Sunday, August 23, 2015

Serikali yamiliki kiwanda cha general tyre kwa asilimia 100


indexx 
Na Lorietha Laurence-Maelezo
………………………………………….
Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kumiliki kiwanda cha kutengeneze magurudumu ya magari cha General Tyre kwa asilimia 100 baada ya kununua hisa 26zenye thamani ya Dola Moja milioni kutoka kwa kampuni ya Continental AG.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya Msajili wa Hazina wakati wa makabidhiano ya nyaraka za ununuzi wa hisa hizo Katibu Mkuu Kiongozi ,Balozi.Ombeni Semfue anasema jitihada za kuhakikisha kuwa serikali inamiliki hisa hizo zilianza tangu mwaka 2012 kwa kufanya mazungumzo ya awali na mwekezaji.
 
“Kufuatia hatua hii ya kuweza kumiliki hisa kwa asilimia 100 sasa tutakuwa na fursa ya kuzalisha magurudumu yetu wenyewe na hivyo kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kilichokuwa kikitumia kununua magurudumu kutoka nje” alisema Balozi.Semfue.
Aidha anaendelea kufafanua kuwa hatua itakayofuata ni kutamfuata mwekezaji atakayeshirikiana na Shirika la Maendelao la Taifa (NDC) katika kuzalisha magurudumu kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
 
Balozi.Semfue anampongeza Rais Mhe. Jakaya Kikwete kwa kufanikisha zoezi zima la kuhakikisha serikali inamiliki hisa za kiwanda cha General Tyre kwa asilimia 100 na hivyo kufufua uchumi wa jiji la Arusha na Taifa kwa ujumla.
Naye Msajili wa Hazina Lawrence Mafuru anasema mpaka serikali kuweza kumiliki hisa hizo ni hatua kubwa sana kutokana na vikwazo mbalimbali vilivyokuwa vikiwekwa na mwekezaji wa kiwanda hicho kilichoanzishwa mwaka 1969.
 
“Haikuwa kazi rahisi kumiliki hisa hizi bila ya jitihada kubwa iliyofanywa na serikali katika kumshawishi mwekezaji baada ya kuona hana kuwa hakuwa tayari kuwekeza na hivyo kurejesha umiliki kwetu” alisema Mafuru.
Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Mhe. Uledi Musa, anaeleza kuwa kiwanda hicho kitatoa fursa za ajira zaidi kitakapoanza kuzalisha tofauti na awali ambapo kiliweza kuajiri wafanyakazi 360

No comments: