Friday, August 23, 2013

Wachimbaji wadogo wa matundasi Wilayani Chunya mkoa wa Mbeya watakiwa kupewa fursa za uwezeshwaji katika shughuri zao za uchimbaji madini

Kamishna wa madini kitengo cha lesenwatano kutoka kulia akiwa katika ziara ya  kutembelea mradi wa uchimbaji madini wa Katundasi wilayani Chunya Mkoani Mbeya.

Kwa sasa kuna kila sababu kwa serikali kuhakikisha wachimbaji wadogo wanapata fursa ya mafunzo ya uchimbaji ili kuweza kuwainua katika tasnia ya uchimbaji wa madini nchini.

Wito huo umetolewa na  Kamishana Msaidizi Kitengo cha Leseni (Wizara ya Nihati na Madini), Mhandisi John Nayopa, katika Kituo cha mafunzo kwa vitendo ya uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu kwa wachimbaji wadogo, Matundasi, Wilayani Chunya Mkoa wa Mbeya ambaye alikua Wilayani humo kukagua na kujionea miradi mbalimbali ya uchimbaji madini wilayani humo.

Mhandisi John Nayopa amesisitiza kuwa kituo hicho kinahakikisha kina panua wigo wake kwa kujitangaza ili watu wenye uhitaji wa mafunzo kufikiwa na kwamba hilo ndilo lengo la Wizara ya Nishati na Madini na Serikali kwa ujumla.

Alisema kuwa kituo hicho kinatakiwa kutoa ushirikiano mzuri kwa serikali ili kuwepo na uratibu mzuri kati ya kampuni inayo simamia kituo hicho na Wizara ya Nishati na Madini ambao wote ndiyo wadau wakuu wa kituo hicho.

Naye Kamishana Masaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Magharibi Mhandisi John Shija ameutaka uongozi wa Kampuni hiyo kuhakikisha kituo kinafikia malengo yaliyowekwa na Wizara ya Nishati na Madini ili kuleta tija kwa wachimbaji wadogo.

Awali, akizungumza Mahandisi Paul Gongo Mkurugenzi Mtendaji  wa kampuni ya Matundasi ASM Limited inayo ratibu, kuendesha na kusimamia kituo hicho, alisema kituo hicho kilianzishwa mwaka 2005 na ilipofika mwaka 2008 kituo kili kabidhiwa rasmi kampuni hiyo ili kukiendesha.

Pia, Mhandisi Gongo alisema kazi zinazofanyika kwa sasa kituoni hapo ni kuanzisha mashapo ya uchimbaji madini ya dhahabu, kukusanya nguvu kazi ya rasilimali watu, kufanya marekebisho ya mitambo na kusimika mitambo wa uchenjuaji wa madini.
Alieleza kuwa mwitikio wa wachimbaji wadogo kupata mafunzo ni mzuri, na kwamba kuna vikundi vya wachimbaji wadogo vilianzishwa vikasaidiwa na kituo kupata mafunzo na vitendea kazi, alidai baadhi ya wachimbaji hao wanacho subiri ni maeneo yatakayo tengwa na Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo.

“tumejenga mtambo ambao tumekiwa  tukiwasagia mawe wachimbaji wadogo kwa gharama nafuu” alisema
Mhandisi ……………ameongeza kuwa pamoja na mafanikio yaliyopo kituo kinakabliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo upungufu wa vifaa vya kuendeshea shughuli za uchimbaji, gharama kubwa za umeme utokana na kutumia jenereta.

Kituo hicho kilianzishwa mwaka 2005 na Wizara ya Nishati na Madini kikiwa na  lengo la kuratibu, kuendesha na kusimamia mafunzo ya vitendo kwa wachimbaji wadogo. Ilipofika mwezi Januari 2009 kituo kilikabidhiwa kwa Kampuni ya Matundasi ASM Limited. Kampuni hiyo kwa sasa inajumla ya wafanyakazi 65 katika eneo la kituo na tayari katika shughuli zauchimbaji inazofanya inauwezo wa kuzalisha Gramu 500 za dhahabu kwa mwezi. Huko ikiuza dhahabu hiyo kwa wafanyabishara wa ndani ya nchi pekee.
 

Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN Ametoa vyeti kwa madereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda zaidi ya 151 wa Igurusi Wilaya ya Mbarali.

Madereva Bodaboda wakijipanga tayari kwa kwenda kupokea vyeti vyao
Madereva Bodaboda wakiandamana kuelekea kupokea vyeti vyao toka kwa kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya


Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN akiongea na madereva Bodaboda kabla ya kuwakabidhi vyeti vyao
Madereva  walikabidhiwa vyeti hivyo baada ya kupatiwa mafunzo ya alama za usalama barabarani kwa msaada wa shirika lisilo la Kiserikali kwa kushirikiana na Kikosi cha usalama Barabarani Mkoani Mbeya.


Picha ya pamoja



Kamanda wa wa Polisi Mkoani MBEYA DIWAN ATHUMAN Ametoa vyeti kwa madereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda zaidi ya 151 wa Igurusi Wilaya ya Mbarali.

Madereva hao walikabidhiwa vyeti hivyo baada ya kupatiwa mafunzo ya alama za usalama barabarani kwa msaada wa shirika lisilo la Kiserikali kwa kushirikiana na Kikosi cha usalama Barabarani Mkoani Mbeya.

Mbali ya kukabidhiwa vyeti pia Madereva hao walipatiwa leseni za udereva ambapo Diwani Athumani aliwataka madereva hao kuwa makini barabarani na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Aidha Kamanda Diwani aliwashukuru madereva wa Bodaboda kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi kwa kufichua vitendo vya uhalifu Mkoani Mbeya ambapo wamekuwa wakitoa taarifa za siri na kupunguza uhalifu mkoani Mbeya.

Hata hivyo Diwani alitumia fursa hiyo kuwataka madereva kuwa makini kwani kwa kipindi cha miezi sita madereva 38 wa bodaboda wamefariki mkoani Mbeya na kusikitishwa na wingi wa ajali hizo za pikipiki kwani wengi wao ni vijana na ni nguvu kazi ya Taifa. 

..........................

Mungu aliniamuru nijiuzulu, asema Papa Benedict XVI;

pope_37848.jpg
Rome, Italia. Miezi sita baada ya kujiuzulu, Papa Benedict XVI, amefungua mdomo na kueleza sababu za kufikia uamuzi huo wa kushangaza.
Jana, vyombo vya habari vilimkariri Papa Mstaafu Benedict akimweleza mgeni wake kuwa aliitwa na Mungu kwa miujiza.

Kiongozi huyo ambaye alishangaza watu kwa uamuzi huo wa Februari 8, mwaka huu, hata hivyo alisema sauti ya Mungu imejibu kupitia kwa mfuasi wake, Papa Francis.

Papa Benedict alitangaza uamuzi wa kujiuzulu Februari 11, maelezo yake yalielekeza katika afya yake.
Alisema nguvu zake zilikuwa zimepungua kiasi cha kutokuweza kumudu majukumu yake ipasavyo.
Alisema, "Mungu aliniambia 'niondoke,' nami nikatimiza wajibu huo bila kusita," alisema Papa Benedict ambaye amekuwa kiongozi wa kwanza kufikia uamuzi huo baada ya miaka 600 ya Kanisa Katoliki. Alisema tangu wakati huo ameishi maisha ya sala.

Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 86 alisema ameshuhudia maono ya Mungu kwa miezi kadhaa huku akisikia sauti na tamaa ya kuendelea kuwa karibu naye (Mungu).
Papa Benedict, hata hivyo alisema Mungu amembariki na kumwezesha kuuona utukufu wake kupitia kwa Papa Francis, akielewa kwa nini alitakiwa kuondoka mapema kwa kuitika sauti na utashi wa Mungu.
Shirika la Habari la Kikatoliki (Zenit), hata hivyo halikueleza ni nani aliyekuwa akizungumza na Papa Benedict.

Hata hivyo, kauli hiyo ya Papa Benedict imeungwa mkono na vyanzo vya kuaminika kutoka Vatican.
"Ni ripoti ya kuaminika, ina usahihi, inaeleza mchakato wa kiroho ambao Papa Benedict aliupitia kabla ya kujiuzulu, vyanzo hivyo vililiambia gazeti la The Times.
Wachunguzi wa mambo wamekuwa wakieleza kuwa Papa Benedict alikatishwa tamaa na kuvuja kwa siri za mawasiliano yake binafsi na msaidizi wake .
 .............................................................................

WATU MILIONI 2.9 KUCHUKULIWA ALAMA ZA VIDOLE NA PICHA

Bw. Thomas William Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na hifadhi hati wakati alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu idadi ya watu waliochukuliwa alama za vidole kushoto ni Georgina Misama afisa habari wa Idara ya Habari Maelezo. 2 
Meneja wa Uchambuzi wa mfumo wa kompyuta NIDA Bw. Mohamed Mashaka akitoa maelezo kwa waandishi wa habari jinsi mtambo huo unavyofanya kazi.
………………………………………………………………………………………
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeanza zoezi la uchukuaji alama za vidole, picha na saini za kielekroniki kwa waombaji wa Vitambulisho vya Taifa katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo watu wapatao milioni 2,900,000 wanatarajiwa kupatiwa huduma hiyo.
Zoezi hili lilianza Julai 15 katika wilaya ya Temeke ambayo imegawanywa katika kanda tano, itafuatiwa na Wilaya ya Ilala na kuhitimishwa na Kinondoni.
Kila Wilaya imegawanywa katika kanda, ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa vizuri na kurahisisha zoezi kwa kuwapunguzia wananchi usumbufu wa kukaa muda mrefu kusubiri katika foleni.
Zoezi la uchukuaji alama za vidole linakwenda sambamba na ujazaji fomu kwa waombaji wapya ambao hawakupa fursa ya kujaza fomu wakati wa zoezi la ujazaji fomu za maombi ya vitambulisho vya Taifa.
Waombaji wanatakiwa kufika kwenye vituo vya usajili na nyaraka halisi za kuthibitisha uraia na umri mathalan, cheti cha kuzaliwa, pasipoti, vyeti vya elimu ya msingi na sekondari, leseni ya udereva, kitambulisho cha bima ya afya na kitambulisho cha mpigakura.
Zoezi la Utambuzi na Usajili wa watu lina hatua mbalimbali ambazo zinatakiwa kufuatwa kwa lengo la kuweza kukusanya taarifa sahihi kwa lengo la kutumika na mifumo mingine. Hatua hizo ni kama ifuatavyo:-
    1. Ujazaji wa fomu za Utambuzi na Usajili;
    1. Uhakiki wa awali wa fomu za maombi;
    1. Uingizaji wa taarifa kwenye mfumo wa kompyuta;
    1. Kuthibitisha taarifa za mwombaji zilizo katika mfumo wa kompyuta;
    1. Uchukuaji wa alama za vidole, picha na saini ya kielektroniki;
    1. Utengenezaji wa Daftari Kuu la Taarifa za Watu;
    1. Uhakiki wa mwisho;
    1. Uchapishaji na Ugawaji wa Vitambulisho.
Mfumo huu una faida kubwa sana kwa taifa hili, hususan katika nyanja za kiuchumi kijamii na kiulinzi. Baadhi ya faida hizo ni kama ifuatavyo:-
    1. Kumtambua Mtanzania, mgeni na mkimbizi
    1. Kusidia katika kuongeza wigo wa ukusanyaji kodi ya Serikali kwa njia ya kuwatambua wachangiaji wengi zaidi
    1. Kuondoa wafanyakazi hewa katika Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara Serikalini
    1. Kusaidia suala la utambuzi hususan kwenye mabenki na hivyo kuwasaidia wananchi kupata mikopo kwa urahisi zaidi
    2. Continue reading →

No comments: