Tuesday, February 4, 2014

Utafiti wa Afya: Ngono ya mdomo ni hatari

kansa1 74ce1
Leo ni siku ya Saratani Duniani. Wakati tunaadhimisha siku hii hapa nchini idadi ya vijana ambao ni tegemeo la taifa inazidi kupungua kutokana kuangamia kwa saratani ikiwemo ya koo. 


Utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini umeonyesha asilimia 20 ya saratani ya koo husababishwa na ngono ya mdomo maarufu kama 'Oral Sex".

Utafiti huo unaonyesha saratani ya koo licha ya kuambukizwa na njia mbalimbali ikiwemo ulaji wa vyakula vyenye pilipili,pombe kali, vitu vyenye uchachu pamoja na kurithi kutoka kwa wazazi.
Utafiti unaonyesha watu wengi hasa vijana wanamejiingiza kwenye vitendo hivi vya kufanya ngono wakitumia midomo hasa ndimi, hivyo kuhatarisha uhai wao.

Katika utafiti huo wa hivi karibuni, ulibaini wanaume 747 na wanawake wakiwa 472 hugundulika kila mwaka kuwa na saratani hiyo huku wanaopoteza maisha kila mwaka ni wanaume 444 wakifuatiwa na wanawake 270 kutokana na ugonjwa huo.

Utafiti unabainisha kuwa asilimia kubwa ya vijana wenye umri kati ya miaka 20 hadi 45 wanatumia staili ya kuwanyonya wenza wao sehemu za siri lengo likiwa ni kuwavutia wapenzi wao katika kushiriki ngono.

Vijana wenye umri huo ndio wahanga wakubwa kwa sasa kutokana na ugonjwa huo kuonekana kuwaathiri kwa kasi, huku wengi wakiwa hawajui athari zake. Baadhi hujisifia kwamba ni wajuzi, kumbe wanajitafutia kifo kwa kufanya vitendo hivyo.

Utafiti unaonyesha kwa watu wazima walio wengi hawana muda wa kufanya hayo wanayofanya vijana, hivyo kujikuta angalau wanakuwa salama na kupatwa na saratani ya koo kwa njia hiyo inayoonekana kama ni chafu pia.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk Crispin Kahesa anasema saratani ya koo ni ya pili katika mtiririko wa saratani zinazowapata wanaume nchini, ikiongozwa na ile ya ngozi (Karposi's Sarcoma) ambayo huambukizwa kwa njia ya kujamiana. Kuna saratani aina zaidi ya 24 zinazoisumbua Tanzania.

Anasema mbali na staili hiyo pia, kuna baadhi ya watu hupata saratani ya koo kwa kurithi kutoka kwa wazazi wao na wengine kuwa na umri mkubwa ambao huchangia kupata tatizo hilo, lakini siyo kwa asilimia kubwa kama ile ya ngono ya mgomo.

"Hali hii ya vijana wenye umri huo kuwanyonya wanawake inatokana na ujana, wengine wanaiga kwenye mitandao, lakini mambo haya hayakuwepo zamani tofauti na sasa, utakuta wanaume ili aweze kumvutia mwanamke anamfanyia hivyo sehemu za siri, lakini zamani staili hii haikuwepo kabisa," anasema Dk Kahesa na kuongeza.

"Kuna njia nyingi tu za kumvutia mwanamke lakini siyo hii bila kujua madhara yaliyopo, vijana wengi nchini wanaona njia rahisi ya kupendwa na mwanamke ni hiyo wakati kuna njia nyingi za kufanya. Nje ya hiyo wanawake wengine huwa na magonjwa mbalimbali, kwa jumla hakuna usalama wowote kwa wanaume kufanya kitendo hicho,"anaongeza

Sababu nyingine zaidi
Anasema staili ya maisha nayo imechangia kuongezeka kwa ugonjwa huo, vijana wengi kwa sasa hutumia muda mwingi kuangalia video za ngono na staili zinazofanywa na wenzetu wa nje na hivyo kuongezeka kwa matumizi ya ngono ya mdomo.

Dk Kahesa anasema asilimia 12 ya wagonjwa wote wa saratani nchini wanasumbuliwa na saratani ya koo, hivyo kuna kila sababu kwa vijana kubadilisha tabia na kuepuka kuiga mitindo ya wenzetu wazungu ambayo mara nyingi inapotosha mila na tamaduni za Kiafrika.

Anasema katika mtiririko wa saratani zinazoongoza nchini saratani ya koo inashika nafasi ya tano, wagonjwa wengi wanaopatwa na ugonjwa huo ni watu wenye umri mkubwa wa miaka 60 na kuendelea hiyo inaonyesha kuwa wengi wao walianza ngono ya mdomo muda mrefu wakati wakiwa bado wadogo.

"Asilimia kubwa ya wagonjwa wanaopatikana na kansa ya koo nchini, inawapata watu wenye umri wa kuanzia miaka 60 na kuendelea kutokana na wengi wao kuanza mapema vitendo vya ngono kwa njia ya mdomo wakati bado wadogo au wengine kurithi kutoka kwa wazazi wao," anasema Dk Kahesa.

Aina ya kansa ya koo
Tafiti zinaonyesha kuna aina mbili za saratani ya koo; aina ya kwanza ni "Oesophagus Carcinoma na Squamous cell carcinoma, zote hutofautiana wakati zinapimwa kwenye darubini lakini
Dalili za saratani ya koo

Moja kati ya dalili za mgonjwa wa saratani ni chakula kukwama kwenye koo, siku za mwanzo mgonjwa anaweza kushindwa kumeza chakula kigumu kisha cha majimaji na baadaye akashindwa kumeza hata mate.

Ugonjwa huo unachukua muda mrefu kugundua na kuona viashiria kwani mwanzo mgonjwa huanza kupata shida kumeza chakula na kwamba wagonjwa wengi wanaofika katika Taasisi hiyo ya Saratani wanakuwa tayari wamechelewa kwani wanakuwa katika hatua ya mwisho.

"Unaweza usionyeshe dalili lakini kadri siku zinavyokwenda ndiyo kunakuwa na dalili zinajitokeza pia katika kipindi hicho mtu anakuwa na maumivu wakati wa kumeza chakula, maumivu katika kifua na mgongo na hata kupungua uzito pamoja na kikohozi kikavu kinachoweza kudumu mwezi mmoja," anasema.

Njia ya kuzuia saratani ya koo.
Kwanza mtu mwenye ugonjwa huo anapaswa kuhawi hospitali ili aanze matibabu mapema kutokana na ukweli kwamba mgonjwa anayewahi kupata matibabu ana uwezekano wa kupona kuliko yule ambaye amechelewa kugundulika na kuanza matibabu.

Kama saratani hiyo itakuwa imeshambulia viungo vyote vilivyopo jirani na koo na hadi kufika katika tezi au kiungo kingine cha mwili, mgonjwa anaweza kutibiwa kwa njia ya upasuaji, kutumia mionzi na hata kifaa maalumu ambacho ni kemikali.

Tafiti zilizofanywa nchini
Wataalamu mbalimbali nchi wamefanya tafiti zinazohusiana na ugonjwa huo na kusema kuwa kati ya mwaka 1983 hadi 1992 kulikuwa na kati ya watu 546 waliopimwa, wanaume 430 na wanawake 116 waligundulika kuwa na ugonjwa huo.


Utafiti huo ulishirikisha watu wenye umri wa miaka 21 hadi 90, ulibaini kuwa wagonjwa wengi walikuwa wenye umri wa miaka 50-59 tofauti na hali iliyopo sasa ugonjwa wa kansa ya koo unawaathiri vijana wenye umri wa miaka 40.

Dk Kahesa anasema katika kipindi cha miaka saba iliyopita takwimu za taasisi yake imeongezeka kutoka kutoka wagonjwa 167 hadi kufikia wagojwa 277. Hali inaonekana huenda ikaongezeka kutokana na ukweli kwamba wengi wa watu wanaonekana kuendeleza tabia hatarishi zikiwemo hizo za kutumia midomo.

Magonjwa mengine sehemu za siri
Miongoni mwa magojwa ambayo yanaweza kumpata mtu ambaye ananyonya au kulambana sehemu hizo ni pamoja na gonjwa wa gonoreha, ambapo ugonjwa huu huanzia katika koo na mwanzoni huhisi kama ni ukavu wa kifua au maradhi ya kawaida ya kifua, ila baadaye hushuka na kuelekea katika viungo vya uzazi.

Ugonjwa mwingine ni kaswende ambao huambukizwa kirahisi zaidi kupitia mdomo na hasa pale inapotekoa mdomo unapokutana na kiungo chenye athari hizo.

Vile vile ugonjwa wa chlamydia ni moja wapo kati ya magonjwa ya zinaa ambao huambukizwa kwa bakteria na kwamba ugonjwa huu pia huambukizwa kupitia mdomo, ingawa waathirika wanaweza wasijijue maana huwa hauna dalili kwa muda mrefu.

Hepatitis A: Hiki ni ni kirusi kinachopatikana katika kinyesi cha binadamu, kirusi hiki huwaingia wale wanaopenda kunyonya na kulambana sehemu za haja kubwa. Ni kwamba kwa ugonjwa huu mtu anaweza akaharibika macho hadi kupofuka.

Hepatitis B: Ugonjwa huu huambukizwa kama virusi vya Ukimwi kwa sababu virusi vyake hukaa katika majimaji yanayotoka katika sehemu za siri na damu. Mtu akiwa na ugonjwa huu, mwili wake unakuwa na vipele vingi na hata majipu ambayo huwa magumu kupona na wapo wanaokufa.
Vile vile ugonjwa wa Hepatitis C: ni ugonjwa ambao hupatikana pindi damu

inapotoka maana vijidudu vyake vinakaa katika damu. Ugonjwa huu humfanya mtu kuvimba viungo na hata kukatika.

Hata hivyo kupitia staili hii yaupeana raha kwa kunyonyana sehemu za siri, kuna uwezekano wa kupata maambukiz ya virusi vya Ukimwi kwa uchache lakini kwa nchi zilizoendelea wamebuni aina ya kondom ambazo huvaliwa katika mdomo wa binadamu na hivyo kupunguza hatari ya kupata madhara hayo.

JE NGUVU ZA KIUME ZINACHANGIA?
Dk Kahesa anasema hakuna utafiti wa moja kwa moja unao onyesha kuwa baadhi ya wanaume wanaofanya ngono kwa njia ya mdomo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume.

"Utafiti wa mtu mmoja hautoshi kuonyesha kuwa baadhi ya wanaume wanafanya ngono kwa njia ya mdomo wanakuwa na ukosefu wa nguvu za kiume, hivyo kinachotakiwa ni kufanya utafiti wa kina ili kubaini kama tatizo hilo lipo licha ya kuwepo kwa kesi nyingi zinazodaiwa kuwa baadhi ya wanaume hawana nguvu za kiume na wapenzi wao huwafichia siri kwa kufanya nao mapenzi kwa njia yam domo"anasema.

NINI KIFANYIKE:
Wataalamu wa masuala ya ndoa na saikolojia wanasema kuna njia nyingi za kuandaana wakati wa tendo la ndoa tofauti na kunyonyanyana sehemu za siri.
Wataalamu hao wanasema sio sahihi kwa mwanaume au mwanamke kunyonyana sehemu za ndoa mwenzake na kwamba staili hizo ni staili za wanzetu wa nje lakini kitu kinachosababisha kukua kwa kasi kwa staili hiyo ya kunyonyonyana sehemu za siri au kufanya mapenzi kwa njia ya mdomo ni kutokana na kasi ya utandawazi.

Wadadisi wa mambo wanadai kuwa baadhi ya watu huiga staili hizo kutoka katika mitandao bila kujali kuwa kuna zina madhara makubwa, hivyo ni jukumu la kila mtu kulinda afya yake na ya mwenza wake.

Sio kila kitu kinachowekwa katika mitandao ya kijamii kina manufaa la hashaa! vitu vingine vinachangia kuhatarisha maisha. Chanzo: mwananchi

 

 ..............................

SERIKALI YASEMA HAINA UGOMVI NA VYOMBO VYA HABARI.

IMG_4746
Frank Mvungi- Maelezo
Serikali imesema haina Ugomvi na vyombo vya habari hapa nchini kama ambavyo baadhi ya vyombo
hivyo vimekuwa vikiripoti.
Akizungumza leo katika ufunguzi wa mkutano wa Maafisa Habari na Mawasiliano  wa Serikali Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara alisema haoni sababu ya kuingia kwenye ugomvi na wadau muhimu kama vyombo vya habari.
“Kuna wanaozunguka zunguka wakieleza kwamba kuna ugomvi kati yetu na vombo vya habari, mkiwasikia wapuuzeni”.alisema waziri Mukangara.
Dkt Mukangara alipongeza kazi nzuri inayofanywa na vyombo vya habari na kuvitaja kuwa wadau muhimu wa Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kutoa taarifa.
Dkt.Mukangara aliongeza kuwa ni jukumu la Maafisa Habari na Mawasiliano kuwaunganisha wananchi na Serikali kwa kutoa taarifa zitakazowasaidia wananchi kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Akifafanua zaidi Dkt. Mukangara amesema kuwa Wizara itaendelea kuratibu mikutano ya Taasisi za Serikali na Vyombo vya Habari ili kuwapa wananchi fursa ya kujua mambo mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali.
Katika Utaratibu huo  Dk Mukangara amesema mikutano 156 kati ya taasisi za Serikali na Vyombo vya Habari ilifanyika  kati ya 204 iliyotarajiwa kufanyika katika kipindi cha julai hadi Desemba 2013 ikiwa ni utekelezaji wa jukumu la msingi la kuwapa wananchi taarifa kwa wakati.
Pia aliwaasa Maafisa Habari na Mawasiliano kote nchini kujituma na kufanya kazi kwa weledi ili kuwasaidia Taifa kufikia maendeleo endelevu.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel Alibainisha kuwa Mafunzo kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii katika kuimarisha mawasiliano ya Serikali kwa umma.,mafunzo ya vitendo kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii na mada kuhusu namna bora ya kutumia na kuendesha radio za kijamii.
Kauli mbiu ya Kikao kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano zaidi ya 100 toka Tanzania nzima ni Matumizi ya Tehama na Mitandao ya Kijamii katika kuimarisha Mawasiliano ya Serikali kwa umma.

No comments: