Friday, May 24, 2013

WAFANYA BIASHARA WADOGOWADOGO WILAYANI RUNGWE KATIKA MJI WA TUKUYU (WAMACHINGA) WAFURAHIA UTARATIBU WA KUFANYA BIASHARA ENEO MOJA LA STAND YA MABASI BAADA YA UWANJA WA MPIRA WA MIGUU KUBADILISHWA MATUMIZI NA KUWA STAN NA PAKING YA MAGALI


BIASHARA IMEANZA KUCHANGANYA HUKU WAFANYA BIASHARA WANAOZUNGUKA NA MATUNDA NA MATUNDA  VICHWANI WAKIFURAHIA UTARATIBU WA KUKAA PAMOJA
KUELEKEA USHIRIKA , KATUMBA NA KIWIRA
USAFIRI WA KUELEKEA MASUKURU
MOJAWAPO WA USAFIRI WA KWENDA LWANGWA UKIONDOKA KWENDA SAFARI YA KWENDA LWANGWA
HII NDIO STANDI YA MABASI TU KWA SASA MABASI YATOKAYO MBEYA, KYELA NA DSM PIA ZITARUHUSIWA TAX TU KUINGIA HAPA

WENGINE WAKIENDELEA NA KUJENGA MEZA KWA AJILI YA BIASHARA
WENGINE WAKIENDELEA NA KAZI ZA KUTENGENEZA MEZA ZAO
UKIFIKA UWANJA WA MPIRA WA ZAMANI TUKUYU MJINI UTAPATA MAHITAJI YA AINA MBALIMBALI KUTOKANA NA WAFANYA BIASHARA WADOGOWADOGO KUFANYA BIASHARA SEHEM MOJA HUKU WAKISUBIRI SEHEMU WALIYOTENGEWA KUFANYIWA UKARABATI WA BARABARA

KWA SASA TUKUYU KUFANYA BIASHARA YA KUZUNGUKA NA VITU MWISHO

KULIA NI MKUU WA WILAYA CHRISPIN MEELA  AKIONGEA NA KINGO KUHUSIANA NA MIKAKATI YA SERIKALI YA KUWAJALI WAFANYA BIASHARA WADOGOWADOGO WILAYANI RUNGWE HASA KWA KUWATENGEA ENEO LAO LA KUDUMU ILI KUFANYA BIASHARA KWA UHURU PIA KUTAMBULIWA NA TAASISI ZA KIFEDHA KULIKO HIVI SASA WAMAMCHINGA KUZURULA NA BIDHAA NDOGO AMBAZO MWISHO WA SIKU MAENDELEO HUWA DUNI

  ..................................................................................................................

MTWARADSC 0112 e53fb


91 9a0e4
92 ffb33
97 22f25
98 a3201
mtwara2 87206
mtwara 6104f
PICHA NA FARID HEMED.

 ..............................................................................

Bajeti Miundombinu: Fedha za wafadhili kumaliza miradi ya Barabara?

Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli 
Na Victor Karega, Mwananchi  (
  • Katika mwaka wa fedha 2012/13, Tanzania ilipanga kupokea Sh397.051 bilioni kwa ajili ya miundombinu. Lakini hadi Machi 2013, Sh16.361 bilioni tu sawa na asilimia 4.1 zikiwa ni ahadi, zimetolewa.
Dar es Salaam. Zikiwa zimepita siku kumi tangu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lipitishe bajeti ya Wizara ya Ujenzi ya Sh1.3 trilioni katika mwaka wa fedha 2013/14, bado mpaka sasa kuna kigugumizi katika kuweka bayana ni kiasi gani cha fedha hizo kimetengwa kwa ajili ya kulipa mikopo ya zamani.
Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli anasema kati ya fedha hizo Sh845.226 bilioni sawa na asilimia 21.8, zimetengwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu. Sh397  bilioni ni fedha kutoka kwa wafadhili.
Pamoja na hayo yote, Kamati ya Bunge ya Miundombinu inasema ni lazima serikali ielezee ni kiasi gani cha fedha kitakwenda kwenye shughuli za maendeleo. Pia kubainisha serikali imetenga shilingi ngapi kwa ajili ya kulipa madeni.
“Kamati imetaarifiwa kwamba mpaka Machi 2013, wananchi na wakandarasi wanaidai Wizara Sh348.666 bilioni, kwa hiyo kamati inataka kupata uhakika kama fedha ambazo inataka ziidhinishwe, kweli zitatumika kufadhili miradi iliyolengwa au sehemu yake italipa mikopo ya zamani,” anahoji Mwenyekiti wa kamati, Profesa Juma Kapuya.
Fedha za wafadhili hazitabiriki
Anashauri kwamba serikali sasa inapaswa kugharimia maendeleo ya miundombinu nchini kwa kutumia vyanzo vya ndani vya mapato kwa kuwa fedha za wafadhili zimekuwa hazitabiriki.
Katika mwaka wa fedha 2012/13, Tanzania ilipanga kupokea Sh397.051 bilioni kwa ajili ya miundombinu. Lakini hadi Machi 2013, Sh16.361 bilioni tu sawa na asilimia 4.1 zikiwa ni ahadi, zimetolewa.
Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally anasema hawezi kuunga mkono bajeti ya Wizara wa Ujenzi kwa sababu ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ya kujenga barabara mpya haijatimizwa mpaka sasa. Ahadi hiyo aliitoa rais katika uchaguzi wa mwaka 2010.
Anafafanua kuwa kinyume na ahadi ya Rais, barabara ya Sumbawanga- Kanazi-Kibaoni, imejengwa kwa kiwango duni cha asilimia 24 baada ya mwaka jana barabara hizo kutengewa  Sh27 bilioni tu.
Lakini kama hiyo haitoshi Keissy  anafafanua kwamba makandarasi wa Kichina wanaojenga barabara hiyo wanaonekana wamechoka kifedha na sasa wanauza mchanga, kokoto, na mawe.
Akichangia hutuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Profesa David Mwakyusa (Rungwe Magharibi) anasema kwa masikitiko kwamba Wilaya ya Rungwe imegawanywa katika wilaya tatu, lakini kwa bahati mbaya, hakuna barabara ya kuunganisha wilaya hizo.
...................................................................................................................................................................

 

No comments: