Thursday, March 14, 2013

WATANZANIA FEKI WAWATESA WATANZANIA HALISI NCHINI CHINA

14. KINANA AKIWA NA WATANZANIA WAISHIO CHINAa 
NA BASHIR NKOROMO, DOGGUAN, CHINA

WATANZANIA wanaoshi nchini China wametakiwa kukiwa na mshikamano mkubwa na kuitangaza Tanzania kwa kuonyesha tabia njema katika matendo kwa wenyeji wao.
Akizungumza na Wanajumuia ya Watanzania wanaoishi China, baada ya kukutana nao katika mji wa Dongguan, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alisema, wasipokuwa na mshikamano na kuwaonyesha tabia njema wenyeji wao, Wataharibu sifa ya Tanzania Kimataifa ambayo inafahamika kwamba ni nzuri kwa miaka mingi.

Kinana ambaye hupo nchini China na ujumbe wa watu 14 kwa ajili ya ziara ya mafunzo katika nyanja mbalimbali, alikutana na Watanzania hao, baada ya kuamua kumtembelea katika hoteli ya Exhibition International hoteli, jana, Machi 12, 2013, ili kumsalimia na kubalishana naye mawazo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Watanzania hao walisema,  wamekuwa wakiishi nchini China kwa mahusiano mazuri kutokana na maadili waliyolelewa nayo ya Kitanzania, lakini hali hiyo huenda ikaingia dosari kutokana na kuwepo Watanzania ‘feki’ ambao wamekuwa wakiingia China kwa pasi za Tanzania na kufanya maovu.

“Hawa Watanazania bandia wakiishaingia hapa hujitambulisha kuwa ni Watanzania, hata wakiulizwa pasipoti ya Tanzania wanayo, lakini cha ajabu ukiwauliza wanakotoka Tanzania wanababaika na hata lugha ya Kiswahili hawajui sawasawa. Utamkuta mtu anajua kusalimia tu, anasema ‘mambo’ basi, sasa jamani kuna Mtanzania ambaye hawezi kuzungumza kiswahili, lakini akawa na uwezo wa kuja ugenini kama huku?” alisema Katibu wa  Jumuia wa Watanzania hao waishio China, David Chgamla.

Alisema, kutokana na hali hiyo, Wachina sasa wameanza kupunguza imani yao kwa Watanzania kiasi kwamba mtu anapojitambulisha kuwa ni mtanzania wakati akiihitaji huduma anatazamwa mara mbili mbili kuthibitisha uaminifu wake.

Akizungumzia baadhi ya Watanyabiashara kutapeliwa au kuziwa bidhaa zisizo na ubora au kwa bei isiyo halali, Katibu huyo alisema, wengi wanakutana na mikasa hiyo kwa sababu wanakifika China wanakwenda mahali ambapo siyo sahihi kwa mahitaji yao na hivyo kutahamaki wakiingia hasara.
“Lakini Ndugu Kinana, Jumuia hii tuliyounda hivi karibuni na kuwa na uongozi huu mpya, nina imani itawasaaidia Watanzania wengi kutopoteza fedha au mali zao wanapokuwa wamekuja hapa kibiashara, kwa sababu tunajipanga vema kuhakikisha kila atakayekuwa anakuja  akipenda anakutana na sisi kwa ajili ya msaada”, alisema.
Uongozi wa Wanajumuia hiyo ya Watanzania unaundwa na John Luhumbiza (Mwenyekiti), Abraham Merishani (Makamu Mwenyekiti),  David Chamla (Katibu Mkuu) na Msaidizi wake ni Aboubakari Mwinyi.

WAKATI HUOHUO

CHINA YAITABIRIA TANZANIA KUPIGA HATUA

Mtumishi katika mnara wa Canton, mrefu kuliko yote nchini China na watatu duniani kwa urefu, Sarah Xie, akimuonyesha mandhari ya jiji la Guangzhou, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, wakati Kinana na ujumbe wake walipopanda hadi mwisho mnara huo wenye urefu wa zaidi ya futi 100, Machi 13, 2013. Wengine Kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine shigella. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo). 3. KINANA NA UJUMBE WAKE NDANI YA MNARAa 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakitazama maumbo ya mandhari ya mji wa Guanzhou, China, yaliyopo ndani ya mnara wa Cnton wenye urefu wa zaidi ya mita 100, walipotembelea mnara huo, Machi 13, 2013.  Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo). 10. DK. MIGIRO NA MAOFISA WA IDARA YA MAMBO YA NJE WA DONGGUANSABINA LIU (L) NA SARAH XIEa 
Katibu wa NEC, Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa mjini Magharibi, Yussuf Mohamed Yusuf wakitazama bidhaa zinazouzwa kwenye kilele Mnara wa Canton ambao ni mrefu kuliko yote nchini China ukiwa na urefu wa zaidi ya mita 100, mjini Guangzhou, China. Dk. Asha-Rose Migiro na Yusuf ni miongoni mwa viongozi walioambatana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana katika ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo). 13. KINANA NA MIGIRO WAKIWA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WA-TZ WAISHIO CHINA. (L) DAVID CHAMALA (KTB), JOHN LUHEMBA (MKT)-L, ABRAHAM MERISHANI MAKAMU MKT NA ABUBAKAR MWINYI KATB MSAIDIZIa 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wanachama wa Jumuia ya watanzania waishio nchini China 14. KINANA AKIWA NA WATANZANIA WAISHIO CHINAa 
NA BASHIR NKOROMO, DONGGUAN,CHINA
CHAMA Cha Kikomunisti cha China (CPC) kimeeleza matumaini yake kwamba upo uwezekano wa Tanzania kupiga hatua kubwa kichumi kama inajikita kwa dhati katika kuzitumia rasilimali ilizonazo ikiwemo ardhi.
Hayo yalisemwa Machi 13, 2013 na Kamishna wa Maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), jimbo la Donguan, China,  Cuo Jian, wakati akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake, katika hoteli ya Exhibition Internation mjini hapa.
Jian ambaye pia ni Meya wa jiji la Donguan, alisema, Tanzania kama zilivyo nchi kadhaa za Afrika, inaweza kupiga hatua kiuchumi ikiwekeza juhudi zake katika kuzitumia rasilimali ilizonazo kwa kuwa rasilimali ndiyo msingi wa kwanza katika kuinua uchumi wa nchi yoyote.
Alisema, anatambuwa kwamba Tanzania ni moja ya nchi za Afrika zenye ardhi kubwa, hivyo haina budi juhudi zake za kuinua uchumi kuzielekeza katika rasilimali hiyo ikiitumia kwa kilimo cha kisasa, kujenga viwanda na vitegauchumi mbalimbali ambavyo vitachochea kukua haraka kwa uchumi.
“Hata hivyo nawapongeza Tanzania, kwa hatua mliyofikia sasa katika kukuza uchumi, asilimia sita ya GDP, inaridhisha, la msingi serikali  kuongeza juhudi na kuwahamasisha wananchi kushiriki katika juhudi hizo”, alisema, Jian.
 

JELA MIAKA 35 KWA KUWAUA NDUGU ZAKE KWA KUWACHOMA MOTO

Na Venance Matinya, Mbeya

MAHAKAMA kuu kanda ya Mbeya  imemhukumu kutumikia kifungo cha miaka 35 Samsoni Daniel Mwang’ombe baada ya kupatikana na hatia ya kuua bila kukusudia ndugu wa familia moja wapatao saba.
Akisoma mashtaka mbele ya jaji wa mahakama hiyo Samwel Karua, Mwendesha mashtaka wa Serikali Rhoda Ngole alisema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Juni 21, 2010 kinyume cha kifungu cha 195 (16) kilichofanyiwa marekebisho Mwaka 2002.
Ngole aliiambia Mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo mwaka huo majira ya 2:00 hadi saa 2:30 usiku ambapo alifika nyumbani kwa baba yake akiwa na sigala mkononi huku akiivuta na baadaye kuidondosha sigala hiyo iliyosababisha moto kuwasha nyumba.
Aliwataja walioathirika na moto uliokuwa  umewashwa kutokana na sigala aliyokuwa ameidondosha mtuhumiwa  kuwa ni Daniel Mwang’ombe, Anitha Richard, Salome Mwang’ombe,Jane Samson, Diana Samson, Maria George na Cloud Samson.
Kutokana na kosa hilo mtuhumiwa huyo alikiri kuhusika na kwamba aliua bila kukusudia ambapo alikiri kuwa akiwa anavuta sigala alidondosha kipande hicho ambacho kilikuwa bado kinawaka moto.
Aidha Mwendesha huyo aliiambia mahakama hiyo kuwa pamoja na mtuhumiwa kukiri kusababisha vifo bila kukusudia mahakama impe adhabu kali kwa mujibu wa sheria.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo Wakili wa  upande wa utetezi Sambwee Shitambala  alisema Mahakama inatakiwa kumwonea huruma na kumpunguzia adhabu mshtakiwa kutokana nay eye  kuwa miongoni mwa wafiwa.
Alisema mshtakiwa ameondokewa na wazazi, watoto na mke katika ajali hiyo ambapo hakuhudhuria mazishi yao pia amekaa muda mrefu akiwa  mahabusu ambapo amekaa kwa miaka mitatu na kuongeza kuwa mtuhumiwa ni kijana ambaye ni nguvu kazi ya taifa hivyo hastahili kufungwa.
Hata hivyo kutokana na utetezi huo Jaji Karua alisema kutokana na hali iliyojitokeza mtuhumiwa atatumikia kifungo cha miaka mitano kwa kila tukio ambalo ni kusababisha vifo saba hivyo jumla atatumikia miaka 35.

Tupige vita rushwa ya mapenzi-jali kile

000mmmmmllll b23fa
Mhe. Jaji Engera Mmari Kileo, akizungumzia  uzoefu wa  Majaji Wanawake wa Tanzania katika kukabiliana na  tatizo la  matumizi mabaya  ya mamlaka kudhalilisha kijinsia na kushawishi rushwa ya mapenzi  ( sextortion) wakati Chama cha Majaji   Wanawake- Tawi la Tanzania  kilipoanda mkutano wa pembezoni ( side-event) sambamba na   mkutano unaoendelea wa 57 wa Kamisheni ya  Umoja wa Mataifa kuhusu Hadhi ya  Wanawake ( CSW). aliyekaa kati kati ya  Jaji Kileo, na  Naibu Mwakilishi wa Kudumu  Balozi Ramadhan Mwinyi ni,  Bw. John Hendra aliyewahi kuwa Mratibu wa UNDP nchini Tanzania,  Bw. Hendra ndiye aliyekuwa mwendashaji wa mkutano huo, bado anakumbuka vizuri kiswahili, kwa sasa ni Katibu Mkuu Msaidizi na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa   Sera na Mipango katika Taasisi ya UN- Women


Hatimae wakatoliki wapata papa mpya   Francis 1

000000000ttttttt dec9f
Kadinali Jorge Mario Bergoglio kutoka Argentina  ametangazwa kuwa Baba Mtakatifu mpya.
 http://www.voxxi.com/wp-content/uploads/2013/03/Pope-Francis.jpg
Askofu Mkuu huyo wa Buenos Aires anaitwa Francis wa kwanza.
Miongoni mwa kauli za kwanza kwa maelfu ya waumini waliokusanyika kwenye uwanja wa mtakatifu Petro Papa mpya aliwataka waumini waungane naye katika  kumwombea Papa  mstaafu Benedikt  wa 16. 
Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha takriban karne moja kwa Baba Mtakatifu kutoka nje ya bara la Ulaya.
Papa Francis wa kwanza mwenye umri wa miaka  76 anachukua nafasi ya Benedikt wa 16 aliejiuzulu mwishoni uliopita.
Papa Francis wa kwanza alichaguliwa katika siku ya pili baada ya kura kupigwa kwa mara ya tano.
Rais Obama alikuwa miongoni mwa viongozi wa kwanza duniani kumpongeza Papa Francis kwa moyo wa mkunjufu. 
Uchaguzi wa Francis wa kwanza umepongezwa pia na Rais  wa  Argentina Christina  Kirchner  aliewahi  kukwaruzana naye katika siku za nyuma juu ya masuala kama ya mashoga.
Mnamo mwaka wa 2010, Papa  Francis wa kwanza aliziita ndoa  za  jinsia sawa kuwa ni jaribio la kuuteketeza mpango wa Mwenyezi Mungu.
 
Sifa na utukufu tunamwachia mungu nami nimekuwa nafuatilia uchaguzi huu kwa mala ya kwanza nakweli yapaswa kuigwa na wengi mambo kufanyika kwa umakini na zaidi utakatifu wa Mungu maana nimeshuhudia chaguzi kadhaa za makanisa kunakuwa hakuna tofauti na chaguzi za siasa. Hii iwe somo kwa wanadinimbalimbali na wanasiasa. 
 
TUMSIFU YESU KRISTO....... 
KINGO 0752881456

WACHEZAJI 23 WAITWA TAIFA STARS KUIKABILI MOROCCO

KIM PAULSENhttp://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2013/03/MAZOEZI.jpg

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja wachezaji 23 watakaoingia kambini Jumamosi (Machi 16 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi ya mashindano dhidi ya Morocco.

 Mechi hiyo ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 Kwa mujibu wa Kocha Kim, wachezaji wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager wanatakiwa kuripoti kambini katika hoteli ya Tansoma, Machi 17 mwaka huu.

 Wachezaji walioitwa ni makipa Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba) na Shomari Kapombe (Simba).

 Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).
 Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

 Mbali ya Kim, benchi la ufundi la Taifa Stars linaundwa na Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

No comments: