Monday, January 6, 2014

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,SACP Ahmed Msangi ajitambulisha kwa waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya, atoa Taarifa ya matukio mbali mbali yaliyotokea kwa kipindi cha Mwaka 2013

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,SACP Ahmed Msangi akizungumza na waandishi wa habari wa Mkoa wa Mbeya (hawapo pichani) alipowaita kwa kuijitambulisha kwao na kutoa taarifa ya matukio mbali mbali yaliyotokea kwa kipindi cha Mwaka 2013.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,SACP Ahmed Msangi 

Baadhi ya waandishi wa habari wakiendelea kufuatilia mkutano na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Ahmed Msangi 

 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali jijini Mbeya wakimsikiliza kwa makini Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,SACP Ahmed Msangi (hayupo pichani).
WILAYA YA RUNGWE – AJALI YA GARI KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU 
                 [ASKARI] NA KUSABABISHA KIFO.
  
MAREHEMU SSGT BENADETHA BONIFASI OLOMI ENZI ZA UHAI WAKE
MNAMO TAREHE 05.01.2014 MAJIRA YA SAA 12:50HRS HUKO ENEO LA MBEYA ONE, KATA YA ISONGOLE, TARAFA YA UKUKWE, BARABARA YA MBEYA/TUKUYU WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA. ASKARI EX WP 1601 S/SGT BENADETHA, MIAKA 52, MCHAGA, ASKARI WA KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI TUKUYU WILAYA YA  RUNGWE, AKIWA KAZINI ENEO HILO ALIGONGWA NA GARI T.613 BUM AINA YA  TOYOTA CARINA LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA ERNEST S/O MATHAYO NDOA, MMAKUA, MIAKA 35, MKAZI WA KYELA NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO. CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI. DEREVA AMEKAMATWA NA GARI LIPO KITUO CHA POLISI TUKUYU. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED. Z. MSANGI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUFUATA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA. AIDHA ANATOA WITO KWA MADEREVA KUEPUKA MWENDO KASI KWANI NI HATARI NA UNAUA.
Signed by:
[AHMED. Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

No comments: