Thursday, April 30, 2015

SIMU ZA MKONONI ZINAWEZA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI


index 
Mahmoud Ahmad Arusha
………………………………..
Imeelezwa kuwa elimu ya juu inaweza kuchangia watu wote kupata elimu hapa nchini ikiwemo matumizi ya simu za mkononi na utandawazi kama matumizi sahihi ya teknolojia na kuwafikia wananchi wengi hata vijijini.
Kauli hiyo imetolewa na makamu mkuu wa Taasisi ya Nelson Mandela Prof.Botrun Mwamila wakati wa hitimisho la mkutano uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na serikali ya Sweden na vyuo vikuu vya nchi hiyo uliofanyika chuoni hapa kwa siku tatu kujadili teknolojia inavyoweza kusaidia kuweza kupata elimu.
Prof.Mwamila alisema kuwa elimu ya vyuo vikuu kama itatumiwa vizuri na wasomi wetu hapa nchini inaweza kuwasaidia wananchi wengi wa madaraja yote kuweza kupata elimu kusudiwa na hivyo kuweza kurahisisha maendeleo na ukuaji wa kiuchumi.
Alisema kuwa katika mkutano huo wamejadili mambo mbali mbali yatakayosaidia kuweza kutoa elimu kwa urahisi kuwafikia wananchi  kwa kutumia teknolojia ya simu za mkanoni ambazo wananchi wengi wanazo hata vijijini.
“Teknolojia na utandawazi ukitumiwa vizuri unaweza kusaidia katika ukuaji na upatikana wa elimu hivyo kuondoa matatizo yatokanayo na wananchi kutoweza kupata elimu na kushindwa kuchangia shemu ya maendeleo”alisema Prof.Mwamila.
Aidha alisema kuwa  maazimo yaliotokana na mkuatano huo  yatakuwa ni sehemu ya Agenda ya mkutano utakaofanyika nchini Korea Kusini ambapo suala la elimu kwa wote bila ya kujali jinsia litapewa kipaumbele katika majadiliano ya mkutano huo.
Akatanabaisha kuwa ukuaji wa elimu na matumizi ya utandawazi ikiwemo simu za mkononi na matumizi ya mtandao wananchi wakiacha kutumia kwa matumizi yasiofaa na wakageukia kutumia kwa kujipatia elimu maendeleo ya haraka yatapatikana hapa nchini na hivyo kila mwananchi kwa daraja lake atasogea kiufahamu.

No comments: