Tuesday, November 12, 2013

KIUNGO MATATA STEVEN MAZANDA: MAANDALIZI YA MAPEMA YAMETUPA MAFANIKIO, NAPENDA VIJANA WANAVYOCHEZA SOKA KWA SASA!!

kikosi 
Kiungo jembe wa Mbeya City FC, Steven Mazanda (waliosimama, wapili kulia) amesema hawana presha na kasi ya timu pinzani, mzunguko wa pili wako fiti zaidi kuliko watu wanavyodhani !

Na Baraka Mpenja wa Kingotanzania

Kiungo wa Mbeya City, Steven Mazanda, amesema siri ya mafanikio ya kikosi chao katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara uliomalizika novemba 7 mwa huu na klabu hiyo kumaliza katika nafasi ya tatu kwa pointi 27 sawa na Azam fc katika nafasi ya pili ni maandalizi ya mapema waliyofanya pamoja na nidhamu kubwa ya wachezaji kuanzia uwanjani na nje ya uwanja.
“Unajua sisi tulijiandaa mapema sana, na ndio maana unaona kikosi kinacheza kitimu na kila mtu anavutiwa. Kiukweli kumekuwepo na changamoto za ushindani, lakini tunaingia katka kila mechi kuhitaji ushindi”. Alisema Mazanda.
Mazanda ambaye  amewahi kuzichezea timu za Tukuyu, Simba, Mtibwa na Kagera Sugar, kabla ya kuisaidia Mbeya City kupanda daraja ameongeza kuwa mzunguko wa pili hakika utakuwa mgumu kwao kwani timu nyingi zinajipanga kujiweka sawa katika msimamo.

“Kuna timu zitakuwa zinawania nafasi ya ubingwa, nyingine nafasi za katikati, wakati hatari zaidi itakuwa mkiani ambao klabu zitakuwa zinawania kukwepa mkasi wa kushuka daraja. Sisi tuko tayari kwa kupambana na hiyo ndiyo kazi yetu”. Alisema Mazanda.

 Kiungo huyo mwenye uwezo mkubwa wa kukaba, kupanda na kushambulia pia, ni mpigaji faulo mzuri amekiri kuwa vijana wamekuwa wakicheza soka safi sana na kuonesha juhudi zao, lakini kwa yeye aliyecheza soka kwa muda mrefu huwa hawampi  presha akiwa dimbani.

“Nafurahi sana kuona changamoto kubwa ya vijana wakiwa uwanjani, timu zote zinazotumia damu changa zinafanya vizuri sana, kiukweli hawa makinda wapewe nafasi ili sisi wakongwe tuwaoneshe jinsi mpira unavyochezwa”. Alisema Mazanda.

Mazanda alisema kwa sasa kazi yao ni moja tu ambayo ni kujiandaa kwa mzunguko wa pili na lazima kieleweke.

“Tulivyoanza, watu walisema nguvu ya soda, nadhani hata wewe mwenyewe ulisikia, lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda mbele, tulipata nguvu zaidi. Sasa ahadi yetu ni kuonesha soka la uhakika”. Alisema Mazanda.
Ingawa umri umeenda lakini uzoefu unaonesha kuwa  viungo huwa bora kwa jinsi umri unavyoenda.

No comments: