Thursday, June 15, 2017

Wahamiaji 1000 waokolewa pwani ya Libya


Image captionWahamamiaji huwa na imani ya kupata maisha bora zaidi Ulaya
Vikosi vya uokoaji vinavyofanya kazi katika pwani ya Libya vimeokoa zaidi ya wahamiaji elfu moja kwa siku moja.
Walikuwa katika boti dogo lililokuwa likielekea Ulaya.
Miongoni mwa waliookolewa ni raia mia moja wa Bangladesh waliokuwa katika boti ndogo na ya wazi.
Italia imepokea zaidi ya wahamiaji elfu sitini na tano kwa kipindi cha miezi sita iliyopita.
Kukabiliana na hilo,serikali ya Italia imepanga kujenga vituo zaidi ya mia sita vitakavyokuwa vikikaliwa na wahamiaji.

No comments: