Thursday, April 3, 2014

UEFA: PSG YAITUNGUA 3-1 CHELSEA, REAL MADRID YAPIGA MTU 3-0, RONALDO ASAWAZISHA REKODI YA MESSI!!

BEKI wa Chelsea, David Luiz amejifunga bao na kuwanufaisha zaidi Paris Saint-Germain katika ushindi wa nyumbani wa mabao 3-1 usiku huu katika mechi ya kwanza ya robo fainali,  ligi ya mabingwa barani Ulaya.
 Lavezzi alianza kufunga karamu ya mabao kwa PSG katika dakika ya 4 ya kipindi cha kwanza. Dakika ya 27, Hazard aliisawazishia Chelsea bao hilo kwa njia ya mkwaju wa penati na kwenda mapumziko matokeo yakiwa  1-1.
Kipindi cha pili, nyota ya mabingwa wa Ufaransa iliendelea kung`ara ambapo dakika ya 62, David Luiz alijifunga na kuufanya ubao wa matokeo usomeke 2-1.
Wakati Chelsea wakihaha kutaka kusawazisha bao hilo, dakika ya 90 ya mchezo, Javier Pastore aliandika baoa la tatu na kuwanyamazisha ghafla mashabiki wa wazee wa darajani.
Baada ya kumalizika kwa mechi hiyo, Kocha wa Chelsea alisalimiana isivyokuwa kawaida yake na  benchi la ufundi la PSG, lakini haijajulikana kama amewakubali sana au vipi.
Zilisalia dakika 28 pekee kwa Chelsea kutoa sare, lakini bao la kujifunga la Luiz liliwachanganya na kubadili upepo wa mchezo. Na kabla ya hapo walikuwa wamejiamini kufanya vizuri.
Kikosi cha PSG: Sirigu 6, Jallet 6.5, Alex 6.5, Thiago Silva 6, Maxwell 6.5, Verratti 6 (Cabaye 76), Thiago Motta 6.5, Matuidi 6.5, Cavani 7, Ibrahimovic 6 (Lucas Moura 68), Lavezzi 8 (Pastore 84).
Kikosi cha Chelsea: Cech 5.5, Ivanovic 6, Cahill 6, Terry 6, Azpilicueta 6, Ramires 6, Luiz 6.5, Willian 6.5, Oscar 6 (Lampard 72), Hazard 7, Schurrle 5 (Torres 59).
Not in the plan: John Terry, David Luiz, Petr Cech and Cesar Azpilicueta look dejected after Chelsea concede a second
Majanga: John Terry, David Luiz, Petr Cech na Cesar Azpilicueta wakiduwaa baada ya kujifunga bao la pili
Oh no! Luiz can't get out of the way of the ball as it hits him and goes in
Oh hapana! Luiz hakuweza kuuzuia mpira usizame nyavuni
Back of the net: Luiz ends up in the goal along with the ball after PSG go 2-1 up
 Kufungwa kubaya, cheki Luiz anavyoshangaa baada ya kuwafungia PSG bao la pili usiku huu
Leaving it late: Javier Pastore celebrates after scoring his sides third
Msumari wa mwisho: Javier Pastore akishangilia bao la tatu usiku huu
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA CHINI

No comments: