatilia  ufundishaji mashuleni kwa kutembelea shule na kukagua maandalio ya somo kwani walimu wengi hufika mashuleni lakini hawafundishi na kukagua nidhumu za walimu hasa walimu wapya, kwa walimu watakao kiuka wafikishwe kwa mgurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Rungwe na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

TUMAIN OBEL
KINGOTANZANIA

No comments: