Monday, May 19, 2014

Taratibu za msiba wa adam kuambiana KIFO CHAKE " alisema muda mchache kabla ya kufikwa na mauti, Kuambiana alimlalamikia maumivu ya tumbo ambapo Ijumaa iliyopita alisema hali yake si nzuri kwani alikuwa akiendesha damu tupu"

k_edb32.jpg
Marehemu Adam Kuambiana ataagwa siku ya jumanne (20/5/2014), katika viwanja vya Leaders Club, kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 9 mchana. Baada ya hapo atazikwa siku hiyo hiyo ya jumanne, katika makaburi ya Kinondoni.

Mwenyekiti wa Bongo movies, Steve Nyerere, amesema marehemu alikuwa anasumbuliwa na vidonda vya tumbo na ndio chanzo cha kifo chake.

HIKI NDICHO KILICHOMUUA MSANII WA FILAMU ADAM KUMBIANA

Msemo huu umetimia juzi kufuatia kifo cha ghafla cha mwigizaji na mwongozaji wa filamu za Kibongo, Adam Philip Kuambiana (38) kilichotokea akiwa njiani kukimbizwa kwenye Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar es Salaam baada ya kuugua.
Mwili wa Adam Kuambiana ukipelekwa Hospitali ya Muhimbili. 
Kuambiana aliugua ghafla kwenye kambi ya kurekodi filamu na wasanii wenzake iliyopo katika Nyumba ya Kulala Wageni ya Silvarado iliyopo Sinza ya Kwaremmy, Dar.
NINI CHANZO CHA KIFO?
Akizungumza na Ijumaa Wikienda Jumamosi iliyopita nje ya Hospitali ya Mama Ngoma, msanii wa Bongo Fleva, Aboubakar Katwila ‘Q-Chillah’ alisema muda mchache kabla ya kufikwa na mauti, Kuambiana alimlalamikia maumivu ya tumbo ambapo Ijumaa iliyopita alisema hali yake si nzuri kwani alikuwa akiendesha damu tupu.
Mmoja wa wasanii aliyekuwa katika harakati za kushuti video na Adam Kuambiana akilia kwa uchungu. 
 Q-Chillah alisema: “Jana (Ijumaa) jioni Kuambiana na wasanii wenzake walikuwa baa wakinywa pombe hadi usiku mnene lakini bado aliendelea kulalamikia maumivu ya tumbo.
“Wenzake walimuuliza ni kwa nini alikuwa akiendelea kunywa pombe kama anaumwa? Akawaambia wamuache!
“Baada ya kumaliza kunywa kila mmoja alikwenda kulala chumbani kwake huku tukiahidiana kwamba itakapofika saa 3:00 asubuhi tuwe tayari kwa ajili ya kwenda ‘location’.
“Lakini ulipofika muda huo sisi tukiwa tayari kwa safari tulikwenda kugonga mlango wa chumba chake bila mafanikio.

Yobnesh Batuli akiwa na simanzi nzito.
 “Cha kushangaza, alisikika sauti yake kwa mbali. Kwa bahati nzuri mlango ulikuwa wazi, mmoja akaingia ndani na kumkuta ameanguka chooni na hajiwezi. Neno lake la mwisho alisema kwamba anajisikia kuishiwa nguvu na anaharisha damu.
“Kutokana na hali yake hiyo mbaya tulimbeba na kumlaza kitandani kisha tukatafuta gari na kumkimbiza Hospitali ya Mama Ngoma ambapo daktari alisema kwamba alishafariki dunia muda mrefu.”

 
Rais wa Bongo Muvi, Steve Nyerere (katikati) na Mtitu wakiwa katika hali ya majonzi.
 VIDONDA VYA TUMBO VYATAJWA
Kwa mujibu wa watu wa karibu, Kuambiana kwa muda mrefu amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa vidonda vya tumbo (ulcers). Lakini pia inadaiwa alikuwa akisumbuliwa na kisukari (diabetes).
DAKTARI AELEZEA
Ijumaa Wikienda lilimtafuta daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (aliomba jina kuhifadhiwa) ili azungumzie kuhusu vidonda vya tumbo, alisema:
“Kwa kawaida, mtu kuharisha damu kwa sababu ya vidonda vya tumbo inawezekana kabisa, hiyo kitaalam inaitwa heamatemesis. Inatokana na perforation ya tumbo yaani kidonda kuwa kikubwa.
“Kwa mtumiaji wa pombe ni kipindi anatakiwa kusimama au kuacha moja kwa moja. Kama hatajali afya yake anaweza kufa ghafla kwani uwezekano wa utumbo kukatika ghafla ni mkubwa.”
ALIJUA KIFO CHAKE
Q-Chilla ambaye ni miongoni wa wasanii wanaocheza filamu hiyo, aliendelea kusema kuwa siku chache kabla ya kifo, Kuambiana alimwambia filamu yake hiyo inayoitwa Jojo ndiyo ya mwisho, hatajishughulisha tena na sanaa na alikuwa na mpango wa kwenda China kupumzika kwa muda mrefu.

Ni simanzi na majonzi. 
“Nimeumia sana kwani hii filamu ndiyo ilikuwa apate fedha nyingi sana kwa sababu ni ya kwake mwenyewe na ni kali mno, amecheza vizuri akinishirikisha mimi.
“Lakini ndiyo hivyo tena imeishia katikati, sijui ni nani atakayeiendeleza maana mwenyewe katuachia majonzi yasiyoelezeka,”alisema Q-Chillah.
AMEMFUATA MDOGO WAKE
Habari zaidi zinasema kwamba, Kuambiana ameaga dunia hata arobaini ya mdogo wake wa damu, Patrick haijafika. Patrick alifariki dunia mwezi mmoja uliopita.
AKUTANA NA MHARIRI WA GLOBAL
Ijumaa saa 10:00 jioni maeneo ya Sinza Kwaremmy jirani na Silvarado, Kuambiana alikutana na Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa ya Global Publishers, Oscar Ndauka.
Mhariri huyo alimuuliza ni kwa nini hawaonani siku hizi, Kuambiana akajibu:
“Nipo Mr Ndauka, nipo bwana. Tutaonana lakini sina hakika sana.” Kuambiana alionekana mwenye afya njema na alimtania mhariri huyo kwa kumwambia: “Naona siku hizi Ndauka unazidi kunenepa tu, mi maisha yananipiga.”

Msanii Sandra akilia kwa uchungu.
 STEVE NYERERE, BATULI WALIA SANA
Baada ya taarifa kuenea, wasanii mbalimbali wa filamu walikusanyika katika Hospitali ya Mama Ngoma ambapo Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ walivunja rekodi ya kulia kufuatia kifo hicho.

WADAU WAZUNGUMZIA MTU KUANGUKA CHOONI

Wadau na mashabiki wa filamu waliokuwa eneo hilo walisikika wakisema kwamba wasanii wengi hawana tabia za kucheki afya zao, jambo ambalo linawagharimu kiasi cha kupoteza maisha.
Wengine walisikika wakisema kwamba watu wanaoanguka chooni mara nyingi huwa hawaponi, wakipona huwa wanapooza miili.

Mke wa marehemu Adam Kuambiana, Janeth Rithe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kunduchi akifarijiwa. 
 “Unajua watu wengi wanakosea, pale mtu anapodondoka chooni wanamkimbiza hospitali badala ya kumtibu kienyeji, mtu akianguka chooni tu anatakiwa kupewa ndizi mbivu lakini akipelekwa hospitali lazima afe,” walisikika watu. HISTORIA YAKE KWA UFUPI Marehemu Kuambiana alizaliwa mwaka 1976, Ifunda mkoani Iringa. Kabila ni Mmakua wa mkoani Mtwara.
Marehemu Kuambiana anatarajiwa kuzikwa kesho kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.

No comments: