Tuesday, May 28, 2013

NBC wamkaribisha Mkurugenzi Mtendaji mpya

nbc 80ab3
Uongozi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) umemkaribisha rasmi Mkurugenzi Mtendaji wao mpya, Mama Mizinga Melu. Mama Melu alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered Zambia, ambapo aliongoza benki hiyo kwa Miaka 6 kabla kuhamia NBC.
Mizinga si mgeni kwenye sekta ya kibenki, kwani keshashika nafasi kubwa  mbali mbali akiwa na Benki ya Standard Chartered. Nafasi hizi ni kama vile Mkuu wa Kimataifa wa Mashirika ya Maendeleo, Uingereza ambapo alikuwa anasimamia maendeleo ya mikakati na utekelezaji, pamoja na kuwa Mkuu wa Taasisi za Fedha nchini Kenya na Afrika Kusini, Kanda ya Afrika.
Mama Melu si mgeni kwa Tanzania, kwani alishawahi kuwa Mkuu wa Hazina katika Benki ya Standard Chartered Tanzania kati ya mwaka 2000 na 2003. Kabla ya kushika nafasi hiyo alifanya kazi kama kaimu Mkuu wa Hazina Benki ya Standard Chartered Uganda mwaka 1998 na Zambia mwaka 1999.

Mizinga ana Shahada ya Pili (Masters) ya usimamizi wa Biashara (MBA) kutoka Chuo cha Henley Management College (Uingereza) na ni mwanachama wa Taasisi ya wafanyakazi wa mabenki(ACIB), pamoja na sifa nyengine mbali mbali.
Akizungumzia juu ya uteuzi huo, Mwenyekiti wa  Bodi ya Wakurugenzi ya NBCi, Dk Mussa Assad alisema, “kuwasili Mizinga ni jambo la furaha sana kwetu kwani amekuja wakati muafaka ambapo NBC inapitia mabadiliko mengi mazuri na tunafuraha kuwa atakuwa sehemu ya mabadiliko haya”.

Pia aliongeza” Kabla ya kuwasili kwake, benki ilikuwa ikiongozwa na Pius Tibazarwa ambaye ameonyesha uongozi mzuri kwa kipindi hiki na kutimiza matarajio yetu yote, na tungependa kumshukuru kwa juhudi zake kwani ametekeleza majukumu ya ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, juu ya jukumu la kuendesha idara yake mwenyewe.”
 Mama Melu amepokea nafasi hiyo kutoka kwa Pius Tibazarwa ambaye alishikilia nafasi hiyo kama Kaimu Mkurugenzi Mtendaji tangu mwanzo wa mwaka huu.
Mizinga amepangiwa kukutana na viongozi wa serikali pamoja na wateja wakubwa kwa ajili kutambulishwa rasmi kabla kuanza safari za kutembelea matawi ya NBC yaliopo mikoani ili kukutana na wafanyakazi na wateja walioko huko.

.................................................................................................................................

Lema amvaa Lowassa kwa helikopta Monduli

 
Na Mussa Juma, Mwananchi  
  • Lowassa ndiye aliyepewa mikoba na CCM ya kumnadi mgombea wa chama hicho na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wabunge wa chama hicho Mei 19, mwaka huu Mjini Dodoma alisema kiongozi huyo anatosha kukipa ushindi katika kata hiyo.
  •  
  • Monduli. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema jana aliongoza kampeni za Chadema za udiwani katika Kata ya Makuyuni, Wilaya ya Monduli kwa staili ya aina yake, akitumia helikopta huku ikidondosha vipeperushi vya mgombea wa chama hicho, Japhet Sironga.
    Akizungumza katika kampeni hizo, Lema alisema: “Chama chetu kina uhakika wa ushindi kwani Sironga ambaye ni mwalimu wa Shule ya Sekondari Ilboru, ana uwezo mkubwa kwa kuwa ni msomi.
    Lowassa ndiye aliyepewa mikoba na CCM ya kumnadi mgombea wa chama hicho na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wabunge wa chama hicho Mei 19, mwaka huu Mjini Dodoma alisema kiongozi huyo anatosha kukipa ushindi katika kata hiyo.
     
    Lema alisema: “Makuyuni, hamna maji, hamna huduma za afya, hakuna barabara za vijiji, wafugaji ardhi yenu inaporwa sasa ukombozi wenu umefika kama mkimchagua msomi Sironga.”
    Alimkabidhi mgombea huyo taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kumtaka kazi yake ya kwanza iwe kuibua ufisadi na kumfikishia bungeni ili kuiokoa Halmashauri ya Monduli.
    Akizungumza katika kampeni hizo, Sironga alisema ameamua kuingia katika kinyang’anyiro hicho, ili kuokoa jamii ya Makuyuni na Monduli kutokana na shida zinazowakabili.
    ADC Kigamboni
    Chama cha ADC kimezindua kampeni ya nyumba kwa nyumba ya uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Mianzini, Kigamboni, Dar es Salaam.
    Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Kigamboni, Mwenyekiti wa ADC Wilaya ya Temeke, Salum Sudi alisema kata hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi  ikiwamo kero ya maji, barabara, elimu ya msingi na soko, hivyo wakipewa ridhaa hiyo kero hizo zitakwisha...
    Nyongeza na Pamela Chilongola.

 .....................................................................................................................................

AFISA Elimu Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda amewaagiza Wakuu wa Shule za Sekondari, Waratibu Elimu Kata na Maafisa Michezo kuhakikisha hawajumuishi wanafunzi wa kidato cha nne katika kushiriki mashindano ya Umiseta.

AFISA Elimu Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda amewaagiza Wakuu wa Shule za Sekondari, Waratibu Elimu Kata na Maafisa Michezo  kuhakikisha hawajumuishi wanafunzi wa kidato cha nne katika kushiriki mashindano ya Umiseta.
Afisa michezo mkoani hapa George Mbijima akitangaza matokea ya mashindano hayo






AFISA Elimu Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda amewaagiza Wakuu wa Shule za Sekondari, Waratibu Elimu Kata na Maafisa Michezo  kuhakikisha hawajumuishi wanafunzi wa kidato cha nne katika kushiriki mashindano ya Umiseta.
Alisema mashindano yatakayofanyika Mwakani yasiwahusishe wanafunzi wa kidato cha Nne kutokana na kuwa ni darasa la mitihani ya Taifa hivyo kuwafanya kukosa maandalizi ya kutosha pindi wanapokuwa wamechaguliwa kushiriki michezo hiyo ambayo hufanyika katika kituo kimoja ambacho ni mbali na shule zao.
Maagizo hayo aliyatoa mwishoni mwa wiki wakati akifunga Mashindano ya Umiseta kwa ngazi ya Mkoa yaliyofanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Iyunga Jijini Mbeya, mashindano yaliyohusisha wachezaji kutoka Kombaini ya timu za Wilaya zote za Mkoa wa Mbeya.
Kaponda alisema mashindano hayo ambayo hufanyika kuanzia ngazi ya Shule, Kata, Wilaya, Mkoa, Kanda hadi Taifa huwanyima fursa ya kusoma wale ambao watabahatika kufuzu ngazi zote hizo hadi mashindano ya Taifa.
Kutokana na hali hiyo zaidi ya Wachezaji 40 wa michuano hiyo waliochaguliwa kuunda timu ya Mkoa ni wanafunzi wa Kidato cha Nne ambapo walitakiwa kukaa kambini kwa ajili ya kujiaandaa na mashindano katika ngazi ya Kanda yatakayofanyika Hivi karibuni Mkoani Mbeya.
Aidha katika kilele hicho timu ya Kombaini ya Jiji la Mbeya ilifanikiwa kuchukua Kombe  la Mpira wa Miguu baada ya kufanikiwa kutinga Fainali kwa kucheza na Timu ya Kombaini ya Wilaya ya Mbozi na kushinda kwa jumla ya magoli 3 kwa moja.
Katika michuano hiyo timu hizo zilicheza kwa kukamiana ambapo katika dakika ya 14 ya Mchezo huo Jiji ilifanikiwa kupata goli la kuongoza lililofungwa na Christopher Edson, ambapo timu ya Mbozi ilisawazisha goli hilo dakika ya 22 kipindi hicho hicho na kufanya timu kwenda mapumziko zikiwa sare ya kufungana 1-1.
  
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Christopher Mwaipopo aliifungia timu ya Jiji goli la pili kwa Mkwaju wa Penati kufuatia kufanyiwa madhambi na mabeki wa timu ya Mbozi na Mwamuzi kuamuru Mkwaju upigwe uliozaa goli katika dakika ya 72.
  
Dakika ya 90  Mbeya Jiji  ilifanikiwa kupata goli la tatu na la ushindi kutoka kwa mchezaji wake Ipyana Muyavilwa kwa mkwaju wa Penati pia kutokana na kuangushwa katika eneo la hatari wakati mabeki wa timu ya Mbozi wakijaribu kuokoa.
Zaidi ya michezo sita ilishindaniwa na kutolewa makombe kwa washindi, zawadi ambazo zilizotolewa kwa ufadhili wa kampuni ya vinywaji ya Pepsi kwa michezo ya Mpira wa Miguu kwa Wanaume na Wanawake, Mpira wa Pete, Basketi Wanaume na wanawake, Voleyball wanaume na wanawake, Handball Wanaume na Wanawake pamoja na mpira wa meza na riadha.
Aidha Afisa Elimu wa Mkoa wa Mbeya Juma Kaponda baada ya kumaliza kukabidhi makombe kwa washindi pia aliwaambia washindi kuwa makombe waliopewa ni vyao moja kwa moja hayatashindaniwa tena bali Mwakani yataandaliwa mengine.
Picha na Mbeya yetu

No comments: