Thursday, April 4, 2013

SAKATA LA KUGOMBEA KUCHINJA LAZUSHA BALAA TUNDUMA VURUGU TUPU POLICE YAWATAKA DIWANI FRENK MWAKAJOKA WA CHADEMA NA MCHUNGAJI WA KKKT NEEMA MWAIPUSA KUJISALIMISHA WENYEWE KABLA YA KUTIWA MBALONI KWA TUHUMA ZA KUCHOCHEA GHASIA HIZO


Hii ndiyo hali halisi ya Mji mdogo wa Tunduma leo kuanzia asubuhi



Matairi yanachomwa katikati ya barabara



Mambo hayo 




Mwandishi wa Mbeya yetu pamoja na waandishi wenzake walipata shida sana kufika mji wa Tunduma walikutana na vikwazo vingi sana lakini wananchi walikuwa waelewa waliwasaidia kutoa magogo na matairi ili wapite wakapate habari





ISHU NI KUCHINJA NYAMA SASA WANACHOMA NA BARABARA ZILIZOJENGWA KWA KODI ZA WATANZANIA







MIENDOMBINU YA UMEME NAYO INAHUJUMIWA











Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani akiongea na waandishi wa habari

Wanafunzi wakisindikizwa na jeshi la polisi kurudi majumbani mwao


Polisi wakiendelea kazi yao katika mitaa ya Tunduma


Baadhi ya magati ya IT yaendayo nchini Zambia yakiwa yamepakiwa nnje kidogo ya mji wa Tunduma kuogopa kuharibiwa kwa magari hayo






Diwani wa kata ya Tunduma Ndugu Frank Mwaijoka (Chadema) pamoja na mchungaji wa kanisa la KKT katika eneo hilo la Tunduma wilayani momba Mkoani mbeya wametakiwa kujisalimisha kituo cha Polisi Tunduma mara baada ya kuhusika na uchochezi wa kidini hali ambayo imepelekea kutokea kwa vurugu  katika eneo hilo.
Vurugu hizo zimeanza majira ya saa 3:asubuhi katika eneo hilo la tunduma mara baada ya kundi la watu wanaodai kuwa wao ni wafuasi wa dini ya kikristo wakidai waruhusiwe kuchinja mifugo na kuuza katika mabucha yao hali iliyo pelekea kuibuka kwa vurugu hizo.
Akizungumza kuhusiana na tukio hilko Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani amesema kuwa kufuatia kuwepo kwa tukio hilo jumla ya watu zaidi ya 40 tayari wamekwisha kamatwa .
Amesema mpaka sasa taarifa walizo zipata kufuatia vurugu hizo zinaeleza kuwa miongoni mwa watu walichochea vurugu hizo ni diwani wa kata hiyo ya Tunduma Ndugu John mwaijoka pamoja na Mchungaji wa kanisa la kkt ndugu Neema Mwaipusa ambao kwa pamoja wametakiwa kujisalimisha kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.
Amesema suala hilo limegubikwa  na siasa kwani tayari viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa mkoa huo Ndugu Abbas Kandoro amekwisha litolea ufafanuzi Apri 02 mwaka huu wakiwepo pia viongozi wa dini .
Amesema kwa asilimia kubwa mgogoro huo juu ya nani achinje umeingiliwa na mambo ya kisiasa kwani hata baadhi ya wananchi wa maeneo hayo wamekuwa wakilalamika juu ya kutokea kwa vurugu hizo.
Amesema shughuli za kibiashara katika eneo hilo zimeshindwa kufanyika katika eneo hilo hivyo kufanya wananchi kupata adha hasa kwa nchi jirani ya Zambia ambao kwa asilimia kubwa wanategema kupata mahitaji kutoka mpakani mwa Tanzania.
Hata hivyo Diwani amesema kuwa katika vurugu hizo askari mmoja  pamoja na mwananchi wamejeruhiwa kwa kupigwa mawe ambapo tayari wamekwisha fikishwa kituo cha polisi.
Kufuati hali hiyo Kamanda huyo wa Polisi amesema kwa sasa hali imelejea katika hali yake ya kawaida hivyo amewataka wananchi wa maeneo hayo kuwa watulivu wakati jeshi hiulo la Polisi likiendela na msako wa kuwatafuta wahalifu wengine.

Picha na Jem

...........................................................................................................

 

Jaji Mstaafu Ernest Mwipopo Amefariki Dunia


1 6210b
JAJI MSTAAFU ERNEST MWIPOPO AMEFARIKI DUNIA JANA ALASIRI KWA AJALI YA GARI MKOANI MOROGORO:
TAARIFA ZAIDI TUTAZIWEKA HUMU KADRI TUKAVYOZIPOKEA
................................................................................................................................
 

MWANAMKE ABAMBWA AKIMUUZA MTOTO WA KUMZAA KWA SHILINGI 100,000/=
Mwanamke mmoja mkazi wa kitongoji cha Seif katika kijiji cha Chiwezi-Mpemba TABU MWASHITETE  anashikiriwa na polisi wilayani Momba kwa tuhuma za kuumuuza mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka mitano kwa shilingi 100,000/=.
Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 12 jioni baada ya majadiliano ya biashara hiyo yaliyodumu kwa saa 7 baina ya muuzaji na mnunuzi.
Akizungumzia mchezo ulivyokuwa mpaka kumkamata mtuhumiwa, Bwana John Sinyinza ambaye alishakuwa mtumishi wa umma na kustaafu anaeleza kuwa alifuatwa na Bi Tabu majira ya saa tano asubuhi  nyumbani kwake.
Anaeleza kuwa katika mazungumzo  na mama huyo alishitushwa alipoambiwa kuwa anamuuza mtoto ambaye amemtoa Malawi na kwamba lengo la kumuuza anataka kupata fedha kwaajili ya kugharimia kumtoa baba yake mzazi wa mtoto huyo ambaye amefungwa nchini Malawi.
Hata hivyo katika majadiliano ya biashara hiyo, mwanamke huyo alitaka kulipwa kiasi cha shilingi 1,000,000/=(Milioni Moja) ambapo walikubaliana kuwa wangeuziana majira ya saa 12 jioni baada ya kupatikana kwa fedha hizo.
Ndipo bwana Sinyinza kutokana na tukio hilo kutokuwa la kawaida aliwasiliana na vyombo vya usalama na kupewa askari wa kike wa upelelezi ili waongozane eneo la tukio ambapo katika mtego wa kufanyika biashara hiyo, mwanamke huyo alifika akiwa na mwanaye ambaye alikuwa uchi ili wakabidhiane.
Bwana Sinyenga katika kuhakikisha kuwa mwanamke huyo hashtukii mchezo alimtambulisha askari huyo kama binti yake na kwamba walikubaliana kulipata fedha hizo kwa awamu ambapo angemlipa shilingi 100,000/= kwanza na kesho yake angemaliziwa kiasi cha shilingi 900,000/= zilizobakia.
Kufuatia makubaliano hayo mwanamke huyo alimkabidhi mtoto wake kwa mnunuzi na baadaye  kuagana kwa makubaliano kuwa angepewa kiasi kilichobakia na binti huyo wa upelelezi kesho yake.
Baada ya mteja  kutoweka na “bidhaa ya mtoto” ndipo  askari wa upelelezi huyo alipomweka chini ya ulinzi bi mkubwa huyo  na baadaye kufikishwa kituo ch polisi  cha Tunduma ambako katika mahojiano imebainika kuwa mtoto huyo ni  mwanaye ambaye baba yake alishafariki.
Alisema kuwa kutokana na ugumu wa maisha aliamua kumuuza mtoto wake huyo ili apate fedha kwaajili ya shughuli za kiuchumi kama mtaji na kwamba anatambua kuwa wanunuzi wangeweza kumuua mtoto huyo ama kwa matumizi mengine!
Kulingana na fununu za jeshi la polisi mwanamke huyo atafikishwa mahakamani leo jumatano katika mahakama ya wilaya ya Mbozi
na DANNY TWEVE
MBOZI
.................................................................................................................................

Kamati Kuu Chadema Kukutana Dar

Published in Siasa
8 e3b83
                                TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa siku mbili kwenye kikao chake cha kawaida jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 3-4 Aprili, 2013.
Katika kikao hicho cha siku mbili, Kamati Kuu itajadili pamoja na mambo mengine, yatokanayo na kikao kilichopita, hali ya kisiasa nchini, pia itapokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika mwezi Februari mwaka huu, ikiwemo mpango wa uendeshaji chama kwa kanda.
Aidha, Kamati Kuu pia itajadili mpango kazi na bajeti ya Chama kwa mwaka 2013-2014
Imetolewa Aprili 2, 2013, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA
..............................................................................................................................

ATCL KUANZA SAFARI ZAKE HIVI KARIBUNI KATIKA MKOA WA MBEYA

NDEGE YA SHIRIKA LA NDEGE ATCL IKITUA KWA MARA YA KWANZA KATIKA KIWANJA CHA KIMATAIFA CHA NDEGE SONGWE KUASHIRIA KUA WAKATI WOWOTE WANAANZA SAFARI YA KUJA MBEYA
BAADHI YA ABIRIA WAKISHUKA KATIKA NDEGE HIYO AKIWAMO MWIMBAJI MAARUFU WA NYIMBO ZA INJIRI  ROSE MHANDO 


KAIMU MKURUGENZI MWENDESHAJI WA SHIRIKA LA NDEGE ATCL NA PIA NI RUBANI WA NDEGE HIYO ILIYOTUA MBEYA HIVI KARIBUNI RICHARD SHAIDI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI MARA TU BAADA YA KUTUKA KATIKA UWANJA WA NDEGE SONGWE AMESEMA HIVI KARIBUNI SHIRIKA LAO LITAANZA SAFARI ZA KUJA MBEYA NA MIKOA MINGINE YA JIRANI HIVYO WAKAZI WA MBEYA NA MIKOA JIRANI MKAE MKAO WA SAFARI NA SHIRIKA LENU LA NDEGE YA TANZANIA


MUONEKANO WA NDANI YA NDEGE



SEHEMU YA RUBANI WA NDEGE

..................................................................................................................................

TTCL YAZINDUA HUDUMA YA ‘BANDO NA TTCL’ NA KAMPENI YA PUNGUZO KUBWA LA BEI YA INTANETI

Peter Ngota Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko akionyesha moja ya simu zinazouzwa na kampuni hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika jengo la makao makuu ya kampuni ya TTCL mtaa wa Samora wakati kampuni hiyo ilipozindua rasmi huduma za Bando na TTCL na Basti  leo jijini Dar es salaam kulia ni Kisamba Tambwe Mkuu wa Mauzo Kampuni ya TTCL. IMG_6852 
Peter Ngota Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko akionyesha kampeni ya Bando na TTCL mara baada ya kuizindua rasmi kushoto anayepiga makofi ni Ernesti Isaya Mkuu wa Maendeleo ya Bidhaa TTCL. IMG_6856 
Peter Ngota Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko akionyesha kampeni ya BASTI ambayo ina viwango vipya vya muda wa kuperuzi kwenye mtandao wa kampuni hiyo.
…………………………………………………………………………
TTCL, imezindua huduma  mpya ya Bando Na TTCL inayoambatana na punguzo
kubwa la bei kwa huduma ya INTERNET. Mtakumbuka ni Juzi tu tareha 21 Machi 2013
tulifungua kituo chetu kipya cha huduma  kwa wateja kilichopo  Kariakoo katika mkoa
wa Dar es Salaam katika kupanua mtandao wa huduma kwa wateja  nchini (>30 CSC
network nchini).
Kifuatacho sasa ni kupanua wigo wa huduma kwa wateja.
Vilevile mtakumbuka kuwa baada ya kujitambulisha sokoni na huduma ya ‘Mobile Internet’
isiyo na kikomo ya BANJUKA; kampuni ya simu ya TTCL sasa inazindua huduma mpya
inayojulikana kama ‘BANDO NA TTCL’. Huduma hii inamuwezesha mteja kufaidika na meseji
za bila kikomo, kuperuzi intaneti na muda wa maongezi kwenda mitandao yote kwa wakati
mmoja kwa bei hadi ya shilingi 500. BANDO NA TTCL inawalenga zaidi watumiaji wa simu za
kisasa za smart phones za TTCL (zinazopatikana ktk vituo vya huduma kwa wateja
nchini). Maelezo zaidi ya juu ya huduma hii yanapatikana kwa kupiga 100 huduma kwa wateja
au tembelea ofisi zetu za mauzo zilizoenea nchi nzima.
Aidha, TTCL imeshusha kwa kiwango kikubwa bei ya vifurushi vyake vya mobile internet kwa
kampeni ya BASTI ikimaanisha peruzi intaneti zaidi kwa gharama nafuu. Hili ni punguzo la bei
la aina yake. Mathalani; kifurushi cha mwezi cha 4GB kilichokuwa kinauzwa shilingi 90,000
sasa kinauzwa kwa shilingi 25,000 tu. Hii ni nafasi si tu kwa wateja waliopo wa TTCL kuongeza
matumizi kwa gharama nafuu bali hata kwa wateja wapya ikiwamo watumiaji wadogo kujiunga
na mtandao wa TTCL. (Haki ya mawasiliano kwa wote)
Leo hii, wateja wengi zaidi na hasa wanafunzi na wajasiliamali wanatumia simu za kisasa (smart
phones, tablet PCs kama iPad, Samsung Galaxy nk) na kompyuta ili kupata huduma za intaneti
na mitandao ya kijamii kwa mfano, Michuzi blog, facebook twitter, LinkedIn n.k ) kwa shughuli
zao za kila siku. Upatikanaji wa vifaa hivi vya kisasa (sambamba na ukuaji wa teknolojia) na
kumewezesha kukua kwa kasi kwa tabaka la kati lawatumiaji hivyo kumesababisha kukua
maradufu kwa soko la intaneti hapa nchini. (Hili nijambo jema sana kwa nchi yetu na maendeleo
ya watu wake kiuchumi na kijamii)
Kwa kuzingatia haya (na kutambua kuwa mawasiliano na habari ni swala mtambuka), TTCL ina
mikakati wa kuwawezesha wananchi wengi zaidi kupata huduma za intaneti na mawasiliano &
habari kwa ujumla na hivyo kuwa chachu kubwa ya maendeleo nchini. Huduma mpya ya
BANDO NA TTCL na kampeni ya BASTI ni juhudi za makusudi za TTCL katika kutimiza
adhma hii.

No comments: