Thursday, February 20, 2014

MBEYA CITY leo yaelekea kuweka kambi MOMBASA kuikabili COASTAL UNION

MBEYA CITY2 be4b7
Wachezaji wa Mbeya City wakipanda ndege mchana jana Uwanja wa Ndege wa Songwe mkoani Mbeya kuelekea Mombasa, Kenya ambako watakaa hadi Jumamosi asubuhi watakapokwenda Tanga na jioni yake kucheza mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani.

......................................................

Mbeya City waanza mchakato wa ujenzi wa uwanja wao

mbeya-city-sept18-201311 537f5
TIMU ya Mbeya City ya Mbeya, ipo kwenye mchakato wa ujenzi wa uwanja wao na kushusha nchini kontena moja la jezi zao kutoka nchini China.
Mbeya City iliyopanda daraja msimu huu, kama ikifanikiwa kutimiza yote hayo basi kimaendeleao itazizidi klabu kongwe za Simba na Yanga ambazo hadi sasa hazina hata viwanja vya maana vya mazoezi.

Mwenyekiti wa timu hiyo, Mussa Mapunda anasema kuwa tayari wamenunua shamba la ekari 15 eneo la Iwambi, Mbeya ambalo wamelitenga kwa ajili ya kujenga uwanja mkubwa wa kisasa.

Anasema, tofauti na uwanja wamepanga kujenga hosteli za kisasa watakazozitumia wachezaji wa timu kubwa, pia kwa ajili ya timu zao za vijana kuanzia umri chini ya miaka 14 hadi 20 watakaowatumia siku zijazo.
Pia watatenga eneo lingine kwenye uwanja huo kwa ajili ya kituo cha michezo. Timu hiyo kwa sasa inatumia Uwanja wa Sokoine unaomilikiwa na CCM.

Akifafanua kuhusu kuingiza nchini kontena moja la vifaa vya michezo kutoka China ambalo litakuwa na jezi, suti za michezo, kofia, skafu, bendera na soksi. Vitu hivyo vitauzwa nchini kote pamoja na nchi za Malawi na Zambia. ......................................................

No comments: