Thursday, October 10, 2013

MWAMBUSI: TUNAZIDI KUPAMBANA MPAKA KIELEWEKE, MASHABIKI WAIPE MUDA TIMU YAO, MAMBO MAZURI YANAKUJA MBELENI!!

mbeya-city-sept18-2013
                                Kikosi cha Mbeya City

Na Baraka Mpenja 

KOCHA wa klabu inayosumbua na kuumiza vichwa wa wanamichezo wengi kwa sasa nchini, timu bora ya Mbeya City, Mwalimu Juma Mwambusi amesema malengo yake kila anapoingia uwanjani ni kutafuta ushindi, lakini anaacha asilimia kadhaa ili matokeo ya mpira yaamua.

Akizungumza na Mtandao wa FULLSHANGWE mara baada ya kupata ushindi wa jana wa mabao 3-1 dhidi ya Rhino Rangers Uwanja wa A.H. Mwinyi mjini Tabora, Mwambusi alisema timu yake bado ni mpya, imepanda ligi kuu msimu huu, lakini kila wakati anajipanga kupambana kusaka pointi tatu muhimu na ndio maana wamekuwa wakipata matokeo mazuri wakiwa wahawajapoteza mchezo wowote mpaka dakika hii.

“Ligi ni ngumu na sisi ni wageni kwa sasa, tumefanya maandalizi ya mechi zote 26, kila timu tunayocheza nayo tunatarajia kushinda. Tumepata sare nyingi sana, ila kwa sasa tunashinda, tunamshukuru Mungu kwa hilo na tunaendelea kujipanga zaidi na zaidi”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi alisisitiza kuwa mpaka sasa wameshakutana na timu kubwa zenye uwezo mkubwa na majina makubwa kuliko wao wakiwemo Simba, Yanga, Kagera na wamehimili mikikimikiki, lakini kwasasa wanakutana na timu zenye uwezo kama wao, hivyo matokeo ni muhimu kabla ya kuelekea mzunguko wa pili ambao huwa na changamoto nyingi zaidi.

Kocha huyo mwenye historia ya mafanikio kila anapokabidhiwa timu mpya, aliwasifu na kuwapongeza mashabiki wa Mbeya ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakiiunga mkono timu toka inacheza ligi daraja la kwanza na mpaka sasa ligi kuu.

“Nawapa mkono wa hongera masbaiki wetu, wamekuwa pamoja na sisi na kuonesha umoja mkubwa, hakika wazidi kutitia moyo katika safari hii ya kusaka mafanikio. Lengo letu ni kuwapa raha kwa kufanya vizuri na ndio maana kila mechi tunapoingia uwanjani tunawafikiria wao kwanza”. Alisema Mwambusi.

Baada ya matokeo ya jana, Mbeya City wamejikusanyia pointi 14 sawa na Yanga, lakini wanazidiwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Akizungumzia mechi ijayo dhidi ya Mgambo JKT katika dimba la Mkwakwani jumapili (septemba 13), Mwambusi alisema hesabu zake ni kutafuta pointi tatu, huku akisema wapinzani wao wana uwezo unaoelekeana na wao tofauti na timu walizokutana nazo.

“Tunaelekea Tanga kusaka ushindi, na hayo ndio malengo yetu. Mara zote tuko tayari kushindani na timu yoyote inayoshiriki ligi kuu soka Tanzania bara, hivyo mashabiki wajiandae kupata burudani”. Alisema Mwambusi.

Mechi nyingine za jumapili zitawakutanisha Ashanti United dhidi ya Coastal Union, Azam fc watavaana na JKT Ruvu, Mtibwa Sugar watawakaribisha JKT Oljoro, wakati Ruvu Shooting watakula sahani moja na Rhino Rangers ya Tabora.

No comments: