Thursday, March 20, 2014

MWIGULU NCHEMBA AHUTUBIA BUNGE LA ACP NA EU,APINGA NDOA YA JINSIA MOJA,WABUNGE WAMUUNGA MKONO

Naibu Waziri wa Fedha  mhe Mwigulu Nchemba amehutubia kikao cha pamoja cha bunge la ACP na EU katika mji wa Strasbourg nchini Ufaransa.
 
Katika hotuba yake, mhe Mwigulu alianza kwa kukishukuru chombo hicho kwa ajili ya msimamo wake usioyumba kwenye maswala ya amani akitolea mfano wa kazi nzuri waliofanya kwenye swala la Jamhuri ya Afrika ya Kati na Sudani  Kusini. Mhe Mwigulu aliitaka Jumuiya ya Kimataifa imsaidie Rais wa muda Mama Carthrine Samba Panza ili kuwezesha kipindi cha mpito na maridhiano kuwezesha zoezi la uchaguzi huru na wa haki. 
 
Kuhusu maswala ya kiuchumi mhe Mwigulu aliwakumbusha wajumbe wa bunge hilo  kuwa umebaki mwaka mmoja tu kumalizia mpango wa malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDG’s). Mhe Mwigulu aliitaka  Jumuiya ya kimataifa kuhakikisha kuwa mpango wa maendeleo baada ya 2015 unalenga nguzo  tatu mhimu akizitaja kuwa  kijamii, kiuchumi na Mazingira.  
 
Kuhusu kiuchumi na Kijamii mhe Mwigulu alisema kuna umhimu sasa wa kuhakikisha malengo yanalenga sector zinazogusa na kubadilisha maisha ya watu wachini na masikini. ‘Tumekuwa na kipindi cha kutosha kushughulikia uchumi mkubwa , tumefanikiwa sana, ila maeneo mengi sekta zilizokuwa hazigusi maisha ya mtu masikini na hazitengenezi ajira kwa watu masikini’  hivyo malengo yamekuza uchumi na kuongeza pengo kati ya watu masikini na watu matajiri.
Ni kiu yangu kuona agenda ya baada ya 2015 inalenga kuwainua masikini kwa kulenga sekta zinazogusa maisha ya watu masikini na kutengeneza na kubooresha fursa kwenye sekta zinazogusa watu wengi. Umhimu huo pia utolewe kwenye swala la mazingira kwani mazingira yanaathiri zaidi shughuli za mtu wa hali ya chini.
 
Mhe Mwigulu alisisitiza kuwa kuna uhitaji mkubwa zaidi wa kuendeleza sekta binfsi kwa kutengeneza sekta binfsi inayolenga ujasiliamali zaidi na kutengeneza elimu ya kujiajri. Kwa sasa misaada mingi inalenga elimu ya siasa na haki za binadam. “Elimu nzuri zaidi ni ya kujiajiri na haki  mhimu zaidi ni ya kuishitena maisha bora” kama tunasaidia kuelimisha uraiani tusaidie kulimisha ujasiliamali, ubunifu wa miradi, uendelezaji miradi, biashara na kutambua fursa. Misaada ilenge kutambua fursa za uzalishaji, kuwekeza kwenye sekta za uzalishaji na kutambua masoko. Mhe Mwigulu alisema, soko la Ulaya limekuwa likiathiri sana mazao ya Afrika kwa bei kutokutabirika na bei kuyumba sana. Mafia makubwa yanalinda wakulima wao na yanazuia mataifa madogo kulinda wakulima wao. 
Mataifa makubwa yanalinda mazao ya wakulima wao kwa kuwahakikishia masoko lakini yanawapambanisha na  wakulima wa mataifa madogo wasiokuwa na ruzuku ya kutosha na wanaopangiwa bei za chini kwa mazao yao. Tukiamua kuinua maisha ya mkulima masikini wa Afrika, tufute wimbo wa kushuka kwa bei za mazao yake ktk soko la Dunia huku wakulima  wa mataifa makubwa wakiwa wamepata hifadhi.
 
Katika hatua nyingine Mwigulu aliitaka Jumuiya ya kimataifa kufikia mwisho kwenye Economic Partnership Agreements kwa kanda ambazo hazijakamilisha kwani limekuwa jambo la muda mrefu. Wanajua kinachokwamisha, wafike mahali wayasikilize na matakwa ya mataifa madogo kama kweli lengo la makubaliano na nia ni kuyanufaisha mataifa madogo ili yaendelee. Alitambua kuwa Afrika Magharibi wamepiga hatua, lakini kwa EAC na SADC mnatambua mahitaji yetu, tusikilizeni. “there can be no celebration in reaching a deal for the sake of it and thereafter, encounter problems with its implementation”. Serikali zitapoteza mapato kutokana na kupungua au kuondolewa kwa tarrifs kuathiri   sana utoaji wa huduma kwa jamii, hivyo nivyema tukajua hizi  Economic Partnership Agreements zinachangia vipi kuyafikia Malengo ya Milenia.
 
Baada ya hotuba hiyo ya dakika 15 ulikuja wakati wa maswali ya papo kwa papo ya dakika 15 ambayo wajumbe wa ACP –EU waliuliza maswali na alijibu kwa ufasha kama

No comments: