Sunday, April 14, 2013

WANANCHI WA WILAYANI RUNGWE KUPITIA UMOJA WA MBIKI WAMSHUKURU MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA KWA KUUMALIZA VIZURI MGOGORO WA MAJI ULIO DUMU KWA MUDA BILA YA KUTATULIWA HADI KUFIKIA WANANCHI KUISHITAKI MAHAKAMANI MAMLAKA YA MAJI KWA KUPANDISHA GHARAMA ZA MAJI KUTOKA TSH 2000/= HADI TSH 4500/= BILA YA KUWASHIRIKISHA WANANCHI.

HALI YA HEWA YA MJINI TUKUYU KWA WIKI HII NI MVUA, BARIDI UKIAMBATANA NA UKUNGU
PAMOJA NA MVUA NA BARIDI BADO MAISHA YANASONGA MBELE CHA KUZINGATIA HAPA NI KUVAA KOTI NA MWAMVURI MKONONI
WATU WA TUKUYU MAHINDI YA KUCHOMA
MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA KULIA AKIWA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WAKISIKILIZA KELO ZA WANANCHI WA RUNGWE



 
 

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKIONGEA NA WANANCHI WALIO HUDHURIA MKUTANO WA ULIOANDALIWA NA WANANCHI KUPITIA UMOJA WAO WA MBIKI WALIOKUWA WAWAKILISHI KWA KUTETEA KUPANDA KWA GHARAMA ZA MAJI WILAYANI RUNGWE KUTOKA TSH 2000/= HADI 4500/= HUKU ONGEZEKO LA USOMAJI MITA LIKIWA LINAONGEZA MACHUNGU KWA WANANCHI WA RUNGWE 

 WANANCHI WA WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA KWA MALA YA KWANZA WAMEUNGANA KUMSHUKURU MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA KWA KUSIMAMIA NA KUUMALIZA MGOGORO WA MAJI ULIO DUMU KWA MUDA WILAYANI HAPO BILA KUFANYIWA UFUMBUZU WA KINA

AKIONGEA KWA NIABA YA WANANCHI WA RUNGWE MWENYEKITI WA UMOJA HUO WATSON PAMESA AMESEMA KUWA KILA MKUU WA WILAYA ANAYE KUJA KUFANYA KAZI RUNGWE ANA KITABU CHAKE LAKINI HUYU MEELA NI KIJANA MWELEVU ANAJUA KUONGOZA WANANCHI WAKE BILA YA KUINGIZA UTENDAJI NA SIASA

LAKINI WAMEMTAKA KUSIMAMIA MISINGI YA HAKI KATIKA KUWAONGOZA WANANCHI WA RUNGWE KWAKUWA PAMOJA NA MATATIZO YALIYOPO WANA IMANI SASA YATAKWISHA AU KUPUNGUA KWAKUWA TANGU AFIKE AMEONYESHA USHIRIKIANO MKUBWA SANA WA KUTATUA MIGOGOORO MIKUBWA ILIYOKUWA SUGU WILAYANI RUNGWE KAMA USIMAMIAJI NA UTARATIBU WA KUKUSANYA USHURU KATIKA SOKO LA KIWIRA, USHURU WA ZAO LA VIAZI KWA WAKULIMA, MIGOMO YA MADELEVA ZAIDI KUHAMASISHA SHUGHURI ZA MAENDELEO WILAYANI RUNGWE HUKU AKIWA MUWAZI KATIKA UTENDAJI WAKE WA KAZI WA KILA SIKU

NAYE MKUU WA WILAYA YA RUNGWE AKIONGEA NA WANANCHI AMEWATAKA WANANCHI WA RUNGWE KUPENDA KUKAA MEZANI ILI KUYAMALIZA MATATIZO YANAYOJITOKEZA MAANA HAKUNA ATAKAYE WATATULIA ZAIDI YA KUKAA NA KUONA NI JINSI GANI MAMBO YA MSINGI YANATATULIWA 




 .................................................................................................................................................................................................................

LEO NILIKUWA KIJIJI CHA LUFUMBI WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA KUJIONEA MAISHA YA WANAVIJIJINI NA CHANGAMOTO ZAO MAKALA HII ITAWAJIA HIVI KARIBUNI TUJIONEE UTAJIRI WA RUNGWE KWA ARDHI YENYE RUTUBA NA KILA ZAO UPANDALO LINASTAWI LAKINI WANANCHI WAKE MASIKINI NIMEZUNGUKA KWA MGUU YAPATA MASAA 9 




 ......................................................................................................................................

WANANCHI  wa Busokelo Wilayani Rungwe wameaswa kutunza vyanzo vya maji pamoja na mazingira ikiwa ni pamoja na kutoa ushirikiano kwa asasi zisizokuwa za kiserikali zinazohamasisha suala la maji.

Afisa wa Maji wa bonde la Ziwa Nyasa, Wilgal  Mkondola, aliyesimama wakati wa warsha iliyowajumuisha wenyeviti wa vijiji vyote vya halmashauri ya Busokelo Wilaya ya Rungwe,
Mtendaji Mkuu wa Elimisha, Festo Sikagonamo, alisema kuwa lengo la kuwashirikisha wenyeviti wa vijiji vyote vya Halmashauri hiyo ya Busokelo, ni kutaka kuwakutanisha na wataalum mbalimbali wa mazingira ili kujadili  na kuweza kuangalia namna ya kutunza  na kuhifadhi vyanzo hivyo vya maji na sambamba na kuangalia vyanzo vya kuharibika kwa vyanzo vingine vilivyopo kwenye maeneo husika.



WANANCHI Wilayani Rungwe wameaswa kutunza vyanzo vya maji pamoja na mazingira ikiwa ni pamoja na kutoa ushirikiano kwa asasi zisizokuwa za kiserikali zinazohamasisha suala la maji.
Mamlaka ya maji ya bonde la Ziwa Nyasa, imesema kuwa itaenedelea kushirikiana na asasi zisizokuwa za Kiserikali, kuhakikisha  inatoa elimu kwa wananchi  na wadau wa maji ilikutambua umuhimu wa kutunza vyanzo vyote vya maji vinavyotililisha katika ziwa hilo.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa wa Maji wa bonde hilo la Ziwa Nyasa, Wilgal  Mkondola, wakati wa warsha iliyowajumuisha wenyeviti wa vijiji vyote vya halmashauri ya Busokelo Wilaya ya Rungwe, iliyoandaliwa na asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya Elimisha ya Jijini Mbeya huku ikiwa na lengo la kujadili na kutambua vyanzo vyote vya maji vilivyopo ndani ya halmashauri hiyo na chgangamoto zake.
Alisema kuwa ili kukabiliana na janga la kupungua kwa maji katika vyanzo mbalimbali vya maji Serikali inatambua umuhimu wa kushirikiana na  asasi za kiraia kwa kuelimisha jamii juu ya utunzaji wa vyanzo hivyo.
Alisema kuwa kilio kikubwa  duniani kote ni kupungua kwa maji baridi kutokana  na uharibifu  wa mazingira ambao kwa nman moja ama nyingine unatokana na shughili za kibinadamu hivyo Serikali kwa kushirikiana na asasi za kiraia zainawajibu wa kuelimisha wananchi ili kujiokoa na janga linaloonekana kujitokeza.
“Nia ya Serikali ni  kushirikiana na asasi zisizokuwa za  kiraia  ili kufikia malengo yanayokusudiwa kwa jamii nzima, na hivi sasa  duniani kote kuna kilio kikubwa cha uharibifu wa mazingira wa kupungua na kutoweka kwa maji  katika vyanzo hivyo ndio maana asasi hii imeliona suala hili la utunzaji vyanzo vyetu vya maji na kuandaa warsha hii,’’alisema Mkondola.
Mtendaji Mkuu wa Elimisha, Festo Sikagonamo, alisema kuwa lengo la kuwashirikisha wenyeviti wa vijiji vyote vya Halmashauri hiyo ya Busokelo, ni kutaka kuwakutanisha na wataalum mbalimbali wa mazingira ili kujadili  na kuweza kuangalia namna ya kutunza  na kuhifadhi vyanzo hivyo vya maji na sambamba na kuangalia vyanzo vya kuharibika kwa vyanzo vingine vilivyopo kwenye maeneo husika.
“Lengo la kuandaa warsha hii ni kutaka kuwakutanisha wenyeviti wa Vijiji pamoja na wataalam wa maji kutoka bonde la Ziwa Nyasa  ili kujadili vyanzo vyote vya maji vilivyopo ndani ya halmashauri ya Busokelo na kuangalia namna ya kuendelea kuhifadhi pia kuangalia sababu za kuharibika kwa baadhi ya vyanzo hivyo sambamba ili jamii ipewe elimu ya kuvijenga na kuvitunza vyanzo hivyo,” alisema Sikagonamo.
................................................................................................................................

Zaidi ya shilingi milioni 50 zimetajwa kupotea katika shirika la umeme tanesco mkoani mbeya kwa kipindi cha miezi 3 kufuatia kuibuka kwa wimbi la wizi wa mafuta ya transifoma pamoja na wizi wa vifaa vingine .

  
Meneja wa shirika la Tanesco mkoa wa mbeya Mhandisi Simon Maganga akiongea na waandishi wa habari juu ya wizi wa umeme kwa wateja ambao sio waaminifu
Mafundi wa Tanesco wakimweleza meneja wao jinsi mteja alivyojiunganishia umeme wa wizi maeneo ya sae mbeya
Hivi ndiyo mwenye nyumba alivyojiunganishia umeme wa wizi katika nyumba yake
fundi wa Tanesco akikata umeme kwenye nguzo

Hii ndiyo gari inayotumika na mafundi wa Tanesco kupita nyumba hadi nyumba kukagua mita zao kama zimechezewa na kulitia hasara shirika hilo


Zaidi ya shilingi milioni 50 zimetajwa kupotea katika shirika la umeme tanesco mkoani mbeya kwa kipindi cha miezi 3 kufuatia kuibuka kwa wimbi la wizi wa mafuta ya transifoma pamoja na wizi wa vifaa vingine .
  
Meneja wa shirika hilo mkoa wa mbeya Mhandisi Simon Maganga amesema kuna tatizo kubwa la wizi wa transifoma na mafuta yake pamoja na vifaa vingine ambavyo thamani yake inakadiliwa kuwa zaidi ya shilingi milioni 50 vimeibiwa katika kipindi hicho .
Amesema suala la wizi limeibuka upya ambapo baadhi ya wananchi wasio kuwa waminifu wamekuwa wakifanya vitendo hivyo hasa kwa maeneo ya wilayani ambako ndiko wizi huo umekuwa ukifanyika marakwa mara.
Kufuatia hali hiyo tayari shirika  hilo limekwisha patiwa vifaa ambavyo vitaweza kuwasaidia katika msako huo wa kuwakamata wahalifu wanao lihujumu shirika hilo.
  
Moja ya vifaa vipya vilivyotolewa na serikali katika kukabiliana na tatizo hilo Mhandisi Maganga amesema kuwa ni pamoja na vyombo vya usafiri ambavyo teyari wamekwisha patiwa gari jipaya aina na Toyota Landcruse ambayo itawalahisishia kufika maeneo mengi zaidi .
  
Hata hivyo Meneja huyo amesema kuwa kutokana na msako waliokwisha kuanza wamefanikiwa kuwakamata baadhi ya wahalifu wanaolihujumu  shirika hilo na wanatalajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni.
  
Ametaja baadhi ya wilaya ambazo zimekuwa vinara wa wizi huo amabyo ni pamoja na Halimashauri ya wilaya ya Mbarali pamoja na Mbeya mjini ambapo Apri 12 mwaka huu walifanikiwa kumakata mkazi wa eneo la Sae Ndugu Saimon Chengula mara baada ya kujonganishi umeme kinyemela.
Kufuatia hali huyo ametoa wito kwa wananchi jijini humo na maeneo ya irani kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa viongozi wa shirika hilo kwa wale ambao wamekuwa wakilihujumu shirika hilo ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu.
.............................................................................................................................
 
 

Tanzania tujifunze hili kuwa Watoto, ''wanadhulumiwa sehemu za vita''


222 9f465
 Shirika la kuwahudumia watoto la Save the Children, linasema kuwa watoto ndio waathiriwa wakubwa wa ubakaji na dhulma zengeine za kingono katika maeneo ya vita duniani.
Ripoti ya shirika hilo inazingatia data waliokusanya pamoja na ushahidi kutoka katika nchi nyingi ikiwemo Colombia, Liberia na Jamuhuri ya kidemorasia ya Congo.
linasema kuwa mipango mingi au miradi ya kusitisha dhulma hizo na kusaidia watoto huwa hazipati ufadhili wa kutosha
Swala hilo litajadiliwa na mawaziri wa mambo ya nje wa kundi la G8 au la nchi zilizostawi kiviwanda.
333 a828c
Uingereza ilisema kuwa itatoa kipaombele kwa swala la dhulma za kingono katika maeneo ya vita wakati wa uongozi wake wa G8 mwaka huu.
Ripoti hiyo ya Save the Children, yenye kauli mbiu, Dhulma za kinyama dhidi ya watoto, inasema kuwa takwimu kutoka katika nchi kadhaa, zilizoathirika kutokana na vita katika miaka kumi iliyopita, zinaonyesha kuwa watoto ndio hudhulumiwa zaidi kingono katika maeneo ya vita na hata baadaye.
:CHANZO BBC SWAHILI
.................................................................................................................................

No comments: