Sunday, April 7, 2013

Nchemba amlipua Waziri Kagasheki

 

Nchemba Amlipua Kagasheki
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba amempiga kombora Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Hamis Kagasheki na Serikali kuhusu ardhi ya Loliondo. Serikali imemwisha kutangaza kuchukua kilomita za mraba 1,500 za ardhi ya Tarafa ya Sale na Loliondo kwa ajili ya eneo maalumu la uhifadhi na uwindaji unaoratibiwa, wakati ardhi hiyo ni mali ya vijiji.
Kutokana na kuibuka kwa mgogoro kati ya Serikali, madiwani, wananchi na wazee wa mila CCM iliunda Tume ya Nchemba kuzungumza na kusikiliza maoni ya wananchi.

Tume hiyo ilifanya mkutano na wananchi Kijiji cha Olorien Magaiduru, Tarafa ya Loliondo juzi,ikiwahusisha pia Mbunge wa Simanjiro Christopher ole Sendeka na Mbunge wa Longido, Michael Laizer.

Katika mkutano huo Nchemba alisema CCM inatambua wazi maslahi ya wananchi ndiyo maslahi ya taifa na kamwe hakuna maslahi ya taifa ambayo si maslahi ya wananchi.

Nchemba aliwataka wananchi, wazee wa mila na madiwani kutoogopa matamshi ya Waziri Kagasheki badala yake Chama kinaangalia uzito wa tatizo.

“Nitapeleka taarifa ya Kamati ya siasa, viongozi wa vijiji, mila na itakayotoka hapa. Wiki ijayo timu niliyokuja nayo na viongozi wenu tutakwenda kumuona Katibu Mkuu ili tumuone Waziri Mkuu,”alisema Nchemba.

Naye Sendeka alisema: “Nimepata fursa ya kujua jinsi wananchi wa Loliondo walivyojipanga, kutoka kijiji cha Piyaya, Arash mpaka Ololosokwani.

“Mashariki ni makazi, Magharibi Hifadhi ya Serengeti na mifugo ya kuchunga inayoelekea mwelekeo mmoja. Hili halikuwa la bahati mbaya ni matumizi bora ya ardhi.”

Alisema mwaka 2009 Bunge lilipitisha Sheria namba 5 ya Uhifadhi, katika sheria hiyo Bunge lilifuta maeneo ya uhifadhi na uwindaji unaotaratibiwa kote nchini.

....................................................................................................................................

WAZIRI MKUU MH. MIZENGO PINDA AWATAKA WATANZANIA KUPENDANA NAKUDUMISHA AMANI

IMG_1117
Waziri  Mkuu Mizengo Pinda amewataka wa Tanzania wapendane na kuishi kama watoto wa baba mmoja na kuondoa tofauti za kidini ambazo zina weza kuliingiza taifa katika matatizo makubwa waziri Mkuu ametoleamfano wa hivi karibuni ambao badhi ya wakristo na waisilamu walianza kugombana kwa ajili ya uhalali wa kuchinja nyama , amesema watanzania hawana budi kuheshimu imani za wenzao kwani miaka ya nyuma watu walikuwa wakishirikiana kiasi kwamba huwezi kujua tofauti ya mkristo na mwisilamu kwa vile watu walikuwa wanapendana nakuheshimu dini ya mwenzao , Hivyo amewaomba viongozi wa dini kusaidia kurudisha upendo ambao  ulikuwepo amesema amefurahishwa na kuona hata viongozi wa dini ya kisilamu Kuwepo kanisani katika ibada ya kubariki ndoa ya Bwana Philip Mangula na Bibi Yolanda Kabelege amesema watu wanjombe ndio mfano wa kuigwa
Waziri mkuu ameyasema hayo alipokuwa amehudhuria sherehe ya kubariki ndoa ya Makamu mwenyekiti wa CCM Bara Mh. Philip Mangula na Mwalimu Yolanda Kabelege ambayo imefanyika katika kanisa la Kilutheri Mkoani Njombe
Naye Katibu mkuu wa CCM Mh. Abdurahamani Kinana aliwapongeaza wana ndoa hao kwa kuamua jambo la kufunga ndoa kwani hata vitabu vitakatifu vinasema nyumba iliyo katika ndoa hata mungu huibariki nakuipa amani
Hapa Mzee Philip Mangula pamoja na mkewe Yolanda wakila kiapo mbele ya Askofu IMG_1145 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana wakipiga picha pamoja na Maharusi baada ya kubariki ndoa yao. IMG_1155 
Bwana Harusi Mzee Philip Mangula akimshukuru Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda mara baada ya kumaliza kutoa nasaha zake katika ndoa hiyo takatifu.

.....................................................................................................................................

WASANII MBEYA WAZINDUKA WAANZISHA SHIRIKISHO LA WACHEZA FILAMU MKOA WA MBEYA

MWENYEKITI WA MUDA WA SHIRIKISHO LA WAIGIZAJI MKOA WA MBEYA SAMWEL MWAMBOMA AKIZUNGUMZA AZMA YA KUWAKUTANISHA WAIGIZAJI WA MKOA WA MBEYA KATIKA KIWANJA CHA CITY PUB MBEYA
KATIBU WA MUDA WA SHIRIKISHO LA WAIGIZAJI WA MKOA WA MBEYA SADY MWANG'ONDA AKIZUNGUMZIA MIKAKATI YA WASANII KUJIKWAMUA KATIKA KAZI ZAO ZA SANAA YA UIGIZAJI MKOA WA MBEYA
BAADHI YA WASANII WA SANAA YA UIGIZAJI MKOA WA MBEYA WAKIWA KATIKA MKUTANO ULIOWAKUTANISHA WAIGIZAJI KATIKA UWANJA WA CITY PUB JIJINI MBEYA
BAADHI YA WAIGIZAJI WA MKOA WA MBEYA WAKIWA WAMESIMAMA DAKIKA MOJA KWA AJILI YA KUMKUMBUKA MSANII MWENZAO STEVEN KANUMBA ANAYETIMIZA MWAKA MMOJA TANGU AFARIKI DUNIA APRIL 7 MWAKA JANA
BAADHI YA WASANII WALIPATA MUDA WA KUWAULIZA MASWALI VIONGOZI WAO WA MUDA NA KUCHANGIA MADA MBALI MBALI KATIKA MKUTANO HUO
BAADHI YA VIONGO ZI WA WAKIHOJIWA NA WAANDISHI WA HABARI


WASANII wa Filamu Mkoani Mbeya wameaswa kufanya kazi kwa ushirikiano na kwa kuaminiana ili kuifanya kazi zao kujulikana kitaifa na kupata masoko mengi ikiwa ni pamoja na kujiongezea kipato.
Mwito huo ulitolewa na Mwenyekiti wa Muda wa Shirikisho la Filamu Mkoa wa Mbeya, Samwel Mwamboma ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha kusambazia Filamu cha Sam Video Centre cha Jijini Mbeya
Mwamboma alisema Mkoa wa Mbeya unawasanii wengi sana na wazuri tofauti na Dar Es Salaam lakini wameshindwa kujulikana kutokana na kukosa ushirikiano na uaminifu unaosababishwa na ubinafsi ndiyo unaosababisha kutofanikiwa  wala kujulikana kwa wasanii licha ya kushiriki katika Filamu nyingi.
“ Wasanii mkiwaamini watayarishaji wa Filamu, Wasambazaji, Waongozaji, Wapiga Picha na Waandaaji kazi zetu zitafika mbali sana lakini mkiwa wabinafsi hatutaendelea kabisa” Aliosema Mwenyekiti huyo.
Aliongeza kuwa Lengo la Kuanzisha Shirikisho la wacheza Filamu Mkoa wa Mbeya ni kuleta Umoja ili kazi za Wasanii wa Mkoa wa Mbeya zijulikane na kupendwa na watazamaji ili Wasanii wakubwa kutoka Dar Es Salaamu watamani kufanya kazi nao na siyo Wasanii wa Mbeya kutamani kuigiza na Wasanii wakubwa.
Kwa Upande Katibu wa Muda wa Shirikisho hilo Sadi Mwang’onda alisema kuwa moja ya vitu vinavyosababisha kazi za wasanii wa Mkoa wa Mbeya kuonekana kutokuwa na ubora ni kutokana na kila mtu kufanya kazi kivyake bila ushirikiano ambapo Watayarishaji, Wasambazaji, Wapiga picha na wadau kutokuwa na umoja.
Aliongeza kuwa Wasanii wa Mkoa wa Mbeya wanakutana na Changamoto nyingi ambazo ni ukosefu wa Mitaji  hivyo kuwaomba Wakazi wa Mkoa wa Mbeya wenye mitaji kuwekeza katika Soko la Filamu ambapo aliongeza kuwa kama wasanii wako tayari kuhakikisha Mwekezaji ananufaika na hajutii kuwekeza kwenye Filamu za Wasanii wa Mkoa wa Mbeya.
Aliitaja Changamoto Nyingine kuwa ni kukosekana kwa Elimu miongoni mwa Wasanii ambapo wengi wao wamekosa elimu ya kawaida ya darasani ili  hali wengine kutokuwa na ufahamu juu ya kitu wanachokifanyia maigizo, kutokana na hilo Katibu huyo amewakikishia Wasanii kuwa baada ya Shirikisho hilo kutulia atawatafutia Semina na Mafunzo ili wapate mwanga kuhusu Filamu.
Katibu huyo alizitaja changamoto zingine kuwa ni pamoja na Wasanii kutofanya utafiti kuhusu kile anachotaka kukiigiza jambo ambalo linasababisha kazi nyingi kuonekana kama zinafanana,ukosefu wa matangazo na wasanii wenyewe kutojiamini kutokana na kazi wanazozifanya hivyo kuonekana ni wababaishaji tu.
Mbali na hayo Mwang’onda aliwasihi Wasanii waliojitokeza katika Mkutano huo uliohudhuriwa na Wasanii zaidi ya 50 kutoka Ndani ya Jiji la Mbeya, Wadau wa Filamu pamoja na Wanahabari kuwa Wasanii wanatakiwa kuishi maisha ya Heshima kama wanavyoigiza kutokana na Jamii kuiamini sana kazi za sanaa.
Aidha Katibu huyo alisema ili Shirikisho lao liweze kuimarika na kuendelea watakuwa wakifanya mikutano ya mara kwa mara na kuwataka Wasanii hao kufanya kazi kwa ushirikiano na kukutana kila wanapopata nafasi na sio kubaguana.
................................................................................................................................... 

JK Apanda Pantoni kwenda na kurudi Kigamboni..

b1 1a7a7
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiongea na watoto waliokutana nao kwenye pantoni ya MV Magogoni walipokuwa  wakitoka Mji Mwema, Kigamboni, jijini Dar es salaam leo April 7, 2013  walikomtembelea Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi
 kig2 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakishuka kutoka  kwenye pantoni ya MV Magogoni walipokuwa  wakitoka Mji Mwema, Kigamboni, jijini Dar es salaam leo April 7, 2013 walikomtembelea Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
PICHA NA IKULU
................................................................................................................................

Serikali iache kutoa uraia kama njugu

 
 Kwa ufupi
Tatizo hapa ni kwamba suala la kutoa uraia limepewa usiri mkubwa. Ndiyo maana kwa makusudi taarifa inayotolewa na Serikali kuhusu watu hao inakuwa nusunusu ili kuwachanganya wananchi wenye pingamizi wasijue pa kuanzia.
Kama kuna suala nyeti kwa taifa ambalo Serikali bado inalifanyia mzaha, basi suala hilo ni namna uraia unavyotolewa kiholela kwa wageni pasipo kuwapo mfumo stahiki wa kusimamia mchakato huo. Kwa muda mrefu sasa, Serikali imekuwa ikiliona suala hilo la uraia kama jambo jepesi tofauti na nchi nyingi duniani ambazo huliona kama msingi wa usalama na kitovu cha maendeleo ya nchi hizo.
Hapa tunajaribu kuonyesha jinsi sera ya Serikali kuhusu uraia na uhamiaji inavyoendelea kututesa, ingawa inawezekana kabisa kwamba lipo kundi la watu linaloweza kuwa limefaidika na kuneemeka kutokana na udhaifu wa sera hiyo inayotoa mianya tele kwa vitendo vya rushwa na ufisadi. Hoja hapa ni kwamba Serikali inaendelea kutoa uraia kwa wahamiaji wengi wasiokuwa na sifa za kupata uraia wa Tanzania.

Wiki iliyopita, Serikali kama kawaida yake ilitoa tangazo tunaloweza kuliita la kisanii katika baadhi ya magazeti kuhusu watu walioomba uraia wa Tanzania. Pamoja na tangazo hilo kuficha mambo mengi muhimu kuhusu watu hao, linamtaka Mtanzania yeyote anayepinga watu hao kupewa uraia amwandikie Waziri wa Mambo ya Ndani na kutoa sababu kwa nini wasipewe uraia.
Hiki ni nini kama siyo kichekesho cha mwaka? Inawezekanaje tangazo lisilokuwa na kichwa wala miguu, kwa maana ya kuwa na taarifa muhimu za waombaji wa uraia lililotoka mara moja tu, tena katika gazeti moja au mawili liwawezeshe Watanzania wengi kuwafahamu watu hao na kuitaarifu Serikali? Je, watawezaje kuwasiliana na Serikali wakati tangazo hilo halionyeshi anuani au simu ya waziri au wizara husika? Serikali kweli ina dhamira ya kuwahusisha wananchi katika mchakato huo wa kuwapa au kutowapa uraia watu hao?
Tatizo hapa ni kwamba suala la kutoa uraia limepewa usiri mkubwa. Ndiyo maana kwa makusudi taarifa inayotolewa na Serikali kuhusu watu hao inakuwa nusunusu ili kuwachanganya wananchi wenye pingamizi wasijue pa kuanzia. Na ndiyo maana hata baada ya zoezi hilo Serikali haitoi taarifa kwa umma kuhusu waliopata na walionyimwa uraia.

Zoezi la kutoa uraia hufanywa kwa tahadhari kubwa katka nchi nyingi duniani. Kwanza, mwombaji lazima atume maombi akiwa nchini mwake. Hapa tunashuhudia watu wakiingia nchini ovyo na baadaye kuomba uraia.
Pili, kuna vigezo vinavyoangaliwa, ikiwa ni pamoja na umuhimu wa elimu na taaluma yake kwa nchi anayoomba uraia; au umri na uwezo wake wa kiuchumi wa kumwezesha kujitegemea; au sababu za kibinadamu kama kukimbia vita, mateso, na kadhalika.
Uzoefu umeonyesha kwamba nchi yetu inatoa uraia kwa watu wazima na tegemezi ambao hawawezi kuwa na manufaa yoyote kwa nchi yetu. Tunatoa uraia kwa watu wanaogeuka wachuuzi na kupigana vikumbo mitaani na vijana wetu wasio na ajira. Hii inatokana na baadhi ya ndugu zao ambao tayari wana uraia wa Tanzania (ambao waliupata kinamna?) kutoa rushwa na kuwawezesha kupewa uraia.
Ndiyo maana Tanzania imekuwa kama nchi isiyo na mwenyewe ambayo inajulikana kwa jina la mitaani kama Shamba la Bibi. Tumegundua gesi na hivi punde tutagundua mafuta.
Uraia sasa utazidi kutolewa kama njugu, kwani wageni watamiminika ili kufaidi nishati hizo. Tusipokuwa makini tutaiuza nchi yetu.

........................................................................................................................................................

No comments: