Saturday, April 6, 2013

Waziri wa Nishati na Madini Tanzania Profesa Muhongo kutembelewa na Waziri wa chuma wa nchini India Mr. Dileep Raj Singh Chaudhary

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisaini mkataba wa uchimbaji madini wa kampuni ya MorogoroRegional Mining Company Ltd wanaotarajia kuanza shughuri hizo mwishoni mwaka 2013 kulia kwake ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo ndugu, Protase R.G. Ishengoma.
Waziri wa Nishati na Madini akiwa katika picha ya pamoja na wawekezaji katika sekta ya madini baada ya kusaini mkataba wao ili waweze kuanza shughuri za uchimbaji. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo akifuatiwa na Kamishna wa Madini ndugu
 
Fursa za uwekezaji zinazidi kutolewa kwa kiasi kikubwa nchini ikiaminika kuwa uwekezaji ndio utakao tufanya tutoke katika nchi zinazoendelea na kuwa nchi za uchumi wa kati. Hayo yameonekana baada ya Waziri wa Nishati na Madini kutembelewa na Waziri wa chuma wa nchini India Mr. Dileep Raj Singh Chaudhary aliyefika kutafuta nafasi za uwekezaji kwa kampuni za india zinazoweza kuwekeza katika sekta za nishati na madini na kuokelewa kwa moyo na wenyeji wake.

Profesa Muhongo ameahidi kuwa na ushirikiano mzuri na nchi hiyo na kwamba wataoneshwa ramani zenye maeneo muhimu kwa ajili ya shughuri za uwekezaji katika sekta za madini na  nishati. 

Pia amesisitiza kuwa ushirikiano baina ya nchi hizo haujaanza leo kwani toka kipindi cha uhuru wahindi walitumika sana katika shughuri za maendeleo ikiwa ni pamoja na kufundisha. 

Muhongo amesema, pamoja na uwekezaji huo, ni lazima serikali ya Tanzania iwe na hisa kwenye makampuni yatakayofika ili kuwekeza nchini ili rasilimali za nchi ziwe za manufaa kwa taifa na wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wake Waziri wa Chuma India Bw. Dileep Raj Singh Chaudhary amefurahishwa na mapokezi mazuri na kwamba kwa upande wao wako tayari kuwekeza katika madini ya makaa ya mawe, manganese, gold, diamond na chuma. 

Pamoja na hayo imeelezwa kwamba katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini ndugu, Eliakim Maswi watasani makubaliano ya kushirikiana kiutendaji na Katibu Mkuu wa India.

.............................................................................................................

MAHAFARI YA PILI YA DIPROMA YA UUGUZI CHUO CHA UUGUZI NTC TUKUYU WAHITIMU 56 WAFANIKIWA KUMALIZA MAFUNZO YAO TAYARI KUWAHUDUMIA WATANZANIA


SHEREHE ILIANZA KWA MAANDAMANO YALIYOANZIA TUKUYU MJINI HADI CHUO CHA NTC TUKUYU KILICHOPO MAKANDANA


SHEREHE ILIANZA KWA MKUU WA CHUO NOLASCA MTEGA KUWAKARIBISHA WAGENI WAALIKWA
ADISON EMMANUEL AKISOMA RISALA KWA NIABA YA WAHITIMU WA DIPROMA YA UUGUZI

MR MANGA KUSHOTO AKIONGOZA KIAPO CHA UKUNGA KWA WAHITIMU

WASHA TAA YA UPENDO
KIAPO KWA WAKUNGA
SHARIF HAMIS (WA KWANZA KITAARUMA DARASANI)
ROSEMARY ARROKO (NIDHAMU BORA KATI YA WAHITIMU)

NEEMA SADDI ( WATATU KITAARUMA DARASANI)

PICHA YA PAMOJA NA MGENI RASM PAMOJA NA WAKUFUNZI WA CHUO CHA WAUGUZI TUKUYU  NA WAPILI KWA MBELE UPANDE WA KUSHOTO NI PILLI KIMATA AMBAYE NI MRATIBU WA MAFUNZO YA UUGUZI TANZANIA
WAHITIMU WAKAKABIDHIWA VYETI

MZAZI AKIMPONGEZA BINTI YAKE ESTER HAULE KWA KUHITIMU DIPROMA YA UUGUZI
PAULINA BROWN AKIFURAHI NA DADA YAKE BAADA YA KUHITIM DIPROMA YA UUGUZI
FAMILIA YA MAREHEMU MCHUNGAJI MWAIKENDA WAKIFURAHIA PICHA YA PAMOJA NA KIJANA WAO LUGANO MWAIKENDA ALIYESHIKA CHETI
...................................................................................................................................................................

ANDIKENI HABARI ZA UCHUNGUZI ZAIDI ACHANENI NA HABARI ZA SEMINA NA MIKUTANO- MWOLEKA

dsc_2199 
Na Gladness Mushi wa Fullshangwe-Arusha
 WAANDISHI wa habari hapa Nchini wameaswa kuhakikisha kuwa wanajiwekea utatibu wa kuandika zaidi habari za uchunguzi kuliko kurtegemea habari za semina na mikutano kwani habari za mikutano na semina bado hazitoi majawabu na changamoto kwa jamii

 Endapo kama waandishi wa habari wa Tanzania wataweza kujiwekea utaribu wa kuandika habari ambazo zina uchunguzi wa kutosha basi watakuwa ni chanzo kikubwa sana cha maendeleo ya Nchi
 Hayo yalielezwa Jana na Anjelo Mwoleka ambaye ni Mkurugenzi wa Jambo  Arusha Publisher wakati  akiongea na wahitimu wa fani ya uandishi wa habari katika chuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC) katika maafali ya sita ya chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo.

 Aidha Mwoleka alisema kuwa kwa sasa kuna wimbi kubwa la waandishi wa habari a wanajihusisha zaidi na masuala ya habari za Semina na kuachana na habari za kiuchunguzi hali ambayo wakati mwingine ina nyima haki za msingi za jamii kwa kuwa waandishi wa habari wana nafasi kubwa sana ya kuibua maovu yanaoendelea kwenye Jamii

 Alifafanua kuwa habari za uchunguzi ndani ya Nchi ya Tanzania ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi hivyo basi wana habari hawapswi kukimbia na badala yake wanapswa kuzipa kipaumbele kikubwa ili kuweza kuruhusu changamoto kwenye sekta zote kujilikana

 “kuwa mwandishi wa habari sio lazima uwe unajua ratiba za mikutano za kila siku bali kuna maana kuwa unapaswa kujua na kutambua kuwa unatakiwa lkuwa mchunguzi na hapo ndio kazi yako itakuwa na manufaa makubwa sana kwa jamii hivyo basi habari za muhimu zinatakiwa kupewa kipaumbele tena kikubwa sana ili nchi ya Tanzania iweze kufika mahali ambapo inatakiwa kufika kama zilivyo nchi nyingine ambazo zimeendelea duniani”aliongeza Mwoleka

 Awali wahitimu wa mafunzo hayo ya uandishi wa habari katika ngazi ya cheti, na shahada walisema kuwa pamoja na kuwa chuo hicho kimewalea katika maadili mazuri lakini bado wanakabiliwa na uhaba wa vifaa kama vile Kompyuta, na Kamera kwa ajili ya mazoezi.
................................................................................................................................................................

No comments: