Saturday, November 9, 2013

UTPC YAANZA UTARATIBU WA KUTOA VYETI KWA WANACHAMA WA VILABU WANAOPEWA MAFUNZO MBALI MBALI


UMOJA  wa  klabu  za  waandishi  wa  habari Tanzania (UTPC) umeanza  utaratibu wa  kutoa vyeti  maalum kwa  wanachama  wa klabu  za waandishi wa habari nchini  ambao  wanapatiwa mafunzo mbali mbali.
 
Mkurugenzi  mtendaji  wa  UTPC Abubakar Karsan  alisema  kuwa  vyeti  hivyo  vimeanza  kutolewa  baada ya  maadhimio  ya wajumbe  wa mkutano mkuu .
Hivyo  alisema  kuanzia  sasa  wanachama  wa vilabu ambao  watapewa mafunzo wanachama  wake  watapewa vye vyeti maalum .
Pia  alisema  vyeti  hivyo vitakuwa vya  viwango  vya  juu na vinaanza  kutolewa  sasa kwa vilabu  hivyo.
 
Wakati  huo  huo umoja wa  vilabu  vya  waandishi  wa habari Tanzania (UTPC)  umewataka  viongozi wa  vilabu  hivyo  mikoani  kutumia changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao kujipanga  badala ya  kuzichukia changamoto  hizo.
 
Kauli  hiyo  imetolewa leo  jijini Mwanza na Rais  wa UTPC Kenneth  Simbaya  wakati akifungua mkutano  mkuu  wa  wanachama  wa klabu za  waandishi wa habari .
 
Simbaya  alisema  kuwa  mbali ya  kuwepo  kwa mafanikio makubwa katika klabu  vya waandishi  wa habari nchini ila  bado wapo baadhi ya viongozi ambao wameendelea kukwepa  changamoto  mbali mbali badala ya  kuzifanyia  kazi.

No comments: