Monday, March 18, 2013

KAMPUNI YA SIMAMIA YASHUSHA MABANGO YA MATANGAZO YA KAMPUNI YA COCACOLA TAWI LA MBEYA KUTONANA NA KUDAIWA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 102



Kampuni hiyo ya simamia ikiendelea na kazi ya kufuta maandishi ya kampuni ya cocacola kwa kutumia rangi nyeusi

Moja ya wakurugenzi wa kampuni ya simamia akiongea na mfanyakazi wa kampuni ya cocacolamwenye kitambulisho shingni akiulizia kulikoni mbona mnatoa mabango yetu? alipata jibu la halaka toka kwa mkurugenzi huyo kuwa mnadaiwa matangazo ya mabango tunayotoa

Mtumishi huyo wa kampuni ya cocacola nae akaungana na sisi katika kupiga picha utoaji wa mabango hayo ya kampuni yao 


Moja ya maafisa wa kampuni ya cocacola alipita hapo kituo kikuu cha mabasi ya kwenda mikoani na kujionea mwenyewe mabango yakitolewa cha ajabu mbeya yetu iliwasiliananae kwa simu jibu alilotupa kuwa hana habari kama mabango yao yanatolewa ilibidi tushangae maana picha ni hii wakati akipita standi hiyi ya mabasi akijionea uondoaji wa mabango yao


Mbali na hapo alienda moja kwa moja katika kampuni ya simamia lakini hakushuka kwenye gari yake akaondoka  kwa kasi mambo hayo




Kazi inaendelea ya kushusha mabango ya matangazo ya biashara ya kampuni ya cocacola mbeya


Mkurugenzi wa   Wakala wa kukusanya ushuru wa mabango ya biashara na Hoteli  Jiji la Mbeya Simamia Company Limited, Ndugu  Aloyce Mrema amesema kampuni yake inatekeleza sheria ya jiji ambayo inataka kila bango la tangazo linatakiwa kulipiwa.




Halimashauri ya jiji la Mbeya kupitia wakala wa ukusanyaji wa  ushuru wa mabango SIMAMIA imeyashusha mabango ya kampuni  ya Vinywaji baridi ya Cocacola tawi la Mbeya kutokana na kudaiwa zaidi ya shilingi milioni 102.
Hata hivyo kampuni hiyo iko   hatiani kuburutwa mahakami kwa kushindwa kulipia gharama za mabango ya matangazo  yaliyowekwa maeneo mbali mbali ya Jiji hilo .
Kampuni hiyo imeshindwa kulipia gharama za kuweka matangazo hayo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2012 – 2013 ambapo deni limefikia Shilingi Milioni 102 ambazo walitakiwa kuzilipa kutokana na wingi wa mabango hayo.
Akithibitisha kudaiwa kwa kampuni hiyoMkurugenzi wa   Wakala wa kukusanya ushuru wa mabango ya biashara na Hoteli  Jiji la Mbeya Simamia Company Limited, Ndugu  Aloyce Mrema amesema kampuni yake inatekeleza sheria ya jiji ambayo inataka kila bango la tangazo linatakiwa kulipiwa.
Amesema kutokana na Kampuni ya Cocacola kushindwa kulipia mabango hayo kampuni ya Simamia imeamua kutoa mabango yote yaliyondani ya Jiji la Mbeya ambapo alisema hatua itakayofuata ni kuifikisha mahakamani kampuni hiyo kwa kushindwa kutekeleza agizo la Halmashauri ya Jiji.
Amesema kabla ya kuanza kutoa mabango hayo wameshapeleka  barua za kuwakumbusha zaidi tatu lakini bado hawakuitikia wito wa kulipa mapema gharama hizo zilizowataka hadi ifikapo Machi 18, Mwaka huu kutoa majibu au kulipia mabango hayo.
Mrema amesema utaratibu wa kampuni hiyo ni kuhakikisha kuwa kila kampuni iliyoweka bango la biashara katikati ya Jiji la Mbeya inalipa gharama kwa mujibu wa Sheria za Jiji ambapo kwa takayeshindwa kufanya hivyo atachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.
Aidha ametoa wito kwa makampuni makubwa kuheshimu sheria za nchi na siyo kukiuka kutokana na kuwa na fedha nyingi ambapo aliongeza kuwa kwa sasa zaidi ya makampuni sita makubwa ya Jiji la Mbeya yameshapewa barua za kuwakumbusha kulipia mabango hayo.
Hata hivyo ameyataja makampuni hayo kuwa ni pamoja na makampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Vodacom, Airtel,Zantel, Tbl na Pepsi ambayo yameshapewa barua za kuwakumbusha kulipia mabango hayo yakiwemo makampuni ya watu binafsi.
Akizungumzia hatua hiyo Ofisa wa Cocacola aliyejitambulisha kwa jina moja la Zekaria amesema hajui lolote kuhusu kuondolewa kwa mabango ya kampuni yake na wakala wa Jiji Simamia ambapo amesema atalifuatilia na kulipeleka kitengo kinachohusika kwa ajili ya kulitolea taarifa.
Hata hivyo Ofisa huyo alionekana kukwepa kutokuwa na taarifa juu ya kampuni hiyo kung’oa mabango ili hali baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo walionekana wakipiga picha na kufuatilia hatua zote zilizokuwa zikifanyika.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Haslmashauri ya Jiji la Mbeya Juma Iddi alipoulizwa juu ya utaratibu wa kampuni hiyo wa kutoa mabango ya biashara ya kampuni ya Cocacola amesema hajui lolote kwa sababu kampuni ya Simamia  ilishinda tenda ya kukusanya ushuru wa Hoteli na mabango ya biashara hivyo yeye hana uwezo wa kuingilia.
Na Mbeya yetu
 
