Saturday, May 25, 2013

MBEYA PRESS CLUB YAPATA UONGOZI MPYA BAADA YA KUTIMULIWA UANACHAMA ALIYEKUWA MWENYEKITI MR CHRISTOPHA NYANYEMBE NA PENDO FUNDISHA KWA TUHUMA YA KUFUJA PESA ZA WANACHAMA MBEYA PRESS CLUB

MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA WALIOKAA WANNE KUTOKA KULIA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA
MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA  AKIONGEA NA WAANDISHI WA MKOA WA MBEYA HASA MAMBO YAHUSUYO KULIJENGA TAIFA MOJA LA TANZANIA KUWA NA AMANI NA MSHIKAMANO NA KUPINGA MATUKIO YA KIFISADI KWA KUWA MWANDISHI WA HABARI NI KIOO KATIKA JAMII NA MTU ANAYEAMINIWA SANA NA WATU HIVYO HAIPASWI KUWA CHANZO CHA UCHAFU KATIKA UTENDAJI WA KAZI NA UCHOCHEZI NA VURUGU ZINAZO SABABISHA  KUTOWEKA KWA AMANI TANZANIA
KULIA MWAKILILI NA MWAKIPESILE WAKIWA MAKINI KUMSIKILIZA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE

JOSEPH MWAISANGO MMILIKI WA MBEYA YETU NA WAJUMBE WENGINE WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA
FRED  & HYNES
KWENYE KUNDI LOLOTE LAZIMA PAWE NA WASHAURI HAPO NI BENJAMINI MWAKILILI AKISISITIZA JAMBO LA KUFUFUA MSHIKAMANO KATI YA WAANDISHI NA WANANDISHI WA NCHI JIRANI KAMA ILIVYOKUWA KIPINDI CHA NYUMA
HAPA ULIKUWA NI WAKATI MZURI NA WA FURAHA BAADA YA CHARLES MWAKIPESILE KUWA NDIO MUASISI WA KUJITOLEA MCHANGO WA TSH LAKI MOJA NA KUOMBA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPN MEELA  KUMUUNGA MKONO KWA LAKI NNE ILI KUWA NDIO MWANZO WA KUANZISWA KWA SACCOS YA MBEYA PRESS CLUB HIVYO CHACHU HII IKAZAA MATUNDA ZAIDI YA MILIONI MBILI ZIKAPATIKANA KWA AJILI YA KUAZISHA SACCOS YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA

HAPA NI UMAKINI TU WAKUMSIKILIZA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI
MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKIONDOKA UKUMBINI HAPO AKISINDIKIZWA NA BAADHI YA WAANDISHI BAADA YA KUONGEA NA WAANDISHI WA MKOA WA MBEYA HASA MAMBO YAHUSUYO KULIJENGA TAIFA MOJA LA TANZANIA KUWA NA AMANI NA MSHIKAMANO NA KUPINGA MATUKIO YA KIFISADI KWA KUWA MWANDISHI WA HABARI NI KIOO KATIKA JAMII NA MTU ANAYEAMINIWA SANA NA WATU HIVYO HAIPASWI KUWA CHANZO CHA UCHAFU NA UCHOCHEZI WA KUTOWEKA KWA AMANI TANZANIA
KAMATI YA MUDA IKAKABIDHI TAARIFA KWA WAJUMBE NA KURUHUSU UCHAGUZI KUFANYIKA KAMA ILIVYOANDALIWA
UKAFIKA WAKATI ULIOSUBIRIWA NA WANACHAMA SIKU YA UCHAGUZI NA HAPO NI KAMATI YA UCHAGUZI ILIYOONGOZWA NA BENJAMINI MWAKILILI KATIKATI NA KUSHOTO MAKAM MWENYEKITI CHARLES MWAKIPESILE PIA KULIA NI KATIBU MR MOSSES
WAGOMBEA NAFASI YA UENYEKITI WAKAPATA NAFASI YA KUOMBA KURA KWA WAJUMBE WA UCHAGUZI
WWAGOMBEA WENGINE WAKATUMIA SIFA ZA KUWA NA PASPOTI KUWASHAWISHI WAPIGA KURA ILI WAWAPE KURA ZA NDIO
UKAFIKA WAKATI WA KUAMUA NANI AWE KIONGOZI KWA KUPIGA KURA KWA WAJUMBE WA MBEYA PRESS CLUB
KWA KUTUMIA KARATASI MAALUM KURA ZILIPIGWA KWA UMAKINI HAKUNA KUCHAKACHUANA HAPO
KWA MKOTO PIA KURA ZILIPIGWA
KURA ZIKAHESABIWA KWA UMAKINI WA KUTOSHA
MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI BENJAMINI MWAKILILI AKITANGAZA MATOKEO YA UCHAGUZI KUWA MWENYEKITI NI USWEGE LUHANGA, MAKAMU MWENYEKITI NI MODESTUS MUKULU NA KATIBU NI EMANUEL LENGWA, MTUNZA HAZINA BRANDINA NELSON, KAMATI YA MAFUNZO FESTO SIKAGONAMO,
UONGOZI MPYA UKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA HUKU VYOMBO VYA HABARI VIKIENDELEA NA KAZI YA KUCHUKUA TUKIO LA KIHISTORIA MKOANI MBEYA BAADA YA KUFUKUZWA UANACHAMA KWA ALIYEKUWA MWENYEKITI CHRISTOPH  NYANYEMBE NA MTUNZA HAZINA  UPENDO BAADA YA KUKUTWA NA TUHUMA YA KUCHAKACHUA PESA ZA CLUB
UONGOZI MPYA UKISHUKURU WAJUMBE KWA KUWAPA NAFASI YA KUONGOZA MBEYA PRESS CLUB
BAADA YA UCHAGUZI AMANI IMEPATIKANA NA MAKUBARIANO NI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADIRIFU ILI MBEYA NA TAIFA ZIMA ILIFAIDIKE NA TAARUMA HII YA HABARI
ALIYE SIMAMA NI CHRISTOPHA NYANYEMBE HAPO SIKU ALIPOKUWA KASHURUTISHWA KUJIUZULU UONGOZI BAADA YA KUTUHUMIWA KUHUJUMU MAPATO YA CLUB YA WAANDISHI WA HABARI MBEYA
KUSHOTO NI PENDO FUNDISHA ALIYEKUWA MTUNZA HAZINA WA MBPC

MWENYE TISHET YA PUNDAMILIA NI MR NYANYEMBE AKISHUHUDIA KURA ZA KUMUONDOA MADARAKANI BAADA YA KUTUHUMIWA KUFUJA PESA ZA WANACHAMA WA MBEYA PRESS CLUB

BAADA YA KAMATI YA MUDA KUPITIA TUHUMA MR NYANYEMBE NA PENDO FUNDISHA KUKUTWA NA HATIA ZA KUFUJA MALI ZA CLUB AZIMIO LA PAMOJA KWA WANACHAMA LIKATOKA NI KUFUTWA UANACHAMA WA MBEYA PRESS CLUB HIVYO WATU HAWA WAWILI SIO WANACHAMA WA MBPC ILA WATABAKI KUWA WAANDISHI NA WAWAKILISHI KATIKA VYOMBO VYAO
MKUU wa wilaya ya Rungwe Bw. Chripin Meela amesema, changamoto zinazokabili sekta ya habari na  vyombo vya habari  kwa ujumla ni matokeo ya umuhimu wa taaluma hiyo katika ukuaji wa demokrasia nchini
Akizungumza kwenye mkutano wa uchaguzi wa klabu ya wandishi wa habari mkoa  Mbeya Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela amesema, wananchi wana matumaini makubwa na vyombo vya habari na pale kipapota doa la utendaji ni muhimu kujirekebisha kabla ya kutengeza picha mbaya mbele ya jamii wanayoihudumia
Amesema hali iliyojitokeza hivi karibuni kwenye klabu hiyo inahitaji kuweka misingi imara ya kiutendaji  na kwamba jitihada za kufanya uchaguzi  wakati huu ni hatua muhimu za kuimarisha mfumo wa kujiwajibisha kama taasisi ya taaluma.
Amesema ikiwa viongozi wa dini na vyombo vya habari vitajihusisha na ubadhirifu na wizi ni dalili kuwa hakutakuwa na mwingine wa kukemea jamii itakayokuwa huru na yenye kukemea vita dhidi ya rushwa
Bwana Meela amesema inashangaza kuona hata vyombo vya habari vinaingia kwenye ufisadi na akaohoji  ninani atakayehoji ufisadi serikali na kwingineko kama nanyi mnaingia kwenye mitego hiyo hiyo?
Katika hatua nyingine amependekeza  Vyombo vya habari kujenga utamaduni wa kujihusisha na ufuatiliaji wa maendeleo vijijini na kwa kufanya hivyo kutawezesha wananchi kuwasilisha changamoto zinazowakabili kwa watunga sera.
Amesema katika kufikia hilo  ni vyema pia Viongozi wa serikali ngazi za chini kuondoa uoga  katika kufanya kazi na vyombo vya habrari na kwa kufanya hivyo kutasadia kusukuma mbele jitihada za maendeleo
Katika hatua nyingine Bwana Meela amechangia kiasi cha shilingi 400,000 kwaajili ya uanzishaji wa chama cha kuweka na kukopa cha wanahabari  SACCOS  ili kuwezesha kuwapa fulsa wana habari  kujisimamia kiuchumi  na kupunguza changamoto za kimaisha zinazowakabili
Katika kufanikisha hilo wanachama wa Mbeya Press club walijitokeza kuchangishana wenyewe ambapo wamefanikiwa kukusanya mtaji wa papo kwa papo kiasi cha shilingi 1,400,000/=
Aidha ameshauri klabu ya wandishi wa habari kuwa na ofisi yake na hvyo kwa kuomba kiwanja kwenye mamlaka za majiji itasaidia kuwapa nguvu katika kusimamia haki zao wakiwa na uhuru wa kuwekeza kwenye majengo yao.
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE WAISHI KWA AMANI NA UPENDO PASIPO UFISADI
.................................................................................................................................................................

HATIMAYE wasamaria wameanza kujitokeza katika kumsaidia mtoto Joshua Joseph ambaye alifungiwa ndani zaidi ya miaka miwili huku akikosa matunzo muhimu na kupelekea mtoto kupata ugonjwa wa utapia mlo.

Mwandishi wetu Joseph Mwaisango aliyembeba mtoto Joshua akiwa na ofisa maendeleo na ustawi wa jamii  Habiba Iblahimu
Mwandishi wetu Joseph Mwaisango akikabidhi msaada ya Magodoro, nguo na lishe kwa niaba ya familia ya Mama Masawe wa DSM ambayo iliguswa sana na hali aliyokuwanayo mtoto Joshua
Hakika mtoto Joshua sasa angalau siku mbili hizi hata kusimama na kutembea ameanza tunawashukuru wote mnaomsimamia mtoto huyu hapo ikuti Iyunga 
Mtoto Joshua akiangalia zawadi alizopatiwa
Mama mlezi wa Joshua akiwa haamini kabisa kwa msaada waliopatiwa kwa ajili ya Joshua
Yaani majirani wakibaki kuduwaa na kusema mungu awabariki kazi za mikono yao wote waliomchangia mtoto huyu na wasiishie hapo wawajali na watoto wengine Tanzania
 Balozi wa Mtaa wa Ikuti  Aron Mboya, aliwashukuru wasamaria hao na kwamba serikali ya kijiji itasimimia na kuhakikisha mtoto huyo anapata huduma zote za kiafya pamoja na kumsimamia mama mlezi kutumia misaada hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa kwa mtoto huyo.
Daktari wa kituo cha Afya, Inyala kilichopo Kata ya Iyunga, Queen Mwakijambile, amesema baada ya vipimo kufanyika mtoto huyo amekutwa na tatizo la utapiamlo huku uzito wa mwili ukiwa haulingani na umri wake.
Mama mlezi wa Joshua akiwa kituo cha afya
Mtoto Joshua siku ya kwanza tulipomkuta alikuwa hivi

HATIMAYE wasamaria wameanza kujitokeza katika kumsaidia mtoto Joshua Joseph ambaye alifungiwa ndani zaidi ya miaka miwili huku akikosa matunzo muhimu na kupelekea mtoto kupata ugonjwa wa utapia mlo.
Moja ya Wasamaria hao Familia ya mama Masawe toka DSM wametoa magodoro mawili, nguo,mashuka,chakula pamoja na lishe ya mtoto.
Akipokea msaada huo jana, ofisa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamiii, Habiba Ibrahimu  alisema wasamaria hao wameonyesha  uzalendo na kuokoa maisha ya mtoto ambayo kwa asilimia kubwa yalikuwa hatarini.
Aidha, Daktari wa kituo cha Afya, Inyala kilichopo Kata ya Iyunga, Queen Mwakijambile, alisema baada ya vipimo kufanyika mtoto huyo amekutwa na tatizo la utapiamlo huku uzito wa mwili ukiwa haulingani na umri wake.
“Baada ya mtoto Joshua kufikishwa kwenye kituo hiki cha matibabu na kufanyiwa vipimo, tumebaini mtoto alikosa lishe pamoja na uzito wake kufikia kilo nane ukilinganisha na umri wake wa miaka miwili,”alisema
Alisema, uzito wa kilo nane ulipaswa kuwa na mtoto wa miezi sita au saba hivyo hatua aliyofikia alikuwa kwenye hatari ya kupoteza uhai wake.
Naye Balozi wa Mtaa wa Ikuti  Aron Mboya, aliwashukuru wasamaria hao na kwamba serikali ya kijiji itasimimia na kuhakikisha mtoto huyo anapata huduma zote za kiafya pamoja na kumsimamia mama mlezi kutumia misaada hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa kwa mtoto huyo.
Picha na Mbeya yetu
................................................................................................... 

RAIS KIKWETE KATIKA MKUTANO WA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA AU JIJINI ADDIS ABABA LEO

Muono wa jicho la samaki katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013 
 au8 
Viongoi AU wakiwakumbuka waliotangulia mbele ya haki. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013au11 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013
PICHA NA IKULU
.........................................................................................................................

No comments: