Friday, May 3, 2013

MAHAFARI YA WALIMU NGAZI YA CHETI YAFANA CHUO CHA UALIMU MPUGUSO TUKUYU MBEYA WAHITIMU NGAZI YA CHETI 544 WAHITIMU


MKUU WA CHUO CHA MPUGUSO KULIA KATIKATI MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA NA ANAYE FUATA NI MWENYEKITI WA BODI YA CHUO MPUGUSO       MZEE MKISI

WADAU WA ELIMU NA WAPILI KUTOKA KUSHOTO MBELE NI MKUU WA CHUO CHA UALIMU TUKUYU MATHIAS MVULA

BAADHI YA WANACHUO WALIOHITIMU CHUO CHA UALIMU MPUGUSO TUKUYU

MKUU WA CHUO CHA UALIMU MPUGUSO DOROTHY MHAIKI AKIONGEA NA WANACHUO PAMOJA NA WAZAZI WALIOHUDHURIA MAHAFARI HAYA HUKU AKIWATAKA WANACHUO KUWA  MABAROZI WAKUTENDA MEMA KUFANYIA KAZI ELIMU WALIO IPATA HAPA CHUONI WAKAKITENDEE KATIKA JAMII NA HASA KUINUA ELIMU YA TANZANIA

MWENYEKITI WA BODI YA CHUO MZEE MKISI AKIONGEA NA WANACHUO NA WAZAZI HUKU AKIWATAKIA KILA LA HERI WAHITIMU KWENDA KWENYE JAMII NA KUWAHUDUMIA WATOTO KAMA WALIVYOFUNDISHWA CHUONI HAPO KUZINGATIA MAADIRI NA UPENDO KWA WATOTO

AFISA UHUSIANO WA LULU MENGELE AKIONGEA NA JUMUIYA YA WAFANYAKAZI WAZAZI NA WANACHUO KATIKA MAHAFARI YA CHUO CHA UALIMU MPUGUSO TUKUYU NA KUONGEA MAMBO MENGI NA FAIDA ZINAZOPATIKANA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA PPF

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKIONGEA NA WANACHUO NA WAZAZI HUKU AKIWATAKA WALIMU WALIO MALIZA KUKUBARI KUFUNDISHA VIJIJINI MAANA WALIMU WALIOWENGI WAKIPANGIWA VIJIJINI HUWA WANAACHA KAZI HIVYO AMEWATAKA WAHITIMU KUWA WAZALENDO NA KUONGEZA UADIRIFU KWA KUTOA ELIMU BORA KWA WATOTO WA KITANZANIA ILI ELIMU ISONGE MBELE KWA MANUFAA YA TAIFA

 ............................................................................................................
HAPA LEO NINA SAFARI YA KWENDA DSM HADI MOSHI KCMC  SAFARI INAANZA MCHANA HUU TUOMBEANE WADAU WA KINGOTANZANIA
BAADA YA RATIBA YA MOSHI TAREHE 6-8 MWEZI HUU  NITAKUWA IRINGA NIMECHAGULIWA KUHUDHURIA SEMINA YA BARAZA LA BIASHARA TAIFA LITAKALO FANYIKA IRINGA KWA NCHI ZA AFRIKA HIVYO NIKIWA MMOJA WA WATU WATAKAO HUDHURIA MIJADARA MBALIMBALI NITAWALETEA MAADA ILI WADAU TUJADILI KWA PAMOJA NA NIPATE MAONI YENU NIKAELEZE NINI MBELE YA MKUTANO HUO MKUBWA WA AFRIKA
.................................................................................................................................................................

GFC- TANZANIA YAPENYA NUSU FAINALI PAN-AFRICAN GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE

02
  GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™
MSIMU WA TATU
ROBO FAINALI – EP7 winners & hype EP 8
*STOP PRESS* *STOP PRESS* *STOP PRESS* *STOP PRESS* *STOP PRESS* *STOP PRESS*
*WATANZANIA NA WAKENYA WAINGIA NUSU FAINALI*
Mai mosi, Dar es Salaam; Jana usiku timu kutoka Kenya na Tanzania ziliwakilisha vizuzi  Afrika mashariki katika sehemu ya saba ya GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™. Timu ya Kenya ilifanikiwa kuzishinda timu nyingine na kufikia hatua ya mwisho ya ukuta wa pesa wa Guinness. Kenneth kamau na Wills Ogutu wote kutoka Nairobi wamefuzu nusu fainali pamoja na watanzania Daniel Msekwa na Mwalimu Akida Hamad ambao walipata nafasi ya pili jana usiku.
Timu hizi mbili kutoka Kenya na Tanzania sasa zina nafasi ya kuwakilisha Afrika mashariki na kushinda hadi dola za kimarekani 250,000 pamoja na kuvikwa taji la ushindi wa Pan-African, watakapoendelea hatua z juu zaidi. Timu hizi zitahitaji kujiandaa vizuri zaidi na kujiamini ili kufanya vizuri katika hatua ya nusu fainali.
Timu zingine nne zitakutana katika robo fainali ijayo ili kuwania nafasi ya kuingia nusu fainali ya mashindano ya GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE.
Usikose kuangalia robo fainali za Pan-African kupitia televisheni za ITV na Clouds TV ambapo timu za Africa Mashariki zinapokutana na timu na timu zingine kutoka Afrika Magharibi huku ukiburudika na kinywaji cha GUINNESS.
Hakikisha kuufwatilia ukurasa wa facebook wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kwa habari mbalimbali.
-www.facebook.com/guinnesstanzania
GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni kipindi cha mchezo wa soka kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya Endemol.  Usikose kuangalia na kufuatialia kipindi hiki katika runinga yako kupitia televisheni za ITV na Clouds TV kila siku ya Jumatano usiku.
Tafadhali kunywa kistaarabu – Hairuhusiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18.
....................................................................................................................................................

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO KWA WAKUU, WAMILIKI WA SHULE NA VYUO

JK-PIc

Na Gervas Mwatebela, Dar es salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wakuu na wamiliki wa shule na vyuo binafsi kwa minajili  ya kuboresha sekta ya elimu haoa nchini.
Akizungumza  na viongozi wa TAMONGSCO Rais Kikwete amesema sekta binafsi ina mchango mkubwa wa kuinua elimu hapa nchini hivyo jitihada za pamoja zinahitajika katika kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza
Rais Kikwete aliwataka wamiliki na wakuu wa shule na vyuo binafsi kupunguza ada  kubwa wanazotoza kwa wanafunzi ili watanzania wengi hasa wa kipato cha chini waweze kupata fursa ya elimu.
Aidha Mheshimiwa Rais alisema serikali iko katika Mchakato wa kutunga Sera Mpya ya Elimu baada ya ile ya mwaka 1995, umefikia katika hatua za mwisho na kinachosubiriwa sasa ni maoni ya Wabunge ili Sera hiyo ikamilishwe na kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu.
Wakati huo huo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania itaanza maandalizi ya kupitia upya mitaala ya elimu nchini ili nayo ilingane na malengo ya Sera Mpya ya Elimu,mahitaji ya maendeleo nchini na duniani kwa ujumla.
Licha ya changamoto zinazoikabili sekta ya elimu serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu imeongeza sekta hiyo ambapo kuna wanafunzi zaidi ya milioni nane katika shule  za msingi,zaidi wanafunzi milioni moja na laki nane  kwa shule za sekondari na zaidi ya laki moja na sitini elfu kwa upande wa vyuo vikuu.

WAKATU HUOHUO
1
Na Gervas Mwatebela, Dar es salaam
Wadau wa elimu wametakiwa kutoa ushirikiano wa dhati kwa taasisi za sekta hiyo kwa minajili ya kuboresha hali ya elimu hapa nchini.
 Mwenyekiti wa mfuko wa kijamii wa walimu  TGTF  bwana Ephraim Mwikuka alisema mazingira ya sasa ya elimu yana changamoto kubwa kwa upande wa waalimu na wanafunzi hivyo kuhitaji nguvu za pamoja kuzitatua.
 Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa TGTF imejipanga kushirikiana na serikali na jamii katika kuboresha mazingira ya elimu ya  msingi na sekondari hapa nchini.
 Bwana Mwikuka amewataka watanzania kuacha kulalamika bali wachukue hatua  katika kukabiliana na taasisi,jumuiya na serikali kwa ujumla kutatua changamoto za kielimu katika jamii.
Aidha Mwikuka aliongeza kuwa elimu ni msingi wa taifa lolote hivyo ni lazima wadau kwa kushirikaiana na watanzania kuonesha juhudi za makusudi kuendeleza elimu na si kuibua lawama zisizokuwa na msingi wowote.
 ..........................................................................................................................................................

KIPANYA LEO

NewDocument d63a5


 

No comments: