WABUNGE-KUKATAA POSHO NI UNAFKI
|
Mhe Peter Serukamba |
Mbunge
wa Kigoma Mjini kupitia CCM Mhe Peter Serukamba amesema suala la baadhi
ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupinga posho
lilikuwa ni unafiki. Serukamba aliyasema hayo katika kipindi cha
Makutano kinachoendeshwa na Fina Mango kupitia Magic FM. Fina aliuliza
moja ya swali kutoka kwa wasilizaji ambapo alisema biashara ya kukataa
posho ni unafiki tu huku akimwambia Fina ataje mbunge gani karudisha au
kukataa posho, alisema "Tumeongezewa mafuta tumechukua, tumeongezewa
vingine tumechukua hakuna ambaye amerudisha na next day ilipokuwa
confirmed wengine wakaanza kukopa" huku akisema hakuna umuhimu wa
kupinga posho za wabunge badala yake wabunge waombe serikali iwaongezee
posho na watumishi wengine.
Alipoulizwa kwa nini wasiiombe serikali ianze na sehemu nyingine kabla
ya kuwaongezea mshahara wabunge akitolea mfano wa shirika la ndege la
taifa ATCL Serukamba alijibu kuwa siku zote binadamu anaanza na "mimi"
kabla hujawafikiria wengine akikumbushia siku alivyopendekeza kama
bunge lifungwe kama watu hawataki wabunge wapokee posho na kuishia
kushambuliwa kupitia mitandao ya kijamii. Serukamba aliongezea kusema
kuwa bunge la Tanzania ni kati ya mabunge yanayolipa hela ndogo sana
watumishi wake ambazo ni milioni mbili tu kwa mwezi bila posho na kusema
wanazidiwa na bunge la nchi ya Burundi wanaolipwa dola 4,500 za
Marekani.
Alimalizia kwa kusema jukumu la wabunge libaki kuwa kutekeleza wajibu
wao wa kibunge ambao ni kutunga sheria na kuisimamia serikali itekeleze
wajibu wake.
Photo Caption
1. Mhe Peter Serukamba akikongea katika kipindi cha Makutano
No comments:
Post a Comment