WATANZANIA WENZETU WANAISHI NA KUTESEKA NA UGONJWA WA UKOMA MAKETE WILAYANI RUNGWE WANAHITAJI MISAADA KWA JINSI MTU ATAKAVYOJISIKIA
BAADHI YA WAGONJWA WA UKOMA WAKIWA WANASUBIRI KUPEWA MISAADA NA WASAMALIA WEMA JUMUIYA YA AKINA MAMA UMOJA WA MAKANISA WILAYANI RUNGWE CCT
SERIKALI KUPITIA TAASISI YA MSALABA MWEKUNDU ILIJENGA MAJENGO HAYA  MWAKA 1850 KUWA KITUO WA WAGONJWA WA UKOMA WALIOKUSANYWA HAPA KITUONI KUTOKA SEHEMU MBALIMBALI ZA AFRIKA LAKINI BAADA YA MWAKA 1931 SERIKALI KUTANGAZA KUISHA KWA UGONJWA WA UKOMA MAJENGO HAYA YAMETELEKEZWA  BILA YA SHUGHURI YEYOTE ILE
LEO NIMETEMBELEWA OFISINI KWANGU NA UONGOZI WA  WANAWAKE WA UMOJA WA MAKANISA CCT KATIBU MAMA ROSTA MWANKENJA NA MWENYEKITI WAKE  ANNA CHARLES. ZIARA HII IMEKUWA NI KWA AJILI YA UMOJA HUO WA WANAWAKE KUTEMBELEA WAGONJWA WA UKOMA NA KUJITOLEA MISAADA MBALIMBALI HII IMEKUWA HII IMEKUWA FARAJA KWA WAHANGA HAWA WA UKOMA AMBAO WANAHITAJI MISAADA MINGI HASA YA MATIBABU, MAVAZI NA CHAKULA HUKU KILIO CHAO NI KUONA SERIKALI IMEWASAHAU MIAKA MINGI IKIAMINI ENEO HILO WAGONJWA WA UKOMA HAWAPOVIONGOZI WA CCT WILAYA YA RUNGWE WANAAMINI WATANZANIA NI WATU WA UPENDO NA FARAJA HIVYO OMBI LAO NI KUSHIRIKIANA NAO KATIKA KUTOA HUDUMA MBALIMBALI KWA WAGONJWA HAWA MAANA NI WATU WASIO JIWEZA KUJITEGEME KUFANYA KAZI. HIVYO WATU WALIO NA MAPENZI MEMA NA WATU WASIO JIWEZA BASI KAMA UNAHITAJI KUUNGANA NA KUJITOLEA CHOCHOTE AU UNAHITAJI KUFIKA KWA WAHANGA HAWA BASI WASIRIANA NA UONGOZI WA CCT KWA NAMBA HIZI. ROSTA MWANKENJA 0755766183 KATIBU, NA ANNA CHARLES 0752282464 MWENYEKITI WA CCT WANAWAKE WILAYA YA RUNGWE.
IBADA YA KWELI NI KUWAONA NA KUWAJARI WAHITAJI NA WASIJIWEZA

No comments: